Facebook Comments Box

Saturday, February 14, 2015

HUU NDIO UKWELI KWA YANAYO ENDELEA AMBONI TANGA

Kamishna wa Polisi Operesheni na Mafunzo Paul Chagonja ametoa maelezo ya kile kinachoendelea Tanga. Kumekuwa na maneno mengi katika mitandao ya kijamii kuhusu yanayo endelea huko Tanga. Hii imepelekea Kamishna huyo kutoa taarifa

Katika taarifa yake ameelezea kuwa manamo tarehe 26 mwezi wa kwanza mwaka huu majira ya saa tano usiku polisi wakiwa katika doria walivamiwa na majambazi na kuporwa silaha na kujeruhiwa.Polisi wakishirikiana na Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) walifanya upelelezi na kugundua zilipofichwa silaha walipofika eneo la tukio ndio yakatokea majibizano ya risasi kati ya majambazi na polisi. Majibizano hayo ya risasi yamewajeruhi askari sita na mpaka sasa msako unaendelea.

Hapa chini ni taarifa ya Kamishna Chagonja





Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU