Facebook Comments Box

Monday, May 12, 2014

CHRISS BROWN AONGEZEWA MUDA WA KUKAA JELA

Brown alifungwa jela baada ya kumchapa aliyekuwa mpenzi wake
Rihana
Mwanamuziki wa Marekani Chris Brown atasalia jela kwa siku
nyingine 131 baada ya kukiri kukiuka amri ya mahakama kuhusu
kifungo cha nje alichokuwa amepewa na mahakama.
Muimbaji huyo wa muziki wa mtindo wa R&B alikiri mahakamani
mjini Los Angeles mnamo siku ya Ijumaa kuwa alitenda uhalifu mjini
Washington Oktoba mwaka jana.
Jaji alimuhukumu kifungo cha siku 365 jela ingawa alimpongeza
kwa kuhudumia siku 234 katika kituo cha kupata ushauri nasaha.
Brown amekuwa chini ya aungalizi wa mahakama tangu mwaka
2009 alipokiri kumpiga mwanamuziki mwenza na ambaye alikuwa
mpenzi wake wakati huo,Rihanna.
Mshindi huyo wa tuzo la Grammy amekuwa kizuizini tangu mwezi
Machi alipokamatwa kwa kukiuka amri ya mahakama iliyomweka
ndani ya kituo cha ushauri nasaha pamoja na jela.
Kifungo alichopata kuongezewa siku kinahusiana na kisa cha
ugomvi kilichotokea mjini DC mwaka jana.
Brown anakabiliwa na mashitaka ya kumchapa mwanamume
mmoja nje ya hoteli moja mjini Washington



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU