Facebook Comments Box

Tuesday, September 16, 2014

YAYA TOURE AINGIA UWANJANI NA BINTI ALIEVAA HIJJAB


Yaya Toure na Aisha
Aisha Dalal amekuwa msichana mdogo wa kwanza wa Kiingereza (Mascot) kuingia na wachezaji mpira Uwanjani akiwa amevaa Hijabu katika ligi kuu ya Nchini Uingereza.

Aisha aliyekuwa ameshikwa mkono na nyota wa mchezo huo Yaya Toure wakati wa kuingia uwanjani ilikuwa ni mechi baina ya timu za Manchester City na Liverpool iliyochezwa Agosti 26 mwaka huu. Matokeo ya mechi hiyo Man city walishinda 3-1.

"Ilikuwa ni kupata uzoefu kwangu na nilifurahia sana siku hiyo", alisema Aisha kuliambia Gazeti la Lancashire Telegraph.

"Wachezaji walikuwa marafiki mno kwetu na kutufanya tujisikie kama tupo nyumbani", alisema Aisha ambaye alikuwa na kaka yake mdogo aitwaye Khalil aliyeshikwa mkono na Samir Nasir wakati wa kuingia Uwanjani.
Aisha anasema walikuwa na bahati kwa kuwa waliruhusiwa kuchagua wachezaji waliotaka kuingia nao Uwanjani. 

Anasema kaka yake Khalil alichagua kuingia Uwanjani na Samir Nasri kwa kuwa ndiye mchezaji anayempenda na yeye alimchagua Yaya Toure.

Anaendelea kuhadithia Aisha kwamba Yaya Toure alikuwa mtu mzuri sana kwake kwani kabla ya kuingia alikuwa akimtoa woga kutokana na kelele kubwa za mashabiki.

Aisha anasema kuvaa kwake hijabu kulikuwa ni jambo muhimu sana na alijisikia ujasiri kufanya hivyo kwani hakuna aibu katika kudhihirisha imani yako popote pale ulipo.
 


SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 16 SEPTEMBA 2014 HAPA

1_fca7e.jpg
2_62d68.jpg
3_358bf.jpg
4_e0b64.jpg
05_5c20c.jpg
5_b1143.jpg
10_1c8d4.jpg
11_683c8.jpg
20_89244.jpg
21_3fdc6.jpg
0022_b6a54.jpg
22_f06c5.jpg
23_5b7bf.jpg
24_ba0fe.jpg
25_21e3d.jpg
26_fc639.jpg
27_f3c8e.jpg
28_195a7.jpg
29_4386d.jpg


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU