Facebook Comments Box

Tuesday, April 30, 2013

WANAWAKE WANNE WAMTEKA ASKARI WAKIUME NA KUMBAKA



Askari mmoja mwanaume anadaiwa kutekwa kisha kudhalilishwa kijinsia na wanawake wanne kwa wiki moja kabla ya kupigwa mawe na kutupwa katikati ya milima huko Zimbabwe. Mateso ya muathirika huyo mwenye miaka 25 yalianza pale alipopata lifti ya gari kuelekea mji wa Mutare nchini nchini humo,Wanawake wawili na mwanaume mmoja walikuwa kwenye gari, Mercedes Benz, na baada ya kuendesha kwa takribani saa moja kuelekea mji huo, dereva wa gari hilo akabadili mwelekeo wa safari hiyo.

Msemaji wa polisi wa Manicaland, Inspekta Msaidizi Nuzondiwa Clean, alieleza: "Baada ya kubadilishwa mwelekeo huo, mlalamikaji alihoji wapi walikokuwa wakielekea na walimweleza walikuwa wakienda kupata chakula. Askari huyo alitaka kushushwa, lakini dereva huyo akatoa kisu na kumtishia nacho. Mmojawa abiria wanawake akamfunga kwa kitambaa cheusi machoni mtuhumiwa huyo."
 Kwa mujibu wa Nuzondiwa,watesi  hao walimpeleka mlalamikaji kwenye nyumba isiyojulikana ambako walimvua nguo zote na kumpora simu yake na Dola za marekani 35.
 
 Watuhumiwa walimwamuru mtu huyo kulala na mmoja wa wanawake hao katika matukio kadhaa na alishikiliwa kati ya Aprili 19-23. Kisha akafungwa tena kitambaa machoni na kushushwa kwenye Milima ya Dangamvura ambako, kwa mujibu wa polisi, alipigwa mawe katika mguu wake wa kushoto, na kumsababishia majeraha makubwa.
 Watuhumiwa hao kisha wakawasha gari lao na kutokomea kusikojulikana.Askari huyo alitoa taarifa Kituo cha Polisi cha Sakubva.




Monday, April 29, 2013

HII NDIO TAARIFA YA LADY JAY DEE KWA WATANZANIA



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Katika mwaka huu 2013, Inatimia miaka 13 tangu nianze kazi ya muziki.
Nashukuru MUNGU tuko pamoja na pia, nashukuru umma wa Tanzania kwa kuendelea ku support muziki wa Tanzania na kunipa nguvu mimi kama msanii.
Nashukuru vyombo vyote vya habari vinavyoshiriki kikamilifu kukuza na kulinda sanaa ya Tanzania bila kujali maslahi binafsi.
Tumeandaa sherehe kubwa na nzuri ya miaka 13 ya LADY JAYDEE, katika muziki.
Na mdhamini mkuu kwa upande wa media ni East Africa TV.
Sherehe ya miaka 13 ya Lady JayDee katika muziki itaambatana na uzinduzi wa album yangu ya sita inayokwenda kwa jina la NOTHING BUT THE TRUTH ambayo ina jumla ya nyimbo 10.
Katika sherehe hizo pia kutakuwa na show ya nyimbo zote bora za JayDee nikishirikiana na baadhi ya wasanii wenzangu hapa nchini.
Sherehe zitafanyika Ijumaa tarehe 31 May 2013.
Nawakaribisha wote tufurahi pamoja
Na Mungu awabariki


KIBONZO: HIKI NDIO KITUKO KILICHOTOKEA JANA KWENYE MECHI YA ARSENAL NA MANCHESTER UNITED




ANGALIA PICHA ZA PADRI ALIVYO FUMANIWA

KANISA Katoliki Jimbo la Moshi limeingia katika kashfa nzito baada ya padri wake, Father Urbanus Ngowi wa moja ya parokia zake kudaiwa kufumaniwa na mwanamke anayesemekana ni mke wa mtu

Father Ngowi akiwa ameduwaa baada ya kufumaniwa akiwa na mke wa mtu aliyejulikana kwa jina la kijamii la Mama P.
Sakata la fumanizi hilo linadaiwa kutokea Jumatatu ya wiki iliyopita chumbani kwa padri huyo, Marangu Wilaya ya Moshi  Vijijini ambako Father Ngowi inasemekana alikutwa ‘laivu’ akiwa na mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la kijamii la Mama P.

Pamoja na kunaswa huko, vyanzo havijaeleza humo chumbani wawili hao walikuwa wakifanya nini!

Habari zinadai siku ya tukio, mwanamke huyo aliingia nyumbani kwa padri huyo ambapo baadhi ya ndugu wa mumewe walikuwa wakimfuatilia baada ya madai yaliyokuwepo kwamba ana ukaribu wenye maswali mengi na mtumishi huyo wa Mungu.

“Unajua siku nyingi ilivuma kwamba Mama P na Father Ngowi wana ukaribu wenye maswali mengi, mume wake alifuatilia na kubaini ni kweli lakini akashindwa kuutenganisha ukaribu wao,” kilidai chanzo.
Father Ngowi akijaribu kuomba samahani baada ya kufumaniwa.
Chanzo kikaendelea kudai kwamba baada ya kuona mkewe amejikita kwa mtumishi wa Mungu, mumewe alinyoosha mikono juu na kumwachia Mungu.

Chanzo: Sasa siku hiyo baada ya ndugu wa mume kumfuatilia mpaka anaingia kwa Father Ngowi, wakaona ni bora watafute mpigapicha ili kupata picha za tukio ambazo zitakuwa ushahidi siku za mbele.


“Walipompata wakazama ndani, sekeseke likaanzia hapo. Walimkuta mwanamke huyo na mtumishi wa Mungu wapo kitandani.”

 
Father Ngowi na Mama P wakivaa nguo zao kwa aibu baada ya kufumaniwa.

Habari zinadai kwamba kufuatia tukio hilo, tayari Kanisa Katoliki limemweka kitimoto padri huyo ambaye alikuwa akihudumu katika Parokia ya Korongoni, Moshi Vijijini kabla ya kuhamishwa na kupelekwa Parokia ya Makomu, Marangu ambako inadaiwa ameshushwa cheo.

Inadaiwa kuwa baada ya tukio hilo, Father Ngowi alikana kukutwa na mke wa mtu chumbani kwake lakini alipobanwa sana na mabosi wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Moshi, alikiri na kudai ibilisi alimpitia na kuomba kanisa limsamehe na kutompa adhabu kali ambayo itamuathiri kisaikolojia.

Hili ni tukio kubwa na la aina yake kuwahi kulikumba Kanisa Katoliki nchini kwa padri wake kudaiwa kukutwa na mke wa mtu chumbani kwake!
Father Ngowi na Mama P wakiwa na nyuso za aibu baada ya tukio hilo.

Kuna madai kwamba mwaka jana (2012), Father Ngowi, mbele ya waumini wake alisoma barua yenye kukana shutuma zote zilizoelekezwa kwake kwamba amekuwa na ukaribu wenye maswali mengi na wake za watu.

Taarifa zilidai kuwa padri huyo aliweka wazi akisema si kweli kwamba amekuwa na ukaribu unaotajwa, akawataka waumini wake wapuuze tuhuma hizo alizosema  zina mwelekeo wa kuchafua sifa yake na taswira ya Kanisa Katoliki kwa jumla.

Hayo ni madai ya vyanzo vyetu ambavyo viliambatanisha na picha mbalimbali za tukio hilo lenye kushtua waumini sambamba na namba za simu za padri huyo kwa ajili ya mawasiliano ili kujiridhisha.
 Father Ngowi akipatiwa suruali yake.
 
Source: Global publisher


HUYU NDIO MWAFRIKA WA KWANZA KUCHAGULIWA WAZIRI ITALIA

Mwanamke wa kwanza mwenye asili ya kiafrika aitwae CECILE KYENGE KASHETU kutoka nchini CONGO DRC amechaguliwa kuwa Waziri nchini Italy, alizaliwa Agust 28 1964 (48 yrs) na baadae aliolewa na Mwitaliano ambapo mpaka sasa ni Mama wa watoto wawili.
Alihamia nchini Italy mwaka 1983 na kuchukua uraia, alihitimu mafunzo yake ya Udaktari unaohusiana na madawa katika chuo cha Universita Cattolica del Sacro Cuore kilichopo Roma, baada ya kumaliza chuo makazi yake yalikuwa eneo moja liitwao Castelfranco Emilia Jimbo la Modena mkoa wa Emilia- Romanga akiwa anaendelea na kazi yake ya udaktari.
 Mwaka 2004 alijiunga na mambo ya siasa katika chama cha PD yani Partito Democratico na alipata nyadhifa mbalimbali mwaka 2010 lakini february mwaka huu ndio alichaguliwa kuwa Mbunge kupitia chama chake cha PD, mwezi huu wa April 2013 ndio huyu mama amechaguliwa kuwa Waziri anaehusika na mambo ya kigeni kwenye Serikali ya Enrico Letta.




HATIMAYE LEMA AACHIWA

Asubuhi ya leo, kama ilivyotarajiwa na wengi baada kufuatia taarifa mbalimbali katika vyombo vya habari, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alifikishwa mahakamani baada ya kukaa rumande tangu alipokamatwa usiku wa kumkia siku ya Jumamosi, Aprili 27, 2013.

Mbele ya hakimu Joyce Msofe na mawakili Kimomogoro na Humphrey Mtui wanaomtetea, Lema amesomewa shitaka la kosa la uchochezi linalomkabili kwamba aliwachochea wanafunzi wa chuo cha uhasibu Arusha kumzomea Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa kuwaambia wanafunzi kuwa Mkuu huyo wa Mkoa, “hajui chuo cha uhasibu kilipo, amekuja akiwa amechelewa na anaingia hapa kama anaingia kwenye send off.”

Hata hivyo, mtuhumiwa Lema amekana kosa hilo.

Mwendesha mashitaka alisema dhamana ipo wazi kwa mtuhumiwa endapo atatimiza masharti ya dhamana.

Mtuhumiwa alifanikiwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni kuwepo kwa mtu mmoja mwenye kitambulisho kinachokubalika kisheria na kuweka rehani kiasi cha shilingi milioni moja.

Baada ya kutoka mahakamani hapo, Lema alielekea kwenye maeneo ya Ofisi za chama, CHADEMA.
Picture


Sunday, April 28, 2013

HAYA NI MABANGO YALIYOPO MAREKANI YAKIELEZEA UONEVU WA SERIKALI YA TANZANIA

Ukipita kwenye mitaa ya Washington DC katika mtaa wa colombia na 18 street [adams morgan]. Utona kuna mabango na Matagazo kuhusu uonevu unaofanywa na serikali ya Tanzania. Ni picha za akina mwangozi, mauaji ya morogoro, mauaji kule songea, na arusha. Watu wengi wanasema hii Tanzania si inchi ya amani hii imetoka wapi tena?.Kuna mwingine akasema imebadilika sana. Tunachotakiwa ni kupiga simu au kumweleza congress man wako kuhusu hii issue. Tupate ukweli wake.




HII NI HATA RI SANA..



HAYA NDIO MANENO PELE NA ROMARIO WALIO RUSHIANA TENA

Mshambuliaji wa zamani wa Brazil Romario ameanzisha upya vita vyake na na gwiji wa soka duniani Pele kwa kumuita ni mtu mpumbavu.
Wachezaji hawa wawili wa zamani wa Selecao wamekuwa kwenye ugomvi kwa muda mrefu kufuatia Romario kupinga rekodi za mabao ya Pele mwaka 2007.
"Kuna watu wengi ambao hawajui nini wanataka na mwishowe wanabaki kushambulia kwa maneno wakati uliopita. Lakini mimi ni mkatoliki na naamini kwamba Mungu siku zote anamsamehe mtu mjinga, hivyo na mie namsamehe mtu wa aina hiyo," Pele alisema Ijumaa.
Na katika kumjibu Pele, Romario aliandika kwenye ukurasa wa Facebook: "Jana, Pele amejibu kuhusu kauli yangu maarufu, 'Kimya, Pele ni mshairi". Ni msemo maarufu unaotumika sana, na yeye mwenye amekuwa akiupa sababu ya kukua.
"Kitu cha kipumbavu kabisa alichosema ni kwamba  yeye ni mkatoliki mkubwa. Sidhani yeye ni mkatoliki wa kiasi hicho, kama angekuwa mtu namna hiyo angemtambua mtoto wake wa kike na angeenda kwenye mazishi.
"Sasa hivi sio tu mshairi, pia ni mpumbavu." - Romario
Miaka miwili iliyopita, Romario alisema Pele anaongea upumbavu mno, baada ya Gwiji huyo wa soka kusema kwamba Romario alikuwa anajaribu kutumia uchawi dhidi ya shirikisho la soka la Brazil kufuatiwa kuachwa kwake kwenye kikosi cha Brazil kilichoshiriki World Cup 1998.


PICHA: MH NASSARI AKIWA NA LEMA KITUO KIKUU CHA POLISI ARUSHA LEO




Saturday, April 27, 2013

WEST HAM WAMUENZI MAREHEMU FOE KWA STAILI HII MPYA


Up and running: Sergio Aguero capped off a magical City move, pouncing onto David Silva's intricate pass to fire past Jussi Jaaskelainen
Sergio Aguero akiifungia Manchester City kwa pasi ya David Silva akimtungua kipa Jussi Jaaskelainen. City walishinda 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu England jioni hii na kujiimarisha katika nafasi ya pili. Tayari Man United wametwaa ubingwa wa ligi hiyo. Chini akishangilia na Nasri.

Up and running: Sergio Aguero capped off a magical City move, pouncing onto David Silva's intricate pass to fire past Jussi Jaaskelainen
Letting fly: Yaya Toure readies to unleash his howitzer, giving Jaaskelainen no chance
Acha ipae: Yaya Toure akijiandaa kuifungia City bao la pili kwa kumtungua Jaaskelainen. Chini akishangilia na wenzake.

Match-winner: Yaya Toure's dazzling strike put the game beyond the visitors
Tribute: Both sets of fans paid their respects to Marc-Vivien Foe in the 23rd minute following the Cameroonian's tragic death in 2003
Ameenziwa: Mashabiki wa timu leo wamemuenzi marehemu Marc-Vivien Foe kwa kusimama dakika ya 23 kufuatia kifo cha kiungo huyo Mcameroon uwanjani mwaka 2003.



Friday, April 26, 2013

HII NDIO KAULI YA MAMA LEMA KUHUSU JINSI ALIVYOKAMATWA MUMEWE

.
.
Taarifa za sasa kutoka Arusha ni kwamba Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi Arusha na kuhojiwa kwa tuhuma za uchochezi wa vurugu za Wanafunzi wa chuo cha Uhasibu dhidi ya Mkuu wa Mkoa Arusha juzi.
Taarifa za uhakika kutoka kwa mke wa Mh. Lema sasa hivi ni kwamba Polisi wamekataa kutoa dhamana yake na kusema mpaka jumatatu ndio itajulikana.
Namkariri Mke wa Lema akiongea na millard ayo akisema “jana usiku saa sita kasoro watu walikuja kugonga nyumbani kwetu tukamtuma kijana aende kutazama ni kina nani, aliporudi akasema ni Polisi.. sisi hatukuamini na tulikataa kwa sababu hatukujua kama ni Polisi kweli au ni watu wanataka kuitumia hiyo nafasi kufanya uhalifu, mimi nimeshinda Polisi kutwa nikifatilia gari mbona chochote hakikutokea?”
.
Picha ya liblary

“Baada ya muda kusogea ikabidi Lema aanze kuwapigia marafiki, jamaa na baadhi ya viongozi wa Chadema, kabla ya hapo pia tuliamua kupiga kengele ya kampuni ya security ambao muda mfupi baadae walikuja na gari yao huku Polisi wakiendelea na vitisho kwamba watapiga mabomu na kuvunja ukuta la sivyo Lema ajisalimishe, Viongozi wa Chadema na marafiki walipowasili wakamshauri Lema ndio akajitokeza wakati huo ni saa tisa usiku” – Mama Lema

“Alipojitokeza Polisi walimchukua na mimi nikaondoka nao, tulipofika kituoni walimtaka Lema kutoa maelezo lakini alikataa na kusema mpaka mwanasheria wake aje hivyo akapelekwa rumande, asubuhi tulipoamka na kuanza kufatilia.. R.C.O alisema yuko kwenye kikao na haongei na yeyote isipokua Mwanasheria wa Lema, walipomaliza kikao saa nane maelezo yakaanza kutolewa huku Mwanasheria akiwepo na kazi ikamalizika jioni saa 11 ambapo Polisi wamekataa kutoa dhamana mpaka Jumatatu” – Mama Lema
“shitaka kubwa lililo mbele yake ni uchochezi na kauli ambayo anadaiwa Lema kuitoa mbele ya Wanachuo cha Uhasibu kwamba dhambi kubwa kuliko zote ni uoga, na hata leo kwenye maelezo Lema amewaambia watu wa Arusha mjini hivyohivyo, kwamba dhambi kubwa kuliko zote ni uoga” – Mama Lema
Kwa kumalizia, Mke wa Mbunge Lema amesema “gari letu lililokua linashikiliwa na Polisi tumerudishiwa baada ya kutakiwa kulipia elfu 50 ya wale waliolivuta, gari liko zima kabisa………… toka nimeolewa na Lema nimeshuhudia akienda polisi zaidi ya mara 20, mara yake ya kwanza kushuhudia anapelekwa polisi ni wakati wa kampeni za Ubunge”

SOURSE:Millard Ayo

Thursday, April 25, 2013

HANS POPE AREJEA SIMBA

SASA ni shwari Simba SC.

Hivyo ndivyo unavyoweza kusema, kufuatia pande mbili zilizokuwa zinavutana, uongozi chini ya Mwenyekiti Alhaj Ismail Aden Rage na wapinzani wake kumaliza tofauti zao.

Pongezi kubwa ziende kwake, Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Zacharia Hans Poppe aliyefanikisha kumaliza mgogoro wa chini kwa chini baina ya Rage na wapinzani wake.

Akizungumza na BIN ZUBEIRY jioni hii, mpatanishi huyo wa mgogoro uliorejesha amani na umoja Simba SC, amesema: “Tofauti zilizokuwapo tumekwishazimaliza na sasa Simba SC ni shwari, tunaanza upya kazi.”

Poppe aliyepigana vita dhidi ya Nduli Iddi Amin Dada kuokoa ardhi ya Tanzania na Watanzania waliokuwa wakinyanyswa na askari na rais huyo wa zamani wa Uganda, aliongeza; “Na kwa maana hiyo, natamka rasmi, nami nimerejea ndani ya Simba SC kwa nafasi zangu zote kama nilivyoombwa baada ya kujiuzulu.”

Poppe alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili- wakati huo huo Mwenyekiti wa Friends Of Simba na aliamua kukaa kando kabisa wakati mgogoro kutofungana na upande wowote, akishughulikia amani ya klabu.

Poppe alisema kwa sasa wanalekeza nguvu zao katika kumalizia Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa heshima na baada ya hapo watatengeneza timu mpya itakayoiteka soka ya nchi hii msimu ujao.

“Tumevuna matunda ya ugomvi na migogoro katika klabu, tulianza msimu vizuri na tukawa juu kwa muda mrefu, lakini baada ya hapo naona tukalewa mafanikio tukaanza kugombana bila sababu.” “Matokeo yake ndiyo haya, tumepoteza mwelekeo, lakini madhali tumemaliza tofauti baina yetu, na tumefikia makubaliano ya msingi ya kudumisha umoja na amani ndani ya klabu, ambavyo ndivyo chimbuko la mafanikio, hakuna shaka wana Simba watafurahi tena,”alisema Hans Poppe.

Mambo yalitibuka Simba SC miezi kadhaa iliyopita kufuatia mgogoro wa chini kwa chini baina ya Rage na wapinzani wake, uliosababisha mgawanyiko hadi ndani ya uongozi.

Makamu Mwenyekiti, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ alijiuzulu sambamba na Hans Poppe na tangu hapo, Simba imekuwa ikienda kama jahazi liso na Nahodha na matokeo yake ni kutaka kuzama kwa kupoteza mwelekeo.

Matokeo yake, timu imepoteza ubingwa wa Ligi Kuu na kukosa hata nafasi ya pili, ambayo ingewawezesha kucheza Kombe la Shirikisho Afrika mwakani.

Amani inarejea Simba SC zikiwa zimebaki takriban wiki tatu kabla ya kumenyana na wapinzani wa jadi, Yanga SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Yanga SC walitaka sana kutumia mwanya wa mgogoro ndani ya Simba SC kulipa kisasi cha kufungwa 5-0 mwaka jana, lakini sasa inaonekana shughuli itakuwa pevu Mei 18 Uwanja wa Taifa.


PICHA: MKUTANO WA CHADEMA MBEYA

Picture
Picha zote zimetumwa na Tumaini Makene
Picture
Picture



Wednesday, April 24, 2013

ANGALIA MATOKEO YA DORTMUND NA REAL MADRID NA MAGOLI MANNE YA LEWANDOWSKI NA MOJA C. RONALDO YALIVYOKUWA

http://cdn.bleacherreport.net/images_root/article/media_slots/photos/000/827/539/ScreenShot2013-04-24at1.38.58PM_original.png?1366836014http://cdn.bleacherreport.net/images_root/article/media_slots/photos/000/827/543/ScreenShot2013-04-24at1.39.04PM_original.png?1366836024Save_originalOverheadgoal_originalScreenshot2013-04-24at1Goal4_originalhttp://cdn.bleacherreport.net/images_root/article/media_slots/photos/000/827/460/ScreenShot2013-04-24at1.00.50PM_original.png?1366833682Goal3_originalGoal2_originalNopenlaty_originalScreenshot2013-04-24at12Ornaldogoal_originalRonaldokick_originalScreenshot2013-04-24at11
Goal1view2_originalGoal1_original

MAMA HUYU WA KIINGEREZA AMESEMA WATANZANIA NI NGURUWE

Bibi. Sarah Hermitage ambaye ni Mwanasheria raia wa Uingereza, mwanaharakati wa kupambana na rushwa na pia mwekezaji katika shamba la Silverdale. Anapatikana @Chomachomp au http://thesilverdalecase.blogspot.com/
Bibi. Sarah Hermitage ambaye ni Mwanasheria raia wa Uingereza, mwanaharakati wa kupambana na rushwa na pia mwekezaji katika shamba la Silverdale.

Anapatikana @Chomachomp au http://thesilverdalecase.blogspot.com/
KATIKA hali inayoonyesha dharau kwa Watanzania na waumini wa Dini ya Kiislamu, Muingereza Sarah Hermitage, amefananisha Watanzania na nguruwe ambaye ni mnyama haramu kwa mujibu wa imani ya Kiislamu.
Sarah ambaye amekua akiwakashifu viongozi na wananchi wa Tanzania mara kwa mara alivuka mipaka na kufananisha Watanzania na nguruwe, baada ya kulalamikiwa kwa vitendo vyake vya kutoa maneno machafu kwa Watanzania katika mitandao ya kijamii.
Kauli hizo za Sarah amekua akizitoa kupitia mitandao ya twitter kupitia ukurasa wake wa https://twitter.com/Chomachomp kwa muda mrefu sasa bila kuchukuliwahatua zozote na viongozi wala watendaji wa serikali ya Tanzania.
Kauli ya Sarah kuita Watanzania ilianzia pale Mtanzania mmoja ambaye ni mwandishi wa habari mkongwe Mbaraka Islam, kulalamikia kitendo chake cha kutukana viongozi na Watanzania wote kwa ujumla wao bila kuwa na hoja zinazowahusu.
Huku akijua aliyewasiliana naye ni Muislamu, Sarah aliandika katika ukurasa wake kwamba “anga la Tanzania limejaa nguruwe wanaopaa, Mbaraka Islam, ni kupe wa mwezi”, akimaanisha kwamba Mbaraka Islam ni mmoja wa nguruwe wengi wanaoelea katika anga la Tanzania.
“Kwa maana yoyote anayotaka kuuaminisha umma na katika mazingira ya Tanzania na Dini yetu, haiwezekani kwamba Sarah hakujua kwamba ni kashfa nzito ya Kidini kumfananisha Muislamu na nguruwe kwa namna yoyote ile. Alijua mimi ni Muislamu alifanya hivyo kusudi.
“Huyu mama (Sarah) amefanya hivyo baada ya kuona Watanzania wamelala na hakuna anayethubutu kumgusa hasa viongozi wetu anaowatukana anavyotaka bila kuguswa na yeyote,” alisema Islam na kuongeza kwamba amechukua hatua kadhaa ambazo hajapenda kuziweka hadharani kwa sasa.
Kwa mujibu wa imani ya dini ya Kiislamu, mnyama nguruwe ni haramu na najisi na kwamba haruhusiwi kuliwa na unapomgusa unapaswa kujitakasa kwa kuoga mara saba moja ikiwa ni kwa kutumia mchanga.
Sarah alikerwa na makala aliyoandika Islam katika gazeti la Raia Mwema, ambayo  ilielezea kukerwa na maneno machafu anayoyatoa kwa Watanzania.
Katika makala hiyo, Islam alisema:
KWA takriban miaka mitano sasa, raia mmoja wa Uingereza, Sarah Hermitage amekuwa akiendesha kampeni ya kumchafua Rais Jakaya Kikwete, Serikali ya Tanzania, taasisi muhimu za nchi yetu kama vile mahakama, waandishi wa habari na hata Watanzania ambao wamekua wakimpinga.
Pamoja na kuwa kumekua na mapungufu katika serikali yake na vyombo vyake kama ilivyo kwa serikali nyingine Duniani ikiwamo ya Uingereza, Muingereza huyu amekua akitoa kashfa kwa kila jambo linaloandikwa ama kujadiliwa kuhusiana na viongozi wa Tanzania na taasisi zake na kwa kutumia lugha isiyo na staha.
Watanzania siku zote wakiwamo wanasiasa, waandishi wa habari na wanaharakati, wamekua wakiikosoa na hata kuishambulia serikali na vyombo vyake inapokosea jambo ambalo ni jema na linasaidia kuimarisha utawala bora, lakini kwa staili anayotumia Muingereza huyu ni kupitiliza mipaka na zaidi ya yote ni udhalilishaji usioweza kuvumilika kwa mtu mwenye mapenzi mema na nchi yake.
Dhumuni la Sarah Hermitage na washirika wake wakiwemo baadhi ya Watanzania ni kuzishawishi nchi za Magharibi wakianzia na Uingereza kusitisha misaada na uwekezaji katika Tanzania. Hilo angeweza kulifanya huko kwao kwa kuwasiliana na serikali yake, lakini badala yake amekuwa akitumia mitandao ya kijamii na barua pepe tena kwa kutumia lugha ya kukashifu na kudhalilisha.
Watanzania wote tuna jukumu la kutetea heshima ya nchi yetu, lakini wapo wale ambao tumewapa jukumu la kusimama mstari wa mbele. Jambo la kusikitisha ni kwamba ni watu wachache sana kama Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe ambaye ambaye amekua na ujasiri wa kumkabili Muingereza huyu, kwa kumwambia wazi kwamba kama ni misaada ana haki ya kuishawishi nchi yake kuzuia misaada kwa Tanzania lakini si kwa kudhalilisha Watanzania.
Zitto alienda mbali zaidi kwa kusema kwamba nchi nyingi tajiri duniani ikiwamo Uingereza, zimejengwa kwa kutumia rasilimali walizozipora katika nchi walizozitawala ikiwamo Tanzania na kwamba nchi hizo zinaweza pia kuendesha shughuli zake bila misaada ya dharau. Bahati mbaya sana watendaji wengine wengi ambao wanapaswa kutetea heshima yetu, hili suala limewapita, pengine kutokana na kutokua na taarifa sahihi ama kwa kutowajibika.
Jambo la kujiuliza, wale ambao miongoni mwa majukumu yao ya kila siku ni kutetea na kulinda hadhi na heshima ya nchi yetu wanafanya kazi gani? Sasa tunawalipa mishahara mikubwa na marupurupu ya nini kama hawawezi kututetea tunapodhalilishwa ama kutukanwa?
Hali hii inatufanya tukumbuke ujasiri wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye mara kadhaa aliwatunishia misuli viongozi wa mataifa makubwa walipotaka kuidhalilisha nchi yetu, sembuse raia mmoja ambaye amekua akitumia matatizo yake binafsi kutaka kuidhalilisha Tanzania na kutaka kuishinikiza serikali yake na nyingine kuichukia Tanzania.
Jinsi anavyotumia mtandao wa twitter kuchafua Tanzania
Sarah Hermitage amekua akitafuta katika taarifa za vyombo vya habari vya ndani na nje ya Tanzania vinavyoandika taarifa zozote kuhusu Tanzania na kuziongezea maneno ya kukashifu na kejeli.
Kwa mfano amekua amechukua taarifa inayomunukuu Raia Jakaya Kikwete akiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kupambana na rushwa hadi ndani ya Baraza la Mawaaziri, na yeye kuongezea maneno akisema, “kundi moja la majambazi linaliambia kundi lingine la majambazi kukamata mwizi”.
Akachukua taarifa iliyochapishwa katika vyombo vya habari ikimnukuu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikaribisha wawekezaji katika kilimo na yeye kuongeza maneno akisema, “Mheshimiwa Pinda kitakachoendelea kukandamizi uwekezaji katika kilimo cha Tanzania ni uporaji wa ardhi ya wawekezaji katika mtindo wa Mugabe (Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe).”
Amekua akidiriki kukashifu hadi majaji wote wa Tanzania kwamba wana bei akisema, “sina hakika kama unaweza kupata jaji ambaye si mla rushwa. Wote wana bei,” kauli ambayo hata Watanzania wanakua wakiitoa kwa uangalifu maana hata kama kuna majaji ambao si waadilifu, haiwezekani wakawa ni wote, kama ilivyo katika taasisi nyingine.
Raia mmoja wa Kenya anayeishi Tanzania, aliyejitambulisha kwa jina la Marigi Patrick aliandika katika mtandao kwa kusema;
“Sisi Wakenya tuna matatizo yetu na tumekua na tofauti kubwa sana za wazi wazi, lakini anapotokea raia wa kigeni kumshambulia kiongozi wetu tena kama Rais wa nchi, tunaungana na kumshughulikia. Kuna wakati Wazungu walimshambulia Rais Mwai Kibaki, sote tukisaidiwa na wabunge wetu na vyombo vya habari tulimshambulia hadi akakoma kutudharau.”
Marigi ambaye anajihusisha na biashara ya bima, anasema Watanzania bado ni wachanga katika demokrasia, ama wanadharau kila kitu bila kujua madhara yake katika hadhi na heshima ya Taifa, na ndio maana wanashindwa kutofautisha kati ya demokrasia na udhalilishaji unaofanywa na raia wa nchi nyingine kama alivyo Sarah Hermitage.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU