Facebook Comments Box

Saturday, February 14, 2015

APPLE SASA WAJA NA GARI LISILOTUMIA MAFUTA

Gazeti la Wall Street Journal linayo ripoti kuwa watengenezaji wa simu maarufu ya iPhone na kifaa cha iPad, Apple wanajishughulisha kutengeneza gari litakalotumia umeme ikiwa ni changamoto kwa kampuni ya Telsa inayotawala soko hilo kwa sasa.

Taarifa hiyo ya WSJ haijamtaja mtoboa siri hiyo zaidi tu ya kusema kuwa ni mwajiriwa wa Apple anayefanya kazi katika mradi huo.

Mtoa habari huyo ametanabahisha kuwa wapo watu mamia kadhaa wanaofanya kazi kwa siri kutengeneza gari hilo la mradi uliopewa jina la "Titan" na tayari wameshaunda muonekano unaoelekea kabisa kufanana na 'minivan'. 

Msemaji rasmi wa kampuni ya Apple alipoulizwa kuhusu hilo alikataa kuthibitisha au kukanusha taarifa hizo.

Nalo gazeti la Financial Times lina habari ambayo chanzo chake ni mtu ambaye hakutaka kutajwa, akisema kuwa wafanyakazi wa Apple wamekuwa wakitafiti kuhusu vipuri vya magari katika eneo moja huko Silicon Valley.

Waajiriwa wa hivi karibuni katika kampuni ya Apple ni pamoja na mkuu wa kitengo cha utafiti cha Mercedes-Benz katika tawi la Silicon Valley.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU