Facebook Comments Box

Saturday, September 6, 2014

AJALI HIZI ZA KIZEMBE MPAKA LINI JAMANI TUCHUKUE HATUA TUTAKWISHA

 
Katika ajali ambayo imetokea jana asubuhi majira ya saa tano katika kijiji cha Saba saba - Butiama, Musoma ambapo magari mawili ya Mwanza Coach na J4-Express yaligongana uso kwa uso na kusababisha watu zaidi ya 36 kufariki dunia na majeruhi 70 kwa uzembe wa madereva wa mabasi ya abiria ambayo yamekuwa yakifanya ajali nyingi bila kuzingatia kuwa maisha ya watu wasio na hatia yanapotea bure.
 Ajali hiyo iliyotokea jana watu wazima, wazee wasio na hatia pamoja na watoto wadogo walipoteza uhai wao bila kutarajia tena ghafla huku wakiacha familia zao bila taarifa yoyote tena bila kuwaaga ndugu na jamaa kwa uzembe ambao umesababishwa na madereva hao wawili wa mabasi hayo.


 bado haijafahamika kama madereva hao ni miongoni mwa watu waliofariki au la, uzembe kama huo ulitokea siku chache Nzega Tabora baada ya Mabasi Mawili kugongana uso kwa uso eti ikisemekana kuwa barabara ilikuwa na vumbi sana kiasi kwamba Madereva walikuwa hawaoni mbele ndiyo maana wakagongana, kama ni kweli hali ya vumbi kiasi hicho ilitakiwa mwendo upungue maana utaendeshaje gari kwa kasi kama mbele unapo elekea hupaoni?



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU