Saturday, June 8, 2013
Friday, June 7, 2013
KIEMBA: MIMI NI MCHEZAJI HURU NA BADO SIJASAINI YANGA
KWA
mara ya kwanza, kiungo Amri Ramadhani Kiemba ameibuka na kukanusha
kusaini Yanga SC, ingawa amesema yeye bado mchezaji huru, kwa kuwa hadi
sasa hajasaini timu yoyote baada ya kumaliza Mkataba wake Simba SC.
Akizungumza Kiemba alisema kwamba hajasaini timu yoyote hadi sasa na anajitambua kama mchezaji huru.
Alipoulizwa
kuhusu mustakabali wake, Kiemba alisema kwa sasa akili yake ipo kwenye
kuisaidia timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars iweze kukata
tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia.
“Sasa
hivi ukiniuliza mambo ya klabu, utakuwa unanionea tu. Nipo katika kambi
ya timu ya taifa, fikra zangu ni majukumu yangu ya kitaifa. Nadhani
baada ya hapa, nitazungumzia hayo mambo,”alisema Kiemba.
Kiemba
aliibua wasiwasi mkubwa kwa wapenzi wa Simba SC, baada ya kuvuma kwa
habari amesaini Yanga SC, huku Mkataba wake ukiwa umemalizika Msimbazi.
Na anaonekana mtu asiye na wasiwasi kabisa kuhusu mustakabali wake- pengine inatokana na kiwango chake cha juu hivi sasa.
Stars inashika nafasi ya pili
katika Kundi C, kuwania tiketi ya Kombe la Dunia mwakani Brazil, ikiwa
na pointi sita nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba, ambayo kesho
itakuwa ugenini ikimenyana na Gambia katika mchezo mwingine wa kundi
hilo.
Stars
ilitua hapa Jumatatu ikitokea Ethiopia ambako iliweka kambi ya wiki
moja na kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Sudan, ulioisha kwa sare ya
bila mabao.
Kabla
ya kuja hapa, Stars iliweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya
Tansoma, Dar es Salaam ikijifua Uwanja wa Karume na siku chache kabla ya
kuondoka ilialikwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete, aliyewapa hamasa kwa
hotuba nzuri.
SOURSE: BIN ZUBEIRY
MWANAMKE AFARIKI AKIJARIBU KOTOA MIMBA
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe ACP Fulgency Ngonyani akizungumza na
mwandishi wa Mtandao Huu bwana Prosper Mfugale Juu ya Tukio Hilo.
Mkazi
Mmoja wa Mtaa wa Idundilanga Mjini Njombe Yasinta Mdetele Mwenye Umri
wa Miaka 25 Amefariki Dunia Wakati Akijaribu Kutoa Mimba.
Amesema Marehemu Alikutwa Chumbani
Kwake Akiwa Amefariki Huku Pembeni Yake Kukiwa na Mtoto wa Kike Ambae
Pia Alikutwa Amefariki na Kuongeza Kuwa Marehemu Hakuacha Ujumbe Wowote
na Hakuna Mtu Yoyote Anaeshikiliwa Kutokana na Tukio Hilo.
Ameongeza Kuwa Jeshi la Polisi
Linaendelea na Uchunguzi wa Tukio Hilo na Kutoa Wito Kwa Wananchi Kuacha
Vitendo Vya Utoaji Kwani ni Kosa la Kisheria na Pia Linaweza
Kuhatarisha.
Thursday, June 6, 2013
MAREKANI WAANDAA SHERIA ITAKAYO KATAZA WATU KUVAA MLEGEZO

Sina
shaka umeshasikia style za uvaaji wa suruali hususan kwa wanaume zenye
majina kama mlegezo au kata k, au yawezekana ukawa huzijui kwa majina
lakini umeshashuhudia vijana wamevaa suruali chini ya makalio.
Kama
ambavyo mabinti wamekuwa wakilaumiwa kwa mavazi ya kuonyesha miili yao
hasa sehemu nyeti, na upande wa wanaume wamekuwa wakilalamikiwa kwa
style hiyo ya uvaaji ambayo imeonekana kuigwa hata na vijana wadogo
ambao bado wako shuleni.
Katika hali
ya kukerwa na tabia ya vijana kuvaa suruali chini ya makalio uongozi wa
Wildwood, New Jersey nchini Marekani umeandaa sheria mpya itakayoweza
kuwadhibiti wale wote wenye tabia hiyo ya kuvaa mlegezo na kukatiza
mitaani.

Sheria
hiyo inaelekeza wavaaji wote wa suruali, kaptura, mavazi ya kuogelea na
sketi zisivaliwe chini ya inchi 3 kutoka kiunoni mwa mvaaji.
Mayor wa
Wildwood Ernie Troiano Jr. aliwaambia waandishi wa habari kuwa
amechoshwa na malalamiko anayoyapata juu ya vijana wanaotembea makalio
nje kwa kushusha suruali zao kupita kiasi.
HII NDIO KAULI YA M 2 THE P BAADA YA KUFIKA TANZANIA KUMZIKA MANGWEA
Rafiki wa wa karibu wa marehemu Albert Mangwea aliyekuwa amelazwa nchini
Afrika Kusini amerejea Tanzania na yuko njiani akielekea mkoani
Morogoro kwaajili ya kushiriki mazishi ya swahiba wake Mangwea jioni ya
leo (June 6).Akizungumza na Times Fm asubuhi hii Mgaza Pende a.k.a M 2
The P amewashukuru watanzania kwa kumuombea japo hali yake bado haijawa
nzuri sana lakini ameamua kurudi Tanzania kuja kumzika ndugu yake
Mangwea. “Ndugu zangu watanzania mimi ni Mgaza Pende M 2 The P
nawashukuru sana kwa kuniombea mpaka muda huu, nimeweza kuwasili
Tanzania salama na tutakuwa pamoja kwenda kumzika ndugu yangu kipenzi
changu Albert Mangwea, nawashukuru sana watanzania kwa kuniombea
asanteni na endeleeni kuniombea hali yangu bado haijawa nzuri zaidi,
asanteni,” alisema. Msikilize hapa
PICHA ZA UTOAJI WA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MANGWEA MOROGORO
Meza kuu
hii ikiwa ni maandalia ya kuuwaga mwili wa msanii marehemu Albert
Mangwea aliyefariki dunia na anatarajiwa kuzikwa leo mkoani
morogoro.Utaratibu huu umeandaliwa katika uwanja wa jamuhuri mkoani
morogoro kwa lengo la kuwapa fursa wakazi wa mji huo kupata nafasi za
kuuwaga mwili huo kabla ya maziko
Umati
mkubwa wa wakazi wa morogoro waliojitokeza katika zozi za kuwaga mwili
wa msanii huyo mchana huu kabla ya maziko yake leo.Marehemu albert mangwea alifariki wiki
iliyopita nchini afrika kusini na maziko yake yatafanyika leo mkoani
hapa.

Mama Mzazi wa Mangweha, Denisia Mangweha akiwa nyumbani kwake kabla ya safari kuelekea Uwanja wa Jamhuri.

Mkuu
wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera asubuhi hii amefika nyumbani kwa Mama
Mangwea eneo la Kihonda Mazimbu Road na kumpa pole kwa niaba ya wakazi
wote wa mkoa wa Morogoro. Baada ya kutoa pole, Mhe. Bendera aliongoza
umati wa watu kutoka Kihonda kuelekea Uwanja wa Jamhuri kwa shughuli za
kuaga mwili wa Albert Mangwea aliyefariki dunia Mei 28 mwaka huu nchini
Afrika Kusini. Mangwea anatarajiwa kuzikwa katika makaburi ya Kihonda
nje ya Kanisa la Mtakatifu Monica jirani kabisa na alipozikwa baba yake
mzazi Mzee Keneth Mangwea.
MAJANGA YAZIDI MUANDAMA MR. NICE SASA MKATABA WAKE NA GRAND PA RECORDS YA KENYA WAVUNJWA
Mwanamuziki aliyevumbua staili ya muziki ya TAKEU (Tanzania Kenya Uganda), Mtanzania Lukas Mkenda aka Mr Nice amepoteza mkataba wake na kampuni ya kurekodi muziki ya nchini Kenya, kwa kile kilichoelezwa na kampuni hiyo kuwa ni tabia ya Mr Nice ya uvivu, ulevi, asiyeaminika na asiye na ushirikiano.
Zaidi ya maandishi yaliyoandikwa na GrandPa Records kwenye ukurasa wao wa Facebook, pia wamezungumzia suala hilo walipohojiwa na kituo cha EA Radio ambapo wamesema Mr Nice amesema ataendelea kubaki mjini Nairobi nchini Kenya akitafuta kujiweka sawa.
Wednesday, June 5, 2013
KOCHA WA YANGA AWASILI KWA AJILI YA KUINOA TIMU KWA AJILI YA MSIMU MPYA
![]() |
Kocha Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Ernie
Brandts (kulia) baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar
es Salaam usiku wa leo akitokea kwao Uholanzi kwa mapumziko mafupi
baada ya kumaliza msimu, tayari kuanza maandalizi ya kikosi chake kwa
msimu mpya. Aliyemlaki kushoto ni Meneja wa Yanga SC, Hafidh Saleh.
|
![]() |
| Anaondoka Airport |
![]() |
| Baada ya kutua, kitu cha kwanza aliwasha simu yake |
![]() |
| Anafungua mlango wa gari lake apakie mizigo |
![]() |
| Anafungua mlango wa nyuma apakie mizigo |
![]() |
| Hahitaji msaada wa mtu, anapakia mwenyewe |
![]() |
| Anafunga mlango baada ya kupakia |
![]() |
| BIN ZUBEIRY anaondoka baada ya kumaliza kazi yake |
![]() |
| Brandts naye anapanda gari lake |
![]() |
| Anapiga stata... |
![]() |
| Anaondoka Airport |
POLISI WATUMIA MBWA KUTAWANYA WATU LEADERS BAADA MUDA WA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KUISHA
Asakari
Polisi wakitumia mbwa kutawanya maelefu ya watanzania waliotaka kuuaga
mwili wa Mangwea baada ya muda uliopangwa kukamilikaASKARI wa Jeshi la Polisi walilazimika kutumia Mbwa kuwatawanya mamia ya Watanzania waliojitokeza kuuaga mwili wa marehemu Albert Mangwea lakini wakashindwa baada zoezi hilo kukatishwa.
Mangewa alifariki Dunia nchini Afrika Kusini katika Jiji la Johannesburg Mei 28 mwaka huu na kusafirishwa kuja nchini jana jioni, mamia hao wa watanzania wameshindwa kuuaga mwili wa kipenzi chao baada muda ulioapngwa kukamilka huku wakibaki katika foleni ndefu.
Kitendo cha Kamati ya maandalizi kukatisha zoezi la kuuaga mwili wa marehemu kwa sababu ya muda uliopangwa kukamilika iliwashangaza mamia ya watu waliokuwa kwenye foleni ya kusubiri kupata nafasi ya kutoa heshma zao za mwisho mbele ya Jeneza la Mangwea.
Zoezi hilo liloanza saa 2:30 asubuhi imesitishwa saa 6:30 mchana kwa saa za Afrika Mashariki na Kati, na msafara ukiongozwa na Askari wa Jeshi la Polisi pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama waliokuwa katika Viwanja vya Leaders Club.
Barabarani Asakari wa Kikoso Cha Usalama Barabarani pia walijiapanga vizuri kuhakikisha kwamba msafara wa mwili wa marehemu unapita vizuri katika maeneo yaliokuwa yamepangwa kuelekea mjini Morogoro.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Mr Blue alifika katika viwanja hivyo akiwa amechelewa na kukosa muda wa kuuaga mwili wa Mangwea lakini alipokutana na mashabiki wa muziki wake aliweza kusimama na kuwapa pole.
Mwili wa Mangwea hivi sasa uko safarini kuelekea Mjini Morogoro ambapo utalala nyumbani kwa mama yake na kesho uwakazi wa Mji huo pia watapata nafasi ya kutoa heshma zao za mwisho
Subscribe to:
Posts (Atom)


























