Facebook Comments Box

Sunday, July 7, 2013

PICHA ZA PAMBANO LA WABUNGE WASHABIKI WA YANGA NA WABUNGE WASHABIKI WA SIMBA

Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua…
Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua Yanga.picha zote na GPL


KOCHA WA AZAM ASEMA HAMTAKI KASEJA: MAKIPA ALIO NAO WANATOSHA

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amekiri Juma Kaseja ni bonge la kipa, lakini amesema kwamba sasa anataka Aishi Manula na Mwadini Ally wapambane kuwania nafasi ya kipa wa kwanza wa timu na hana mpango wa kusajili kipa mwingine.
Muingereza huyo amesema kipa wake mwingine, Jackson Wandwi anampeleka kucheza kwa mkopo Ashanti United ya Ilala iliyopanda Ligi Kuu msimu huu, ili kukusanya uzoefu baadaye arejee kushindana na Mwadini na Aishi.
Hatumuhitaji Kaseja; Stewart Hall kulia akiwa na Msaidizi wake, Kali Ongala

“Najua Kaseja ameachwa Simba SC, na nasikia watu wanamzungumzia sana wakimhusisha na Azam. Mimi nakubali yule ni kipa mzuri na ana uzoefu. Ila mimi nina makipa wazuri wawili, Aishi na Mwadini. Nataka hawa wagombee kuwa kipa wa kwanza wa timu,”alisema.
Hall amesema kwamba bado Azam ina makipa wengine wazuri wa timu za vijana, ambao watakuwa wakipewa nafasi ya kujifua na kikosi cha kwanza msimu ujao.
“Kama nitakuwa na Aishi na Mwadini kama makipa wawili imara wa timu ya kwanza, maana yake Wandwi ataendelea kuua kiwango chake. Nimeona bora nimpeleke Ashanti ili akakusanye uzoefu, baadaye arejee kwenye timu akiwa imara,”alisema.
Azam wakiwa mazoezini ufukwe wa Coco Dar es Salaam jana. Wandwi (katikati) anapelekwa kwa mkopo Ashanti United.

Aidha, kuhusu maandalizi ya msimu mpya, Hall amesema kwamba kwa sasa Azam ambayo itaiwakilisha Tanzania kwa mara ya pili mfululizo kwenye Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, iko katika mazoezi.
“Tunaendelea na mazoezi ya msimu mpya. Kwa sasa tupo katika programu ya ufukweni na gym. Baada ya hapo tutaanza programu rasmi ya uwanjani. Lakini wiki mbili za mwanzo za Agosti tutakwenda Afrika Kusini kuweka kambi,”.
“Tukiwa huko tutafanya mazoezi katika Uwanja mzuri na kupata mechi nne za kujipima nguvu dhidi ya timu kama Orlando Pirates, Kaizer Chiefs, Mamelodi Sundwons na nyingine,”alisema

Endelea kusoma hapa 

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU