Facebook Comments Box

Saturday, February 14, 2015

PIKIPIKI YAO YACHOMWA BAADA YA KUKWAPUA SIMU YA MWANADADA MMOJA

 Pikipiki hiyo ikiteketea kwa moto.
 Wananchi wakishuhudia pikipiki hiyo ikiteketea.
Wananchi wakipiga picha pikipiki hiyo.

Kamera yetu mtaani:

Wizi wa kukwapua kwa kutumia Pikipiki umeshamiri sana Jijini Dar es Salaam kwa watumiaji hao wa pikipiki kukwapua vifaa kama simu za mikononi, mabegi ya wanawake maarufu kama "vipima joto", laptop na vitu kama hivyo.

Kuna vijana wawili waliwahi kuchomwa moto baada ya kutimiza siku zao arubaini kama msemo usemavyo kuwa "Za Mwizi arubaini" katika maeneo ya Tabata-Liwiti.

Hali hiyo ilitokea tena katika maeneo ya Hospitali ya Ocean Road ambapo wataalamu hao wa kuiba kwa pikipiki walipokutwa na zahma hiyo baada ya kumkwapulia simu mwanadada mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja na wao kukimbia ndipo msamaria mmoja akawakimbiza kwa gari lake na watu hao kuzidiwa ujanja na kukamatwa katika eneo hilo na pikipiki yao kuchomwa moto kama inavyoonekana pichani.






Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU