
Afisa Habari wa TFF Baraka Kizuguto
Kamati ya
 Uendeshaji na Usimamizi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) 
imethibitisha ushindi wa pointi 3 na mabao matatu kwa timu za Majimaji na 
Toto Africans baada ya mechi zao za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) 
kuvurugika kutokana na sababu mbalimbali.
Toto 
Africans imepewa ushindi huo kwa mujibu wa Kanuni ya 41(3) ya FDL baada 
ya vurugu za washabiki wa Geita Gold kusababisha mechi hiyo iliyochezwa 
Februari 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita kuvunjika 
dakika ya 12.
Pia 
Kamati hiyo iliyokutana Dar es Salaam jana (Februari 12 mwaka huu) 
imezuia mechi za FDL kuchezwa kwenye uwanja huo ambao hauna uzio wa 
kutenganisha wachezaji na washabiki kwa sababu za kiusalama.
Naye 
mchezaji Venance Joseph wa Geita Gold ambaye alimpiga kichwa refa 
akipinga adhabu ya penati iliyotolewa dhidi ya timu yake kwenye mechi 
hiyo amesimamishwa wakati akisubiri kosa lake kusikilizwa na Kamati ya 
Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Malalamiko
 ya Friends Rangers kwenye mechi dhidi ya Majimaji yametupwa na kupigwa 
faini ya sh. 500,000 kwa kusababisha mchezo huo uliochezwa Januari 29 
mwaka huu Uwanja wa Majimaji mjini Songea kuvunjika dakika ya 39. Adhabu
 hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 28(4) ya FDL.
Friends 
Rangers imepoteza mechi hiyo kwa mujibu wa Kanuni ya 28(1) ya FDL, 
Majimaji kama ilivyo Toto Africans imepewa ushindi wa pointi tatu na 
mabao matatu.
Naye 
Kocha wa Friends Rangers, Herry Chibakasa (Mzozo) suala lake limepelekwa
 kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF ili aweze kuchukuliwa hatua za 
kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni ya 39(8) ya FDL kwa kuhamamisha vurugu 
kwenye mechi dhidi ya Majimaji.
Mwamuzi 
John Mafuru wa Mbeya aliyechezesha mechi ya Majimaji na Friends Rangers 
amefungiwa miezi 12 (kumi na mbili) kwa kutozingatia sheria kiasi cha 
kuvuruga mchezo. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 37(1) ya FDL.
Pia 
Kamishna wa mechi hiyo Kim Rajab wa Dodoma amefungiwa miezi 12 (kumi na 
mbili) kwa mujibu wa Kanuni ya 38(1) ya FDL kwa kutoa taarifa zisizo 
sahihi.
Lipuli ya
 Iringa imepewa ushindi wa mabao matatu na pointi tatu baada ya timu ya 
KMC (Tessema) kumchezesha mchezaji Morris Paulo Katumbo aliyekuwa na 
kadi tatu za njano kinyume na Kanuni ya 41(12) ya FDL. Katumbo ambaye 
alipata kadi hizo kwenye mechi namba 85, 100 na 112 alicheza mchezo huo 
uliomalizika kwa timu ya KMC kuibuka na ushindi wa bao 1-0.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog