Facebook Comments Box

Monday, August 18, 2014

MARCO REUS NI CHAGUO SAHIHI KWA ARSENAL HII

Marco Reus
Kama watanzania wapenda Arsenal wanavyo ona kuwa winga ya kushoto na mshambuliaji imekuwa tatizo kidogo kwenye kikosi cha Arsenal. Sidhani kama Jack au Santi ndio jibu sahihi kwa hili ni kama Giroud ambavyo ameshindwa kukidhi haja pale mbele.
Ufumbuzi wa swala hili ni Marco Reus. Nadhani hamna haja ya kuwashawishi sana kuwa huyu ni chaguo sahihi bali naweza kuwaambia kuwa huyu ni mtu ambae anahitajika kwa muda huu pale Arsenal. Akisajiliwa kama winga wa kushoto nakuwa na uhakika wa makombe pale Emirate hebu angalia kidogo takwimu zake ana magoli 42, pasi za mwisho za magoli 39 katika mechi 94. Huyu ni winga mwenye uwezo wa kupenyeza kwenye msitu wa watu,kufunga na kupiga krosi ambazo kwasasa tunazikosa pale Arsenal hata ukiangalia mechi na Crystal Palace zilikosekana. Sio hayo bali huyu jamaa bi bingwa wa upigaji mipira iliyokufa.

Kila mtu anataka mshambuliaji bila kujua washambuliaji wapo ila inachotakiwa ni kuwaimarisha kwa kuwapa pasi na kutengeneza nafasi za kutosha kwa kumsajili Reus. Hebu fikiria pale mbele Reus, Sanchez na Walcott (wakibadilishana majukumu kulingana na kiwango cha timu) 

SASA TURUDI UPANDE WA UFUNDI:
Reus amekataa hela ambayo amepewa hii ni kutokana na yeye kuwa na soko kubwa. Kama £30/35 milioni zinaweza zikawashawishi Dortmund wakatuuzia mchezaji huyo na sidhani kama kuna mshabiki yoyote wa Arsenal atakaona ni hela nyingi kwa mchezaji huyu muhimu. Wakimuwekea mshahara wa £60,000, ukizingatia kwasasa tuna wajerumani pale Arsenal ambao watampa kampani ya kutosha na kumshawishi mchezaji huyu tunae Rosicky ambae ni gumzo la uingereza ambae Reus akiangalia uchezaji wake atavutiwa kucheza timu moja nae. Nafikiri huu ni muda wa kumpa Reus kiasi kikubwa tu ambacho klabu haijawahi kufikiria kwa wachezaji wa kiwango chake,tena sio klabu yetu tu tumpe kiasi ambacho hata Barcelona na Madrid wasingeweza kumpa nina uhakika ataturudishia zaidi ya hicho uwanjani.

Nafikiri hofu kubwa kwetu ni kuwa kwasasa imebaki usajili wa mchezaji mmoja, tunajiuliza amsajili winga wa kushoto,mshambuliaji au beki wa kati? Ni vizuri kujipa ujasiri kuwa tutampata Carvalho na sio Reus. Na tukimpata Carvalho nitajisikia vibaya kumkosa Reus.

Sisi ni Arsenal tunaojua biashara na najivunia kwa hilo maana biashara zetu zote huenda vizuri. Sisi sio Man City tunaotumia bila kujali kwa hiyo sidhani kama tunaweza kumpata winga mshambuliaji kwa £30 milioni na beki wa kati kwa £30 milioni, hapana sisi tunaangalia mbele zaidi hatujazi tu wachezaji.  Reus ndio mchezaji tunaemtaka kwasasa ili kuimarisha timu yetu.
Haya ni maoni yangu kama mpenda Arsenal kwa hiyo naomba nisihukumiwe,  Naipenda timu yangu na ninataka maoni yangu watu wayajue. 

Ahsanteni.
COYG!


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU