Facebook Comments Box

Friday, October 31, 2014

SHEIKH SORAGA UNAJICHANGANYA NA UNAPOTOSHA

Sheikh Fadhil S. Soraga
Hivi karibuni kumekuwa na barua ya katibu wa mufti wa zanzibar Sheikh Fadhil S. Soraga kilichonichanganya ni Katibu huyo kuto ikanusha barua hiyo ambayo haina kichwa cha juu cha barua na anuani (Headed letter). Ukiiangalia utaiona imekaa kama tangazo na chini ina saini ya sheikh huyo.Nadhani wengi wetu hatuuijui saini ya Sheikh Soraga na huenda watu wameitumia vibaya ili kumdhalilisha. Kingine kinacho nichanganya ni kuwa kikao kilifanyika tarehe 18 mwezi wa 8 kwanini leo ndio iwekwe kwenye mitandao ya kijamii na iwe gumzo?

Nahisi kuna watu wanataka kuwavuruga waislam wa Zanzibar au kuanzisha mjadala huu ili baadae walipitishe maana ni dhahiri kuwa ile kuswali kufuata uislam na idadi ya waislam wa Zanzibar ina waumiza.

Labda tuzungumze upande wa pili huenda ni kweli Sheikh Soraga ameandika maana hawa BAKWATA kutumiwa ni raisi sana (Naomba wanisamehe kwa kauli hii lakini ndio ukweli) watakuwa wameambiwa na mtu mmoja mwenye hela ambae huwapa vijisenti sasa wamelileta hili. Wakasahau kuwa ikiishakuhusu swala atawaambia hata adhana na kwenda msikitini pia inamkera maana inaonesha haridhiki na uislam kabisa. Inakuwaje asichukizwe na adhana ambayo hutolewa kwa nguvu na kuna wakati mtu hugeuka kulia na kushoto ili kutawanya sauti. Aje achukizwe na nyiradi ambazo husemwa na imam mara moja tu na wengine kufuatiliza kwa mdomo.

Naomba BAKWATA wawe wanafikiria kidogo kabla ya kuamua jambo. Kwani huko kuna matamasha ya filamu na mziki ambayo yanakesha usiku kucha na sijasikia malalamiko. Mi nina uhakika wameanza hapo ila watakuja mpaka kwenye adhana.

Tangazo/Barua ya katibu wa mufti Zanzibar



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU