Facebook Comments Box

Thursday, June 6, 2013

PICHA ZA UTOAJI WA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MANGWEA MOROGORO

Meza kuu hii ikiwa ni maandalia ya kuuwaga mwili wa msanii marehemu Albert Mangwea aliyefariki dunia na anatarajiwa kuzikwa leo mkoani morogoro.Utaratibu huu umeandaliwa katika uwanja wa jamuhuri mkoani morogoro kwa lengo la kuwapa fursa wakazi wa mji huo kupata nafasi za kuuwaga mwili huo kabla ya maziko

Umati mkubwa wa wakazi wa morogoro waliojitokeza katika zozi za kuwaga mwili wa msanii huyo mchana huu kabla ya maziko yake leo.Marehemu albert mangwea alifariki wiki iliyopita nchini afrika kusini na maziko yake yatafanyika leo mkoani hapa.


 Mama Mzazi wa Mangweha, Denisia Mangweha akiwa nyumbani kwake kabla ya safari kuelekea Uwanja wa Jamhuri.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akiwasili nyumbani kwa Mama mzazi wa Mangweha.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera asubuhi hii amefika nyumbani kwa Mama Mangwea eneo la Kihonda Mazimbu Road na kumpa pole kwa niaba ya wakazi wote wa mkoa wa Morogoro. Baada ya kutoa pole, Mhe. Bendera aliongoza umati wa watu kutoka Kihonda kuelekea Uwanja wa Jamhuri kwa shughuli za kuaga mwili wa Albert Mangwea aliyefariki dunia Mei 28 mwaka huu nchini Afrika Kusini. Mangwea anatarajiwa kuzikwa katika makaburi ya Kihonda nje ya Kanisa la Mtakatifu Monica jirani kabisa na alipozikwa baba yake mzazi Mzee Keneth Mangwea.
943280_10152915710755525_916679441_n
 Wakazi wa mjo wa morogoro waanza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu albert Mangwea kabla ya kumpeleka katika Nyumba yake ya Milele. Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahala Pema.




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU