Facebook Comments Box

Saturday, March 7, 2015

AENDA JELA KWA KUWAHI KUFIKA KAZINI NA KUANZA KAZI YAKE MAPEMAA

Kevin McGill

Mwendesha lori la kuzoa taka kwenye majumba ya watu mji wa Sandy Spring jimbo la Georgia nchini Kevin McGill Marekani anatakiwa kwenda jela wikiendi 14 kwa kisa ni kuwahi kuchukua taka mida ya saa 11 asubuhi badala ya saa 1 asubuhi.na kuwapigia watu kelele wakiwa wamelala.

Kervin McGill yeye mwenyewe alibaki mdomo wazi baada ya kusomewa mashitaka kwamba anapochukua taka saa 11 asubuhi anawapigia kelele waliolala na inakua usumbufu kwa 

wengine na majirani hao walijaribu kuifungulia kampuni yake Kervin McGill lakini wao walisema sisi hatuondeshi hilo lori, na ikabidi kibao kimgeukie yeye na kuhukumiwa kwenda jela wikiendi 14.

Kesi hiyo imewashtua watu wengi na kuwa gumzo kwenye vyombo vya habari huku wengi wao wakiwa wamepigwa na butwaa kwa mtu kwenda jela kwa sababu ya kuwahi kufanya kazi yake. 

Mtu kama huyu alistahili kupata onyo sio kwenda jela. Hakimu alimwambia Kervin McGrill kuanzia sasa anatakiwa achukue taka saa 1 asaubuhi na saa 1 usiku tu na si vinginevyo.


WAMJUA SAID SALIM BAKHRESSA? HEBU MUONE HAPA KATIKA UZINDUZI WA STUDIO ZAKE ZA KISASA ZILIZO ZINDULIWA NA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE


a7_2b2c5.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe akiwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara pamoja na uongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Azam TV wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam.
a2_58044.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Naibu Mkurugenzi wa Azam TV Bw. Dunstan Tido Mhando wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam.
a5_f5589.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitangaza rasmi kuzinduliwa kwa studio mpya za stesheni ya Azam TV Tabata Relini jijini Dar es salaam, Pamoja naye kwenye kilinge cha utangazaji ni mmiliki wa stesheni hiyo Bw. Saidi Salim Bakhressa
a8_8c9ac.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo kutoka kwa fundi mitambo Mkuu wa Azam TV Bw. Mehdoub al Hadad juu ya namna gari la kurusha matangazo nje ya studio (OB Van) linavyofanya kazi wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam.
ssb1_82b8d.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa na Bw. Saidi Salim Bakhressa wakati alipohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam.
a6_cc23b.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara pamoja na uongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Azam TV wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam.


Wednesday, March 4, 2015

SERIKALI YASITISHA MATUMIZI YA TIKETI ZA KIELEKRONIKI KATIKA UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM

TIKETI ZA KIELEKRONIKI ZILIZO SITISHWA NA SERIKALI

Serikali imesitisha matumizi ya tiketi za kielektroniki kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia (Machi 3, 2015) hadi kasoro zilizopo katika matumizi ya tiketi hizo zitakapoondolewa.

Uamuzi huo umetangazwa Machi 3, 2015 jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Juma Nkamia mbele ya viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na benki ya CRDB.

 IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


KAPTENI KOMBA AZIKWA KIJIJINI LITUHI HUKU RAIS JAKAYA KIKWETE AKIONGOZA MAZISHI HAYO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, aliungana na mamia ya waombolezaji kumzika Mbunge wa Jimbo la Nyasa na msanii mahiri wa muziki nchini, Mheshimiwa Kepteni John Damiano Komba, kwenye makaburi ya Kanisa Katoliki katika Kijiji cha Lituhi, Wilaya ya Nyasa, Mkoa wa Ruvuma. 

Mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Songea, akitokea Dar es Salaam, kiasi cha saa tano na robo asubuhi, Rais Kikwete alikwenda moja kwa moja Lituhi, karibu kiasi cha kilomita 140 kutoka mjini Songea, kwa ajili ya mazishi ya Mheshimiwa Komba ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM). 

Rais Kikwete alijiunga na waombolezaji akiwemo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Anne Semamba Makinda kiasi cha saa tisa mchana kwa ajili ya mazishi hayo. 
 
Shughuli za mazishi za kidini ziliongozwa na Askofu John Ndimbo wa Jimbo Katoliki Mbinga.

Mwili wa Marehemu Komba uliteremshwa kaburini saa 9:30 mchana huku ukishuhudiwa na mjane wa marehemu Salome Komba na watoto wake 11. 

Rais Kikwete ameondoka Lituhi mara baada ya mazishi kurejea mjini Songea kumalizia ziara yake ya siku mbili ya kikazi mkoani Ruvuma.



SOMA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 03-03-2015



























Sunday, February 22, 2015

CHELSEA YATOKA SARE NA TIMU AMBAYO HUWA INAISUMBUA KATIKA LIGI BURNLEY

 Mshambuliaji wa Burnley akisawazisha bao na kufanya sare ya 1-1


Ivanovic akiifungia timu yake bao la kwanza katika mechi hiyo likiwa ni goli la 4 katika michezo 6 aliyocheza.
Mchezaji wa Chelsea Matic alipewa kadi nyekundu na kutolewa katika mchezaji huo baada ya kumsukuma mchezaji wa Burnley mpaka kumdondosha chini baada ya awali kumchezea rafu.
Wachezaji wa Burnley wakipongezana baada ya kufanikiwa kusawazisha wakiwa ugenini na kufanya mpambano huo kumalizika kwa kufungana 1-1.


ARSENAL YAICHAPA CRISTAL PALACE UGENINI

 Wachezaji wa Arsenal wakishangilia bao la kwanza lililofungwa katika dakika ya 8 na Sant Carzola
 Sant Carzola akishangilia baada ya kuipatia timu yake bao la kwanza likiwa ni bao lake la 7 katika msimu huu.
Straiker Force Giroud akiwatoka walinzi wa Cristal Palace na kufunga bao la pili na la ushindi kwa Arsenal lakini likiwa ni bao lake la 5 katika michezo saba aliyocheza.
Hapa Beki na kipa wa Cristal Palace wakiokoa michomo ya Monreal na Kosienly wa Arsenal


LEO NDIYO LEO FAINALI YA LIGI DARAJA LA KWANZA KATI YA MWADUI FC NA AFRICAN SPORTS YA TANGA NDANI YA AZAM COMPLEX CHAMAZI


Mwadui FC

African Sports

Fainali ya kumsaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL), inatarajiwa kufanyika leo kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Awali mchezo huo wa fainali ulikuwa umepangwa kufanyika leo kwenye dimba la Uwanja wa Taifa, lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TTF imelazimika kuhamishia mchezo huo Chamazi.

Mchezo huo wa fainali utaanza saa 10 kamili jioni, na utaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Azam TV ili kuwapa nafasi wapenzi na wadau wa soka waliopo mbali na hasa mikoani kuweza kushuhudia mchezo huo.

Bingwa wa Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na medali, huku mshindi wa pili akipata kikombe na medali pia. Viingilio vya mchezo huo ni tsh.5,000 kwa jukwaa kuu na tsh. 3,000 kwa majukwaa ya mzunguko.

Lakini pia katika uwanja huo wa Azam Cmplex kutakuwa na mpambano mwingine wa wenyeji Azam watakao cheza na Tanzania Prisons ambapo mchezo huo utaanza majira ya saa mbili kamili usiku.

Mjini Shinyanga wenyeji timu ya Stand United wataikaribisha Simba SC kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku wagonga nyundo wa jiji la Mbeya, timu ya Mbeya City wakicheza na timu ya Young Africans kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

 IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA

MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


WATAKA KUWA NA LADY JAY DEE COMMANDO, MAMAA SOME FOOD? ONA SIFA ZA MWANAUME AMTAKAE

 Judith Wambura a.k.a Lady Jay Dee hapa akiwa na aliyekuwa mumewe ambae wameachana Gardner G Habash ambae kwa sasa ni Mtangazaji wa kituo cha E-FM kilichopo Dar es Salaam.
Lady Jay Dee akiwa amesimama nyuma ya gari lake Range Rover.


Kama wewe ni Mwanaume mwenye ndoto za kuwa na Nyota huyu wa Muziki wa Tanzania angalia sifa alizo orodhesha katika mtandao wa Instagram huenda ukawa wewe.

Jide ambae ameachana na aliyekuwa mumewe kwa sasa yupo single na ameonekana kutaka kuwa na mtu mwingine ambae atakuwa na sifa ambazo amezitaja kuwa ni Anaejali na kujiheshimu, Mwenye roho ya upendo na huruma, Anaeweza kum take care financially, Asiechepuka hovyo, Asiwe tegemezi, Hata kama sio tajiri lakini asimtegemee yeye, Asiwe mlevi kupindukia wa kulala bar au kulala nje kwa "machangu" wa kinondoni au wa sehemu yoyote.

Lakini pia Jide amesema kuwa kwa sasa ana marafiki wengi lakini wengi wao ni wa kiume ambao walio wengi ni wa kutoka nje ya nchi na huwa anakutana nao kwenye mikusanyiko ya watu wengi na urafiki wao ni wa kubadilishana mawazo, kwenda dinner, na kualikana majumbani kufungua shampeni na kuchoma nyama. "Kama mmeniona nao huko We were just having fun", nothing serious alisisitiza Jide.

Amesema kwa sasa anae mpenzi wa miaka mingi sana ambae amekuwa akimpa karibia kila anachotaka kama vile, Amemjengea nyumba, amemnunulia viwanja, magari, anamlisha na kumvisha pia anamsomeshea ndugu zake, Amemfungulia Restaurant na ameahidi kumnunulia Beach House na Land Rover model ya 2015 ila hizo ni ahadi bado hajazitimiza.

Kila akitaka kwenda holiday anagharamia kila kitu, akitaka kwenda kwa Fans wa Paris analipa tena anmlipia ndege Business Class. "Sasahivi ameahidi kunilipia Trip ya Italy nikawaone kina Kayumba, Shopping na n.k tena hajawahi kunisaliti. JE WAMJUA HUYU MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI?, ANAITWA "MUZIKI".

Ila akasema maswali kuhusu mambo ya ndoa yake atayajibu siku nyingine ili aongelee maswala hayo tu hataki kuchanganya na mambo mengine maana yamesemwa mengi.


Wednesday, February 18, 2015

RAIS KIKWETE ATEUWA WAKUU WA WILAYA WAPYA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
RAIS KIKWETE ATEUA WAKUU WA WILAYA WAPYA 27
 
Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya kwa kuwateua Wakuu wapya 27, kuwahamisha vituo vya kazi 64 na wengine 42 amewabakisha kwenye vituo vyao vya kazi vya zamani.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa OWM TAMISEMI leo mchana (Jumatano, Februari 18, 2015) Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema mabadiliko hayo yamesababishwa na kuwepo kwa nafasi wazi 27 ambazo zilitokana na wakuu wa wilaya watatu kufariki dunia; kupandishwa cheo wakuu wa wilaya watano, kupangiwa majukumu mengine wakuu wa wilaya saba na kutenguliwa kwa uteuzi wa wakuu wa wilaya 12.

Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema, Rais  Kikwete amewabadilisha vituo vya kazi wakuu wa wilaya 64 na kuwabakiza kwenye vituo vyao vya zamani wakuu wa wilaya 42.

Wakuu wa Wilaya wapya 27 walioteuliwa ni:- 

Mariam Ramadhani Mtima anayeenda Ruangwa; Dk. Jasmine B. Tiisike anayeenda Mpwapwa; Pololeti Mgema (Nachingwea); Fadhili Nkurlu anayeenda Misenyi; Felix Jackson Lyaniva anayeenda Rorya na Fredrick Wilfred Mwakalebela anayeenda wilayaya Wanging’ombe.

Wengine na vituo vyao kwenye mabano ni Zainab Rajab Mbussi (Rungwe); Francis K. Mwonga (Bahi); Kanali Kimiang’ombe Samwel Nzoka (Kiteto), Husna Rajab Msangi (Handeni), Emmanuel J. Uhaula (Tandahimba); Mboni Mhita (Mufindi); Hashim S. Mgandilwa (Ngorongoro); Mariam M. Juma (Lushoto); Thea Medard Ntara (Kyela); Ahmad H. Nammohe (Mbozi); Shaban Kissu (Kondoa) na Stephen Zelothe (Musoma).

Wengine ni Pili Moshi (Kwimba); Mahmoud A. Kambona (Simanjiro); Glorius B. Luoga (Tarime); Zainab R. Telack (Sengerema); Bernard Nduta (Masasi); Zuhura Mustafa Ally (Uyui); Paulo Makonda (Kinondoni); Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na na Maftah Ally Mohamed (Serengeti).

Wakuu wa Wilaya saba ambao uteuzi wao umetenguliwa lakini watapangiwa kazi nyingine ni:- 

Brig. Jenerali Cosmas Kayombo aliyekuwa Simanjiro; Kanali Ngemela E. Lubinga (aliyekuwa Mlele); Juma S. Madaha (aliyekuwa Ludewa); Mercy E. Silla (aliyekuwa Mkuranga); Ahmed R. Kipozi (aliyekuwa Bagamoyo); Mrisho Gambo (aliyekuwa Korogwe) na Elinas A. Pallangyo (aliyekuwa Rombo).

Waziri Mkuu pia aliwataja Wakuu wa Wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na sababu za umri, kiafya na kuimarisha utendaji Serikaini na wilaya zao kwenye mabano kuwa ni:-

 James K. Ole Millya (Longido); Elias Wawa Lali (Ngorongoro); Alfred Ernest Msovella (Kongwa); Danhi Beatus Makanga (Kasulu); Fatma Losindilo Kimario (Kisarawe); Elibariki E. Kingu (Igunga); Dk. Leticia Moses Warioba (Iringa); Evarista N. Kalalu (Mufindi); Abihudi M. Saideya (Momba); Martha J. Umbulla (Kiteto); Khalid J. Mandia (Babati) na Elias Goroi (Rorya).

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMATANO, FEBRUARI 18, 2015


Monday, February 16, 2015

MWADUI FC NA TOTO AFRICAN ZAKAMILISHA IDADI YA TIMU NNE ZILIZOPANDA LIGI KUU


MWADUI FC

Timu ya Mwadui yenye maskani yake Mwadui - Shinyanga imefanikiwa kurudi ligi kuu baada ya miaka 27 tangu iliposhuka daraja hilo. 

Timu hiyo inayofundishwa na Kocha JAMHURI KIWELU "JULIO ALBERTO" Imerudi ligi kuu baada ya kuichapa timu ya Bukinafaso kwa mabao 4-1 na kuongoza katika kundi lao kwa kufikisha point 46 kileleni huku Mshindi wa pili wakiwa wana kishamapanda Toto Africans wa Jijini Mwanza ambao nao walishinda mechi yao iliyopigwa katika uwanja wa CCM - KIRUMBA kwa kuwafunga Rhino Rangers mabao 2-0 na kufikisha point 45 baada ya kuongezwa point 3 za mechi iliyokwisha kwa vurugu ya Geita.

Kwa ujumla timu zilizopanda ligi kuu ni nne ambazo ni AFRICAN SPORTS(TANGA), MAJIMAJI(SONGEA), MWADUI FC(SHINYANGA) na TOTO AFRICANS(MWANZA). Ligi ya msimu ujao itakuwa na timu 16 baada ya kupanda hizo nne na kushuka timu mbili.




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU