Facebook Comments Box

Tuesday, October 9, 2012

MAJAMBAZI YAKAMATWA KWA CCTV BAADA YA KUIBA KWENYE M-PESA




JANET JACKSON NDANI YA HIJJAB



Pop star Janet Jackson mwenye umri wa miaka 46 ambae ni mpenzi wa zamani wa producer Jermain Dupri anaolewa mwaka 2013 na tajiri bilionea wa kiarabu Wissam Al Mana na inaaminika kwamba Janet itabidi abadili dini na kuwa muislam

YANGA WALALA TENA MZUNGU WA NNE

HISTORIA ya wachezaji wa Yanga kulala mzungu wa nne imejirudia tena Bukoba, baada ya kulala kwa kubanana katika kitanda kimoja kama ilivyokuwa Mbeya, licha ya kufikia katika Hoteli ya Smart, yenye hadhi kubwa.

Hali kama hiyo ilijitokeza wakati timu hiyo ikijiandaa kucheza na Prisons, Mbeya, huku aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Tom Saintfiet akianika ukweli ambao baadaye ulimponza na kufukuzwa.

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake, mmoja wa wachezaji alisema, mambo ni yale yale kama ilivyokuwa Mbeya.

“Mambo kama ya Mbeya, hoteli ni nzuri, lakini wachezaji tumelala wawili wawili katika hoteli, pamoja na kupata huduma nzuri lakini tatizo lilikuwa ni hilo,” alisema mmoja wa wachezaji hao.

Hata hivyo wachezaji wanatarajiwa kurejea kwa usafiri wa basi, badala ya ndege maalumu ya kukodi ya Kampuni ya Precision Air, iliyotumika kwenda Kagera kwa ajili ya mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, dhidi ya Kagera, uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Kaitaba.

Habari zilizopatikana kutoka kwa kiongozi mmoja, ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, zinasema wachezaji hao watarejea kwa usafiri huo baada ya mchezo wao dhidi ya Toto African, ambao utachezwa keshokutwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Wachezaji hao wanatarajiwa kuondoka mjini Mwanza Ijumaa, baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Toto African, kwa basi maalumu walilopewa na wadhamini wao, Kampuni ya Bia Tanzania TBL kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro.

Hata hivyo, gazeti hili liliweza kuongea na mkuu wa msafara, Mussa Katabaro, ambaye alisema anachojua yeye ni kwamba timu yao itarejea kwa ndege kama ilivyokuja.

Wakati huo huo, uongozi wa Kagera Sugar uliondoa mabango ya wadhamini wa Yanga, Kampuni ya Bia Tanzania, kutokana na kuwa wenyeji wa mchezo huo.

Kagera Sugar ambao ndio wenyeji wa uwanja huo kupitia kwa mratibu wake Mohamed Hussein, ilikataa katu katu mabango hayo kuwekwa katika uwanja huo, kwa kuwa wao ndio wa miliki wake.

MATUMLA NDANI YA MKASI NA SALAMA JABR





VURUGU ZA UVCCM MARA NDIO HIZI




UDA KULITEKA SOKO LA TANZANIA BAADA YA KUPATA MUWEKEZAJI

 
Picture
Viongozi wa Kampuni ya Simon Group na wengine Wakielekea kuzindua mabasi15 waliyowekeza UDA.
KAMPUNI ya Usafiri jijini Dar es Salaam (UDA) imejipanga kuteka soko la usafiri nchini ifikapo mwezi Machi mwaka 2013.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena alipokuwa akipokea mabasi 15 kutoka kampuni ya Tata Africa ya India ikiwa ni sehemu ya mabasi 30 yanayotarajiwa kuingizwa nchini ifikapo Desemba mwaka huu.

Kisena alisema kampuni ya Simon Group iliyowekeza katika shirika la UDA imejipanga kuwa kampuni kubwa barani Afrika kwa mtaji wa Dola25 milioni (sawa na Sh375 bilioni)  utakaowezesha kupatikana kwa mabasi 300 ifikapo mwezi Machi mwakani, “Simon Group imejipanga kuwa kampuni kubwa Afrika ifikapo Machi mwakani na tuna mpango wa kununua mabasi 300 kwa mtaji wa Dola25 milioni,” alisema Kisena.

Aliongeza kuwa kati ya mabasi hayo kutakuwa na mabasi ya wanawake, mabasi ya wanafunzi, mabasi ya binafsi, mabasi ya mikoani na mabasi yatakayosafiri barani Afrika, “Mazingira mabovu ya sasa ya usafiri katika jiji la Dar es Salaam mara kwa mara yamekuwa yakisababisha udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake, bila shaka wengi wenu mtakumbuka vizuri kisa cha Maumba. Tunataka kukomesha udhalilishaji huo kwa wanawake ili wasafiri kwa uhuru na raha mstarehe,” alisema Kisena.

Kuhusu mabasi ya wanafunzi, alisema yatakuwa matano kila barabara kuu jijini Dar es Salaam na yatafanya kazi hiyo tu.

Kuhusu mabasi ya binafsi (Executive class), alisema yatakuwa na nauli ya juu lakini yatatoa huduma kama vile televisheni, vinywaji, magazeti na kiyoyozi, “Tunataka tuwahamasishe watu wasitumie tena magari yao binafsi. Unajua kwa mwezi mtu hutumia katiya Sh800,000 hadi Sh1milioni kununua mafuta ya gari, hela ambayo ni nyingi mno. Lakini kwa kutumia usafiri huu, inawezekana kubana matumizi,” alisema.

Akizungumzia mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART) alisema kuwa wanatarajia kushinda zabuni ya kuuendesha kwa kuwa kampuni hiyo haina mshindani katika usafirishaji nchini, “Kwa sasa Dart inajengwa barabara ya Morogoro na barabara itakamilika mwaka 2014. Kwa sasa tutaendesha mradi huo kabla Dart haijaanza na kwa barabara nyingine baada ya hapo. Kwa kuwa sasa UDA haina mpinzani katika sekta ya usafirishaji nchini, naamini tutashinda zabuni ya kuendesha,” alisema. Aliongeza kuwa mradi huo unatarajia kutoa ajira kwa zaidi ya Watanzania 1,500.
Picture
Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group,Robert Kisena (wa pili kulia) Wawekezaji wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA akipokea mfano wa funguo kutoka kwa Meneja wa Biashara wa TATA Afrika Holding Tanzania Ltd,Srinivas Nemalapuri (wa pili kushoto) kulia ni Mkurugenzi wa Simon Group, Leonard Rubuye na kushoto Kaimu Meneja Biashara,Sarvan Keshri. ikiwa ishara makabidhiano ya mabasi 15 katika awamu ya kwanza, hafla hiyo ilifanyika kwenye Ofisi za UDA Dar es Salaam.
Picture
Mwenyekiti Mtendaji wa Simon Group,Robert Kisena (wa nne kushoto) akiwaongoza viongozi wengine ndani ya Basi la UDA.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU