Facebook Comments Box

Friday, September 27, 2013

USHAHIDI WA NGASSA KULIPA MILIONI 45 ZA SIMBA LEO HUU HAPA

Mrisho Ghalfan Ngassa akionesha risiti ya malipo aliyopewa na TFF baada ya kulipa milioni 45 anazo alizo takiwa kuilipa timu ya simba
Kiungo mshambuliaji wa timu ya Young Africans Mrisho Khlafani Ngassa leo amelipa jumla ya mil 45, deni la mil 30 pamoja na faini ya mil 15 za klabu ya Simba SC kwa Shirikisho la Soka nchini TFF ili aweze kuitumikia timu yake kuanzia kesho.
Hundi ya milioni 45 ya Ngassa kwenda TFF kwa ajili ya kuwalipa simba

Ngassa ambaye aliambatana na viongozi wa klabu ya Yanga mjumbe wa sekretariat Partick Naggi, Afisa Habari Baraka Kizuguto na mhasibu Rose Msamila alikabidhi hundi za malipo kwa idara ya fedha ya shirikisho hilo.
Mara baada ya kukabidhi hundi hiyo Ngassa aliongea na waandishi wa habari nje ya ofisi za TFF na kusema ameamua kulilipa deni hilo ili aweze kuitumikia klabu yake, kwani kukosa michezo sita kumemnyima fursa ya kuisaidia timu yake.
hapa Ngassa akionesha hundi hizo
Naomba mnielewe hizi fedha nimezitoa mimi mwenyewe kwenye akiba yangu iliyopo bank, hivyo kama kuna mtu yoyote ataguswa na hili suala anaweza kuwasiliana na mimi katika kujaribu kunichangia juu ya hili.
Hizi hapa
Aidha Ngasaa amesema kwa sasa akili yake yote ipo kwenye michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom na lengo lake ni kuhakikisha anaisadia timu yake kufanya vizuri n akupata ushindi katika kila mchezo watakaocheza.
Kocha Ernie Brandts kwa sasa ana fursa ya kumtumia mchezaji Mrisho Ngasa kwa kuanzia kwa mchezo wa kesho kutokana na kuwa amekamilisha kila kitu.
Naye Afisa Habari wa Yanga Baraka Kizuguto amewaomba wapenzi, washabiki na wanachama kujitokeza kwa wingi kesho uwanja wa Taifa kuja kuishangilia timu yao itakapokua ikicheza na maafande wa Ruvu Shooting.
Muhasibu wa TFF akikunja goti kuandika risiti
Young Africans itacheza na Ruvu Shooting katika uwanja wa Taifa majira ya saa 10:00 kwa saa za Afrika Mashariki.

CHANZO: BIN ZUBEIRY




PICHA YA UJENZI WA DARAJA LA KIGAMBONI ULIPO FIKIA SASA

Mafundi wa kampuni ya MBEC ya China wakiendelea kusuka nondo za daraja litakalo unganisha kigamboni na jiji la Dar es salaam kwa upande wa kurasini. Daraja hilo linajengwa kwenye bahari ya hindi na litakamilika mwaka 2015.

CHANZO: MWANANCHI






VIDEO: ANGALIA JINSI MAGAIDI WALIVYO JIPANGA NA KUVAMIA WEST GATE MALL




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU