Facebook Comments Box

Friday, June 7, 2013

MWANAMKE AFARIKI AKIJARIBU KOTOA MIMBA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe ACP Fulgency Ngonyani akizungumza na mwandishi wa Mtandao Huu bwana Prosper Mfugale Juu ya Tukio Hilo.
Mkazi Mmoja wa Mtaa wa Idundilanga Mjini Njombe Yasinta Mdetele Mwenye Umri wa Miaka 25 Amefariki Dunia Wakati Akijaribu Kutoa Mimba.

Kamanda wa Polisi Mkoani Njombe Fulgency Ngonyani Amethibitisha Kutokea Kwa Tukio Hilo na Kusema Kuwa Tukio Hilo Limetokea June Tano Mwaka Huu Majira ya Saa Tatu Asubuhi Baada ya Kunywa Kinywaji Kinachodaiwa Kuwa na Sumu.
Amesema Marehemu Alikutwa Chumbani Kwake Akiwa Amefariki Huku Pembeni Yake Kukiwa na Mtoto wa Kike Ambae Pia Alikutwa Amefariki na Kuongeza Kuwa Marehemu Hakuacha Ujumbe Wowote na Hakuna Mtu Yoyote Anaeshikiliwa Kutokana na Tukio Hilo.
Ameongeza Kuwa Jeshi la Polisi Linaendelea na Uchunguzi wa Tukio Hilo na Kutoa Wito Kwa Wananchi Kuacha Vitendo Vya Utoaji Kwani ni Kosa la Kisheria na Pia Linaweza Kuhatarisha.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU