Facebook Comments Box

Saturday, February 14, 2015

TAMBWE WA KIMATAIFA: APIGA MBILI ZILIZOIPA YANGA USHINDI DHIDI YA BDF YA BOTSWANA

Amis Joselyn Tambwe akishangilia goli lake pamoja na Simon Happygod Msuva
YANGA Leo ndani ya Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam imeichapa Klabu ya Botswana BDF XI Bao 2-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Awali ya Mashindano ya CAF ya Kombe la Shirikisho.
 
Bao zote za Yanga zilifungwa na Straika wao Amisi Tambwe anaetoka Burundi moja katika kila Kipindi.
Tambwe akishangilia goli lake na Mrisho Ngassa na Msuva ambao ndio wapishi wa magoli yake.

Tambwe alifunga Bao la Kwanza Dakika ya Kwanza tu ya Mchezo alipounganisha kwa Kichwa Krosi ya Simon Msuva na kupiga Bao la Pili katika Dakika ya 55 pia kwa Kichwa baada ya Krosi safi ya Mrisho Ngassa.
Mrisho Ngassa akichanja mbuga


Timu hizi zitarudiana huko Botswana Wiki mbili baadae na Mshindi wake atatinga Raundi ya Kwanza kucheza na Mshindi kati ya Sofapaka ya Kenya na FC Platinum ya Zimbabwe.
Hapo Kesho Jumapili, Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam FC, watakuwa kwao Azam Complex huko Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam kuivaa El Merreikh ya Sudan katika Mechi ya Raundi ya Awali ya CAF CHAMPIONZ LIGI.
Timu nyingine mbili za Tanzania ambazo pia zimo michuano ya CAF Barani Afrika ni KMKM na Polisi, zote za toka Zanzibar, Wikiendi hii zinaanzia Ugenini kwa KMKM kucheza Sudan na Al Hilal kwenye CAF CHAMPIONZ LIGI  na Polisi kucheza Nchini Gabon na CF Mounana kwenye Kombe la Shirikisho
Mchezaji wa BDF akimfanyia rafu Haruna Niyonzima



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU