Facebook Comments Box

Tuesday, March 5, 2013

ISRAEL LAUNCHES SEGREGATED BUS SERVICE



A 'Palestinians-only' bus line is launched in Israel after settlers complain Palestinians are a 'security risk'.




Palestinian labourers use the buses to travel from the West Bank into Israel for work

Israel has launched two Palestinians-only bus lines in the occupied West Bank, a step an Israeli rights group described as racist and which the Transport Ministry called an improvement in service.
The left-wing Haaretz daily reported that the ministry opened the lines on Monday, to be used by Palestinian labourers travelling between the West Bank and Israel, after Jewish settlers complained that Palestinians on mixed buses were a security risk.
"Creating separate bus lines for Israeli Jews and Palestinians is a revolting plan," Jessica Montell, director of the B'Tselem rights group, said on Army Radio. "This is simply racism. Such a plan cannot be justified with claims of security needs or overcrowding."
The Transport Ministry said the two new lines would "improve public transport services for Palestinian workers entering Israel" and replace pirate buses charging them "exorbitant prices".
"The Ministry of Transport has not issued any instruction or prohibition that prevents Palestinian workers from travelling on public transport in Israel nor in Judea and Samaria," it said, referring to the West Bank.
"Furthermore, the Ministry of Transport is not authorised to prevent any passenger from using public transport services."
Concerns
Rights groups, however, voiced concern that Israeli police at checkpoints in the West Bank would remove Palestinian passengers from regular bus lines and order them to use the new ones.
Police spokesman Micky Rosenfeld said all Palestinians returning to the West Bank would be searched for stolen property, describing this as a routine Israeli precaution.
He said he did not know whether and how this might affect Palestinian travel on regular buses.
Herzl Ben-Zvi, mayor of the Karnei Shomron settlement, said the new lines "answer the needs of all passengers; Palestinians and settlers" because they would relieve overcrowding on buses in the area.
Israel occupied the West Bank in the 1967 Middle East war and maintains a network of roadblocks in the territory, severely restricting movement of Palestinians in the area.
Palestinians seek the West Bank, along with the Gaza Strip and East Jerusalem, for a future state, a claim supported by most world powers, which also view the settlements as illegal.


HALI ILIVYO DAR ES SALAAM LEO JIONI BAADA YA MVUA

Hapa ni maeneo ya kijitonyama wakati mvua ikiendelea kunyesha
Kama kawaida haya ni maeneo ya Kariakoo mvua kuanza kidogo mitaro ikaziba na maji yakajaa barabarani na kusababisha hali ngumu kwa usafiri. Wakati wa jioni kulikuwa na foleni kubwa katika barabara ya Uhuru na Barabara ya Mandela
Mvua zikianza tu lazima mitaro izibe na maji yajae barabarani



WAZANZIBAR HAWATOKUBALI KUKOSEKANA Z’BAR YENYE MAMLAKA KAMILI-MALIM SEIF

 

Chama cha wananchi CUF kupitia katibu mkuu wa chama hicho ambae pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, kimemuhakikishia Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania , Jaji Joseph Warioba, kwamba Wazanzibari kwa umoja wao hawatokubali chochote kile ambacho kitasababisha kukosekana kwa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mfumo mpya wa ushirikiano na Tanganyika kupitia Muungano.

Maalim Seif aliyasema hayo huko Makunduchi mkoa wa kusini Unguja alipokuwa akizungumza na wananchi mbali mbali kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho,amesema kutokana na matukio ya asilimia 66 ya maoni ya wazanzibar kutaka mamlaka kamili ya nchi yao basi hakun haja ya kutokuirjesha Zanzibar hadhi yake.
Kufuatia mkutano huo Maalim Seif amesema kuwa kwa sasa Zanzibar haiwezi tena kukubali kukosa mamlaka yake ya kuwa na udhibiti wa mambo ya nje na mahusiano ya kimataifa kwani imechoka na udhalilishaji inaofanyiwa na Tanganyika kupitia Serikali ya Muungano.
Aidha Maalim ametolea mifano mbali mbali ambayo Serikali ya Muungano imeilazimisha Zanzibar kujitoa katika Umoja wa Nchi za Kiislamu (OIC) mwaka 1993 pamoja na hatua ya hujuma iliyofanywa na Waziri wa Mambo ya Nje, Benard Membe, ya wiki iliopita ya kufuta maeneo ya ushirikiano yaliyohusu Zanzibar yaliyokuwa yawe sehemu ya makubaliano katika Mkataba wa Ushirikiano kati ya Tanzania na Oman.
Sambamba na hayo Maalim Seif alitaja athari ya Zanzibar kukosa nafasi ya kufaidika na misaada ya kimataifa katika maeneo yote yasiyo ya Muungano kwani Tanganyika hutumia jina la Tanzania kujichukulia nafasi hiyo kwa manufaa na maslahi yake peke yake jambo ambalo limewatoa imani wazanzibar waliowengi kuendelea na Muungano huu uliopo sasa.
Maalim amefahamisha wazi kuwa kwa sasa Zanzibar inataka kuwa na Wizara na Waziri wake wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na haitokubali chochote chini ya hapo. Amesema kuwa “udhibiti wa mambo ya nje ndiyo kigezo cha nchi kukubalika na kutambulika kimataifa na Zanzibar inataka kurejesha mamlaka hayo na kurejesha kiti chake kwenye Umoja wa Mataifa”.


WATAALAM WA MAMBO WANASEMA HUYU NDIO MCHUMBA WA JUSTIN BIEBER


Justin Bieber
Ella-Paige.

Kuna uwezekano mkubwa Justin Bieber alikuwa na sherehe mbaya ya kuzaliwa ijumaa iliyopita ila alipata mtu ambaye alifanya sherehe yake ya kuzaliwa iwe nzuri  kidogo. Na huyo sio mwingine bali ni Ella Paige mrembo ambae anajihusisha na muziki nchini uingereza.
 Mrembo huyo ana miaka 17 tu. Inasemekana walionana mara ya kwanza Los Angeles wakati binti huyo akirekodi kama mwenzi mmoja uliopita baada ya hapo wamekuwa wakionekana jijini London wakila raha na kuwa pamoja kwa muda mwingi 

UHURU KENYATTA BADO ANAONGOZA

Kura zikihesabiwa kwenye kituo kilichopo Viwanja vya Kibera Social, jijini Nairobi baada ya wananchi wa Kenya kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo jana.
  
Matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu nchini Kenya yanaonyesha kuwa Uhuru Kenyatta, mtoto wa Rais wa Kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta anaongoza, huku akifuatiwa kwa karibu na aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Raila Odinga.
Kama alivyo Uhuru, Raila pia ni mtoto wa mmoja wa waasisi wa taifa la Kenya, ambaye alikuwa Makamu wa Mzee Kenyatta, Jaramong Oginga Odinga.
Hadi majira haya ya  saa 6.45 usiku wa kuamkia leo,  Uhuru ambaye ni mgombea wa TNA alikuwa amepata kura 744,648 sawa na asilimia 56.1 wakati Raila ambaye ni mgombea wa ODM alikuwa akifuatia kwa kupata kura 527, 780 sawa na asilimia 39.7.
Matokeo hayo ni kutoka katika vituo zaidi ya 5000 kati ya 31,000 na yalikuwa yakionyeshwa moja kwa moja na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) kadri yalivyokuwa yanaingia.
Hata hivyo Mwenyekiti wa IEBC, Isaack Hassan akizungumza na vyombo vya habari jana usiku alisema matokeo hayo ni ya awali na kwamba matokeo kamili yangetangazwa na tume yake baada ya kukusanya taarifa kutoka vituo vyote vya kupigia kura.
Wagombea wengine walikuwa wameachwa mbali. Hao ni Musalia Mudavadi, Peter Kenneth, James Kiyiapi, Martha Karua, Mohamed Dida na  Paul Muite.
Waliokufa wafikia 22
Wapema watu 22 wakiwamo askari polisi tisa waliripotiwa kuuwawa  baada ya kuvamiwa na kikundi cha watu zaidi ya 200 huko Mombasa na Kilifi saa chache kabla ya Wakenya kuanza kupiga kura jana.
Saa chache kabla ya uchaguzi huo, askari polisi tisa waliuawa katika mashambulizi yaliyotokea kwenye miji ya Mombasa, Kilifi na Kwale na kuacha wavamizi wapatao 10 na raia wa kawaida watatu pia wakifariki.
Baada ya vifo hivyo, serikali ilipeleka vikosi vya askari kutoka Mariakani Barracks kwenda kutuliza ghasia hizo wakati kundi lingine la askari lilitoka Nyali Barracks kwa ajili ya kuweka doria katika miji ya Mombasa na North Coast.
Taarifa zilizopatikana baadaye jana zilisema kuwa kwenye mji wa Mombasa askari polisi wanne waliuawa na watu zaidi ya 100 waliovamia kituo cha kura cha Miritini.
Polisi pia ilithibitisha kuuawa kwa watu saba katika mapigano hayo huku na wengine kadhaa kutiwa nguvuni.
Wavamizi wengine waliuawa katika miji ya Kisauni na Kilifi huku polisi wanne wakiuawa Chumani na mmoja huko Chonyi huku watu watatu wakiuawa kwa kupigwa risasi.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU