Facebook Comments Box

Sunday, February 22, 2015

WATAKA KUWA NA LADY JAY DEE COMMANDO, MAMAA SOME FOOD? ONA SIFA ZA MWANAUME AMTAKAE

 Judith Wambura a.k.a Lady Jay Dee hapa akiwa na aliyekuwa mumewe ambae wameachana Gardner G Habash ambae kwa sasa ni Mtangazaji wa kituo cha E-FM kilichopo Dar es Salaam.
Lady Jay Dee akiwa amesimama nyuma ya gari lake Range Rover.


Kama wewe ni Mwanaume mwenye ndoto za kuwa na Nyota huyu wa Muziki wa Tanzania angalia sifa alizo orodhesha katika mtandao wa Instagram huenda ukawa wewe.

Jide ambae ameachana na aliyekuwa mumewe kwa sasa yupo single na ameonekana kutaka kuwa na mtu mwingine ambae atakuwa na sifa ambazo amezitaja kuwa ni Anaejali na kujiheshimu, Mwenye roho ya upendo na huruma, Anaeweza kum take care financially, Asiechepuka hovyo, Asiwe tegemezi, Hata kama sio tajiri lakini asimtegemee yeye, Asiwe mlevi kupindukia wa kulala bar au kulala nje kwa "machangu" wa kinondoni au wa sehemu yoyote.

Lakini pia Jide amesema kuwa kwa sasa ana marafiki wengi lakini wengi wao ni wa kiume ambao walio wengi ni wa kutoka nje ya nchi na huwa anakutana nao kwenye mikusanyiko ya watu wengi na urafiki wao ni wa kubadilishana mawazo, kwenda dinner, na kualikana majumbani kufungua shampeni na kuchoma nyama. "Kama mmeniona nao huko We were just having fun", nothing serious alisisitiza Jide.

Amesema kwa sasa anae mpenzi wa miaka mingi sana ambae amekuwa akimpa karibia kila anachotaka kama vile, Amemjengea nyumba, amemnunulia viwanja, magari, anamlisha na kumvisha pia anamsomeshea ndugu zake, Amemfungulia Restaurant na ameahidi kumnunulia Beach House na Land Rover model ya 2015 ila hizo ni ahadi bado hajazitimiza.

Kila akitaka kwenda holiday anagharamia kila kitu, akitaka kwenda kwa Fans wa Paris analipa tena anmlipia ndege Business Class. "Sasahivi ameahidi kunilipia Trip ya Italy nikawaone kina Kayumba, Shopping na n.k tena hajawahi kunisaliti. JE WAMJUA HUYU MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI?, ANAITWA "MUZIKI".

Ila akasema maswali kuhusu mambo ya ndoa yake atayajibu siku nyingine ili aongelee maswala hayo tu hataki kuchanganya na mambo mengine maana yamesemwa mengi.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU