Facebook Comments Box

Tuesday, February 5, 2013

UTOTO WA WABUNGE WETU UNACHANGIA UMASIKINI WETU

Picture
Na. Emmanuel J. Shilatu
Mara baada ya kufanikiwa kuziondoa tawala mbovu, nyonyaji na za kidhalimu za Wakoloni hapa nchini, aliyekuwa akiongeza harakati hizo ambaye pia ni Baba wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema ya kuwa “tumefanikiwa kuwaondoa wakoloni na hivyo tupo huru na Uhuru ni kazi”. Hapa Mwalimu Nyerere alikuwa na maana ya kuwa ili tuweze kupiga hatua kimaendeleo ni lazima tuutumie huu uhuru wetu vilivyo kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa yote ili kuleta maboresho katika Nyanja zote za kimaisha yaani uchumi, kijamii na kisiasa.
Na ndio maana yeye kama kiongozi alianza kuonyesha mfano wa dhahiri kwa kuanzisha mapambano kwa vitendo dhidi ya maadui zetu watatu ambao ni ujinga, maradhi, na umaskini. Sehemu ya mafanikio yake ni kwa kupitia kuanzisha maazimio, mashirika, kauli mbiu na sera mbalimbali. Hayo yoote (yaani tangu kusaka uhuru wa Tanganyika) aliweza kufanikiwa kutokana na kufanya mambo kwa matendo zaidi kuliko maongezi (porojo) zisizoisha.
Pia Mwalimu Nyerere alikuwa na falsafa (dhana) ya kimaendeleo ambapo aliamini kuwa maendeleo sahihi hayawezi yakapatikana nje ya uwepo wa mambo manne ambayo ni“Watu”, “ardhi”, “siasa safi”na “uongozi bora”
Ndio “Watu”ni kiungo kimojawapo cha hakikisho la maendeleo chanya yeyote yale ndani ya familia, jamii na Taifa kwa ujumla. Kama tutakuwa na miundombinu bora ni watu wamechangia uwepo wake; kama tutakuwa na mazao ya kutosha kwa ajili ya chakula, kiada na biashara ni watu ndio wamechangia hayo; Endapo kuna amani na utulivu nchini basi ujue watu wamechangia hayo; ama taifa likiwa na wasomi wa kutosha ni watu mbalimbali ndio wamechangia hilo.
Licha ya kwamba Taifa letu Tanzania lina watu zaidi ya Milioni 45 lakini hao watu wamekuwa ndio kikwazo kikubwa katika uletaji wa maendeleo ya kweli na ya dhahiri. Tatizo lililopo ni uibukaji wa umaskini mkubwa wa utegemezi na utajiri mkubwa wa porojo ndani ya jamii na kila Mwana jamii ni mwathirika wa hili si Kijana wala Mzee awe ni Mwanamke au Mwanaume.
Utakuta vijana wengi kutwa wanashinda kwenye kucheza “pool table” na kukaa vijiweni tu; Wazee ama akina Baba nao kutwa wanacheza “bao” ama “draft” tu; na akina Mama nao kila kukicha wapo vibarazani wakisutana na kupashana umbea tu. Hayo ndio maisha ya kila siku ya baadhi ya wanajamii ya kutokupenda kufanya kazi kwa bidii.
Jamii inachojua ni utegemezi pekee. Kivipi? ... Kwa jinsi tuanavyoishi utadhani tunawangojea baadhi ya watu kutoka nje ili waje watuletee maendeleo yaani imefika kipindi kwa mtu hata kutandika kitanda chake mwenyewe anacholalia imekuwa ni kazi kuubwa kwake. Pia suala la maendeleo ya nchi yetu wenyewe tumewaachia viongozi pekee huku tukijiengua katika kapu la dhana ya neno“Serikali” wakati kiuhalisia na kikatiba pia ni kwamba Serikali inaundwa na viongozi pamoja na Wananchi.
Hii yote inatokana na jamii kuziasi mitazamo miongozo na falsafa za Mwalimu Nyerere (mathalani ile ya “Uhuru ni kazi”) hali inayosababisha kiwango cha idadi ya watu maskini kuzidi kukua nchini licha ya kujaariwa rasilimali na mali za asili kwa kuyachakachua maendeleo yetu wenyewe. Kisa? Porojo kutawala maisha yetu.
Hali hii tuliyonayo ya kutaka kuongea ongea ovyo huku parojo zikituendesha katika masuala ya kimsingi ya maisha yetu, tunataka tuwaambukize hata na viongozi wetu. Imefika kipindi kigezo ama kipimo cha uwezo wa Kiongozi unapimwa na utokeaji wa mara kwa mara kwenye vyombo vya habari ama uongeaji, uropokaji na ubwatukaji wa mara kwa mara kwenye jumba letu tukufu la kutunga sheria na wala si utendaji wake kazi na uletaji wa maendeleo katika jamii yaani ni usanii, usanii mtupu. Hii ni hatari sana.
Hivi tunachotaka kutoka kwa Kiongozi ni mazungumzo pekee ama matendo yake ya kimaendeleo? Ama uwezo wa kiongozi bora upo kwenye mazungumzo tu ama utakelezaji wa kimaemdeleo? Hivi uhodari wa mbunge wangu unatoka na amezungumza mara ngapi Bungeni ama amenipunguziaje zigo langu la matatizo ya kimsingi? Bila shaka majibu ni hapana ila ajabu ya firauni ni kuwa kwa miaka ya hivi karibuni kumeibuka dhana mfu ya kupima uwezo wa Kiongozi si kwa uletaji wa maendeleo bali ugwiji wake wa kuzungumza Bungeni kwa kuchangia hoja kuulizwa maswali ya msingi na kadhalika.
Mtazamo huu unaonyesha kuwa kiongozi bora anapimwa kwa uwezo wake wa kuongea Bungeni na si utetaji wa maendeleo; Pili, wanawafundisha viongozi wetu tabia mbaya ya kuwa wawe ni wazungumzaji tu na si watendaji; Tatu, inavyoonyesha hawaijali thamani ya maisha ya Mtanzania bali ya Yule anayeiwasha vipaza sauti mara kwa mara pale mjengoni.
Katika kipindi fulani cha nyuma tafiti mojawapo nchini walitoa matokeo yao ya utafiti ambapo waliueleza Umma kuwa Mh. Edward Ngoyai Lowassa ndiye anayeongoza pale Bungeni kwa kutokuongea pale Bungeni tangu 2005. Jamani hivi ni kweli?
Lowassa wanayemzungumzia ni yule yule ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa kwanza katika serikali hii ya awamu ya nne kwa takribani miaka miwili. Kikatiba, Waziri Mkuu ndiye Kiongozi wa shughuli nzima za Serikali Bungeni. Hivi inawezekana vipi kwa kiongozi mkubwa kama huyo (Waziri Mkuu) kutokuongea lolote lile kwenye mikutano na vikao vya Bunge? Amu hoja au maswali mazito yahusuyo serikali yakiwashinda Mawaziri, M/Waziri au Mwanasheria Mkuu huwa yanatolewa ufafanuzi na nani?
Suala la kuongea mno Bungeni sio hoja ya kuwaletea neema ya kimaendeleo bali Wapiga kura wanahitaji matendo na wala sio maneno matupu . Wapo Wabunge ambao sio waongeaji lakini kwenye majimbo yao wameleta neema ya ajabu kupitia uongozi wao.
Mathalani Mh. Nimrod Mkono ambaye ni Mbunge wa Musoma Vijijini katika kipindi cha ubunge wake amewaletea neema kubwa Wapiga kura wake. Amewajengea shule ya sekondari kubwa na ya kisasa na kuikabidhi kwa Serikali, amejenga maabara ya kisasa iliyojitosheleza kila kitu mihimu, amejenga nyumba za walimu. Pia amewanunulia gari la kubebea wagonjwa kwa wana wa jimbo la Musoma vijijini na kadhalika. Pamoja na kutokuongea kwake Bungeni lakini Wapiga kura wake hauwaelezi kitu kwani ni Mkono, Mkono tu. Hivyo kutokuongea Bungeni sio tatizo.
Pia mwangalie Mohamed Dewji “MO” (Mbunge wa Singida Mjini) ambaye yeye si muongeaji lakini nyakati zote ameonyesha nia ya dhati ya kuwapenda na kuwathamini wapiga kura wake. “MO” amejitolea kwalipia ada ya vyuoni wale wote wa jimbo lake waliobahatika kupata elimu ya juu (chuoni), kwa wale pia ambao wana vigezo amewaahidi kuwapa ajira za kudumu kupitia makampuni yake, hata hivyo pia amekamilisha miradi mingi ya maendeleo ambayo ilikuwa inasuasua.
Hao ni baadhi tu ya wale ambao sio waongeaji lakini ni watendaji haswaa ambao Wapiga kura wao wanajivunia nao. Lakini wapo wale ambao ni mafundi wa kuongea hadi kuwa wabwatukaji pale Bungeni lakini uongeaji wao huo haujawasaidia lolote lile Wapiga kura wao.
Licha ya ufundi wao wa kuongea lakini wameshindwa kuwatatulia kero za maji, umeme, hospitali, shule ama masoko kwa ajili ya bidhaa zao; wengine waliahidi kuwajengea majosho ya kuogesha ng’ombe wao, kuwajengea machinjio ya kisasa na hata wengine wameshindwa kuikamilisha mradi wa ujenzi wa kawaida cha kusindika Tangawizi tu. Wengine ndio wameua kabisa sekta ya kilimo katika majimbo yao hali ambayo inawafanya Wananchi waishi maisha magumu na yasiyoelezeka.
Nimelazimika kuyaeleza haya kutokana na mitazamo isiyo na tija kwa jamii inayozaa matukio ya uletaji ushabiki wa kisiasa kwenye chombo muhimu cha kutunga sharia za nchi ambapo Wabunge wanawatelekeza wapiga kura wao kwa kutokupigania maslahi yao na badala yake wanaendekeza ushabiki wa kichama ndani ya Bunge.
Ni aibu isiyoelezeka kumuona Mbunge anawasha kipaza sauti na kuanza kutoa maneno ya kebehi kwa kufuata utashi wa kisiasa. Huko ni kuwapotezea muda wapiga kura wao.
Dhana ya hiyo ya kushabikia waongeaji ndani ya Bunge imewafanya Wabunge wengi wasiwe watiifu mbele ya kiti cha Spika kwa kujiamulia kuwasha vipasa sauti na kila mmoja kuanza kuzungumza na hatimaye kuligeuza Bunge kuwa gulio na si tena mhimili wa dola.
Utoto wa Wabunge haustahili kuvumiliwa hata kidogo kwa kuwa wao ni Watu wazima na watu wamewaamini kiasi cha kuwapatia madaraka.
Endapo Mbunge atakuwa anatumia muda mwingi kwa ajili ya kuzomea zomea ndani ya Bunge ama kutoa lugha za kebehi na dharau ndani, atapata wapi wasaa wa kuwasemea matatizo ya Wapiga kura wao? Je, sisi Wananchi wa kawaida tunanufaikaje na matokeo hayo ya kitoto yanayofanywa na Wabunge wetu tuliowachagua?
Kimsingi, umaarufu wa Mbunge hauji kwa kuzunumza kwa jazba wala kutoa lugha za maudhi awapo Bungeni, umaarufu wa Mbunge utatokana na kutekeleza ahadi ahadi ya kukidhi matarajio kwa waliomchagua.
Ni vyema Wabunge wakatambua ya kwamba fursa na uhuru waliopewa na watu waliowaamini una mipaka na una mwisho wake, ni vyema wakautumia huo uhuru kabla wakati haujawapita kwani wakati ni ukuta, wakishindana nao wataumia.
Ndugu zangu, kuna haja kubwa ya kuwa makini sana wakati wa upigaji kura ili kuepukana na wabunge wasijali maslahi ya Wananchi bali maslahi yao na ya chama chao, kuwaepuka viongozi watovu wa nidhamu dhidi ya kanuni na utaratibu husika. Bila ya hivyo, tutazidi kuwa maskini!


NDUGU WAWILI WAUWAWA KINYAMA ARUSHA






WANAWAKE wawili wanandugu wameuawa kinyama katika nyumba waliokuwa
wakiishi na watu wasiojulikana na miili yao kukutwa baada ya siku tatu
ikiwa imelaliana huku ikiwa imeharibika vibaya.
Kugundulika kwa miili hiyo kumetokea leo majira ya saa 3.15 katika
eneo la daraja mbili manipsaa ya jiji ya Arusha baada ya majirani
kuhisi harufu kali iliyokuwa ikitokea ndani ya chumba hicho
walichokuwa wamepanga katika nyumba inayomilikiwa na merehemu Samson
Kivuyo.
Taarifa zimeeleza kuwa majirani hao walijikusanya na kutoa taarifa
kwa uongozi wa eneo hilo ambao kwa pamoja walikubaliana kutoa taarifa
polisi ambapo ,polisi walifika eneo la tukio na kuvunja mlango ,ndipo
walipokuta miili ya marehemu hao ikiwa imeharibika vibaya.
Miiili ya marehemu hao ilikutwa na majeraha sehemu mbalimbali za
mwili, huku ndani ya chumba hicho kukiwa kimevurugika na baadhi ya
vitu kuvunjika hali ambayo inaaminika kwamba kabla ya mauaji hayo
kulikuwa na mvutano wa kutoelewana.
Akizungumza na vyombo vya habari msimamizi wa nyumba hiyo,Fatina
Mringo aliwataja marehemu hao kuwa ni,Zainabu Iddy(Zai) mwenye umri wa
miaka 19 na Zena Sadick Shengwatu mwenye umri wa miaka 40 ambaye
alikuwa mfanyabiashara wa nguo na mmiliki wa chumba hicho.
Alieleza kuwa siku ya jumamosi marehemu hao walionekana majira ya
mchana wakiwa nyumbani, na marehemu Zena alikabidhiwa fedha na
wapangaji wenzake na kwenda kulipia bili ya umeme Tanesco na baadae
alirudi na kuendelea na shughuli zake kama kawaida.
Hata hivyo habari zimedai kwamba marehemu hao kwa pamoja hawakuweza
kuonekana tena hadi miili yao ilipokutwa chumbani ikiwa imeharibika
vibaya na kutoa harufu kali.
Hata hivyo baadhi ya majirani wakielezea tukio hilo wamebainisha
kwamba marehemu hao mara nyingi walionekana kuwa na mahusiano ya
kimapenzi na wanaume tofauti na kwamba siku ya tukio Zena alionekana
akichukuliwa na gari dogo aina ya teksi huku gari jingine lilionekana
likingia nyumbani kwake.
Majirani hao wamedai kwamba marehemu hao ambao ni wakazi wa Lushoto
mkoani Tanga waliishi katika nyumba hiyo katika mazingira ya kutokuwa
na waume .
Kamanda wa polisi mkoani Arusha Liberatus Sabas alithibitisha kutokea
kwa tukio hilo na kueleza kwamba uchunguzi unaendelea na kwamba hadi
sasa hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo na miili ya marehemu
hao imehifadhiwa katika hospitali ya mkoa Mount Meru kwa uchunguzi wa
daktari.

MSIKILIZE RAIS OBAMA AKIONGEA KISWAHILI AKIWATUMIA UJUMBE WAKENYA




HABARI MPASUKO:WATU WATANO WAMEFARIKI DUNIA MBEYA

Habari zilizo tufikia kutoa Mbozi - Mbeya zinasema, Watu watano(5) wamekufa wakiwemo watatu(3) wa familia moja baada ya kupigwa na Radi kutokana na mvua kubwa sana iliyoambatana na Radi hizo kunyesha wilayani Mbozi katika Mkoa wa Mbeya.

Habari zaidi tutawaletea kadri muda unavyozidi kwenda.


HII NDIO AKAUNTI MPYA YA TWITTER YA AL-SHABAAB

somalimemo.net 
 
 
 
 
Habari ilizozipata kutoka kwa afisa mmoja anayehusika ktk Ofisi ya habari na maelezo ya Harakat Al-shabaab Al Mujahideen ameihakikishia kuwa account ya Al-shabaab imefunguliwa kwa jina nyingine upya na kwanza kufanya kazi,ambapo kwanzia sasa umma unaweza kuufuatilia Habari na matamko kutoka kwa Harakat Al-shabaab Al Mujahideen.

Afisa huyo ametabanaisha kuwa accounti hiyo mpya inayojulikana kwa jina la @HSMPRESS1, imeanza kufanya kazi kwanzia jana usiku ambapo baadhi ya habari muhimu zimetangazwa kwenye ukurasa huo kwa lugha ya kingereza,ambapo Al-shabaab wameelezea jinsi maadui walivyo jaribu kuwafunga mdomo na kuwasikizisha propaganda zao za uongo wanayo yatangaza,


ilikuwa wiki mmoja iliyopita tangu Shirika la Twitter ilipoifungia ukurasa waliokuwa nao la @HSMPress ambapo uliwavutia watu wengi zaidi ya wanachama 21000 waliokuwa wakiyafuatilia maoni,matamko pamoja na Habari za Mujahideena wa Somalia,shirika hilo la Twitter ilidai kuwa ilipata Shinikizo kutoka Nchi za Magharibi na Ufaransa ili kuufunga Accounti hiyo ya Harakati Al-shabaab Al Mujahideen wa Somalia.


Kwanzia sasa Ummah wote wa Kislaam waliokuwa wakiyafuatilia ukurasa wa Harakat Al Shabaab Al Mujahideen wanatangaziwa rasmi kuwa ukurasa mpya @HSMPRESS1 unafanya kazi,


HIZI VIDEO NI ZA TANGAZO LA TV LA TURKISH AIRLINE, WAMECHEZA LIONEL MESSI NA KOBE BRYANT! TAZAMA PIA LILIVYOKUA LIKITENGENEZWA







NCCR-MAGEUZI WAIBOMOA CHADEMA MBEYA: VIONGOZI NA MAKADA ZAIDI YA 20 WAJIUNGA NA NCCR MAGEUZI

Moses Mwasubira, ambaye alikuwa mwenezi wa Chadema wilaya ya Mbeya akikabidhiwa kadi ya NCCR na 
Mmoja wa kada Chadema, Emanuel Mwangoka (Cash Money), ambaye inadaiwa kuwa ndiye alikuwa mfadhili Mkuu wa mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Chadema), akikabidhiwa kadi ya chama kipya, alisema atatumia uwezo wake wote kama alivyofanya kwa sugu kuhakikisha NCCR-Mageuzi inaibuka na kung’ara mkoani 
Mjumbe wa Halmshauri Kuu taifa ya chama hicho, Juju Danda,
 Mjumbe wa Halmshauri Kuu taifa ya chama hicho, Juju Danda, katika tukio la kuwapokea wanachama wapya 21 waliojunga na chama hicho, wakitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

 Aliyewahi kuwa Katibu wa Chadema Mkoa wa Mbeya na kujiunga na NCCR-Mageuzi , Januari 20 mwaka huu Eddo Mwamalala, alisema wanachama hao waliomfuata ni mtaji mkubwa wa kuhakikisha inakimaliza chadema mkoani hapa.



PATA MUDA KUANGALIA VURUGU ZA WABUNGE JANA BUNGENI




KIKWETE WAKUTANA NA DIAMOND IKULU NDOGO WALIOONGEA HAYA HAPA




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete usiku wa kuamkia leo, Jumatatu, Februari 4, 2013, alikutana kwa muda mfupi na kundi la wasaniii wa muziki la Diamond Group wakiongozwa na kiongozi wa bendi hiyo Nasib Abdu maarufu kwa jina la Diamond.

Katika mkutano huo uliofanyika kwenye Ikulu Ndogo ya mjini Kigoma, wasanii hao walimshukuru Rais Kikwete kwa msimamo wake usioyumba wa kuunga mkono wasanii wa Tanzania na kuhakikisha kuwa wanafaidika na kazi zao.
Rais Kikwete alikuwa mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi ya siku tatu ambako jana, Jumapili, Februari 3, 2013, alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za miaka 36 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) zilizofanyika kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma na ambako Diamond na kundi lake walitumbuiza.

Mwanamuziki huyo alimshukuru Rais Kikwete kwa juhudi zake nyingi na za wakati wote kuunga mkono wasanii wa Tanzania na hasa kuunga mkono mapambano ya jitihada za wasanii hao kunufaika na kazi zao.

Shukurani kubwa za Diamond zilihusu hatua ya Rais Kikwete kumlipa mtaalamu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam aliyefanya utafiti wa namna ya kuwasaidia wasanii, hatua iliyopelekea Mamlaka ya Kodi Tanzania (TRA) kuanzisha mfumo wa kusaidia kuthibiti kazi za wasanii mwaka huu. Mtaalamu huyo alilipwa Sh. milioni 20 kwa kazi hiyo.

Diamond amemwomba Rais Kikwete kuangalia jinsi gani Serikali inavyoweza kuwasaidia wasanii kupata malipo ya haki kutokana na nyimbo zao zinazotumika kama milio ya simu.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM


RAIS KIKWETE AZINDUA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA KIGOMA NA KUKAGUA DARAJA LA MALAGARASI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na viongozi wengine akikata utepe kuzindua ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jana Januari 4, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi Bw Phillipe Dongier, wakifunua kitambaa cha jiwe la msingi katika uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jana Januari 4, 2013.
Rais Kikwete akiongezana na mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi Bw Phillipe Dongier mara baada ya uzinduzi huo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi mbalimbali wakipata maelezo juu ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma toka kwa mhandisi George Sambali wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jana Januari 4, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na viongozi wengine baada ya uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jana Januari 4, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wananchi wa Kigoma wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jana Januari 4, 2013.
mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Uganda na Burundi,Bw. Phillipe Dongier akiongea na wananchi wa Kigoma wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jana Januari 4, 2013.
Msanii Diamond na kundi lake wakitumbuiza wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma jana Januari 4, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza maelezo ya Daraja la Maragarasi kutoka kwa Meneja wa Kampuni ya HANIL ambao ni Wakandarasi wa ujenzi wa Daraja hilo,Bw. Jung-Sik You kutoka nchini Korea,jana Januari 4,2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameongozana na Mama Salma Kikwete na maafisa mbali mbali wakikagua ujenzi wa Daraja la Mto Malagarasi lililopewa jina la Daraja la Kikwete mkoani Kigoma jana Februari 4, 2013. Asilimia zaidi ya 90 ya ujenzi wa daraja hilo zimekamilika nan linatarajiwa kufunguliwa baadaye mwaka huu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Muungano eneo la Kibaoni wilayani Uvinza, Kigoma, akiwa njiani kuelekea mjini Kigoma, akitokea kukagua ujenzi wa daraja la Mto Malagarasi jana

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU