Facebook Comments Box

Thursday, June 20, 2013

HAYA NDIO MAONI YA MBUNGE WA KIGOMA KUHUSU TUKIO LA MABOMU ARUSHA



KIBONZO:ILI KUIPA PROMO BLOG SASA WANAWAUA WATU MAARUFU

Ukiipenda unaweza kushea mtu wangu!



MBOWE NA LEMA WAJISALIMISHA POLISI LEO ASUBUHI



Kwa Taarifa zilizo tufikia zinasema kwamba Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha Chadema Freeman Mbowe na mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema wamejisalimisha wenyewe leo asubuhi  katika kituo Kikuu cha Polisi Mkoani Arusha kwa ajili ya kuhojiwa.


WABUNGE WA CHADEMA WATHIBITISHA MKONG`OTO WALIOPEWA NA POLISI ULIKUWA WA NGUVU

Mbunge wa Singida Mashariki,Tundu Lissu akiwaonyesha waandishi wa habari miwani yake aliyodai kuvunjiwa na polisi. Lissu alipata dhamana katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kati, jijini Arusha jana baada ya kukamatwa juzi. Picha na Moses Mashalla
 
Arusha/Dar es Salaam. Wabunge wanne wa Chadema, ambao waliachiwa na polisi kwa dhamana wamesimulia mateso waliyoyapata wakiwa rumande baada ya kukamatwa juzi.
Vigogo hao; Mbunge wa Mpanda Mjini Said Amour Arfi, Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti maalumu), walikamatwa juzi baada ya wao na wafuasi wa chama hicho kutawanywa kwa mabomu ya machozi na polisi kwenye Viwanja vya Soweto, Arusha.
Wabunge hao waliachiwa baada ya kujidhamini wenyewe huku watu wengine 65 waliokamatwa pamoja nao wakiachiwa baada ya kudhaminiwa.
Wote wanatakiwa kuripoti kwenye kituo hicho Julai 22, mwaka huu na wataelezwa hatma ya suala hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja alisema jeshi lake linaendelea kuwasaka Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha, Godbless Lema na kuwaonya kuwa wanatakiwa kujisalimisha mara moja.
Chagonja alisema Mbowe na Lema wanatafutwa kwa kosa la kufanya kusanyiko lisilo halali katika viwanja hivyo vya Soweto walipokuwa wakitaka kuomboleza vifo vya watu watatu; Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally waliofariki dunia baada ya kuumizwa kutokana na mlipuko wa bomu, Jumamosi iliyopita.
Pia aliwaamuru Mbowe na Lema kuwasilisha mara moja ushahidi wa kuwahusisha polisi na shambulio la bomu na kama hawana imani na Polisi, basi wawasilishe ushahidi wao kwa Rais Jakaya Kikwete.

Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alilalamikia kitendo cha polisi kumwagia maji ya kuwasha baada ya kumkamata.
“Walinimwagia maji ya kuwasha kwa mfululizo nikalazimika kulala chini kifudifudi huku nikiwa nimefunika macho kukwepa yasiingie maji. “Kuna askari walitaka kunipiga lakini niliokolewa na mwenzao mmoja aliyenikinga nisishambuliwe. Kwa kweli ilikuwa hali ya hatari,” alisema.
Alisema polisi hao waliomkamata walivunja miwani yake kwa makusudi akisema aliikabidhi kaunta ikiwa haijavunjika.
“Wakati naingia mahabusu nilikabidhi miwani yangu lakini ajabu wakati tukiachiwa ilikuwa imevunjika.” Alilalamikia hatua ya polisi kuwashambulia kwa mabomu, kuwamwagia maji ya kuwasha walipokuwa wakiwatawanya watu waliokusanyika Soweto akisema awali, waliwaruhusu.


TUME YA UCHAGUZI YAPIGA MARUFUKU MIKUTANO YA KAMPENI ARUSHA


Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC, imevikataza vyama vya siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi mdogo wa Madiwani kwenye Kata  nne za Arusha Mjini, kufanya kampeni katika kipindi hiki ambacho uchaguzi huo umehairishwa hadi Juni 30 mwaka huu.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo, JULIUS MALLABA amesema kwamba sheria za uchaguzi haziruhusu kwa sasa vyama vya siasa kufanya kampeni kwa kuwa uchaguzi katika Kata hizo umeahirishwa baada ya muda wa kampeni ulikwisha.

Vyama ambavyo vitaonekana kukiuka taratibu hizo vitachukuliwa hatua na kamati za maadili ambazo zinajumuisha wajumbe kutoka vyama vyote vya siasa nchini.

MALLABA pia ametoa wito kwa wananchi wa Kata hizo nne -- Themi, Kaloleni, Kimandolu na Elerai -- kuwa ifikapo siku ya kupiga kura, washiriki zoezi hilo kwa amani na utulivu.



TAARIFA YA BARAZA LA MITIHANI KUHUSU HATI ZA MATOKEO (RESULT SLIP) ZA MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE

Picture

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU