Facebook Comments Box

Sunday, March 3, 2013

YALIYOJIRI KWENYE KILIMANJARO MARATHON LEO: WAKENYA WAENDELEA KUTAMBA


Washiriki wa Kilimanjaro Marathon wakiwa tayari kabisa kwa ajili ya kukimbia
Vituko hafikukosekana wazungu hawa wao hawakukimbia marathon ila wametembea mpaka wamemaliza

Afisa ujasiliamali watu wa Kilimanjaro Christian Medical University College Victor Selengia katikati akiwa na mwanafunzi wa mwaka wa udakitari Carl Jacob(Kulia) na mwanafunzi wa udakitari mwaka wa nne Nico (kushoto) wakifurahia medali zao baada ya kumaliza kilometa 21
Dr Fransis akifurahia medali na |Carl baada ya kumaliza kilomita 21
Dr Sudai (kulia) akiwa na Dr Joseph (katikati) wakifurahia medali zao

Mwanafunzi wa udakitari David Majule akishuka kumalizia kwa kasi sana. Ameiambia KITONGONI kuwa mwaka huu ameweza kuvunja rekodi yake kwa kupunguza zaidi ya dakika 32 kutoka muda alio utumia mwaka jana. Amekuwa akishangazwa na watanzania kufanya vibaya katika haya mashindano na kuaacha kila mwaka mshindi akitokea Kenya na wakati mashindano yanafanyika Tanzania. Ameomba viongozi wa chama cha riadha wajiangalie upya na ikiwezekana wawajibike kwa hili

Principal Investigator wa MEPI Tanzania kutokea marekani akifurahia medali yake baada ya kumaliza kilomita 21 na Carl Jacob

Motta, Carl na Kimario baada ya kumaliza mbio. \Wanafunzi wengi wa KCMUCo wameshiriki kwenye mashindano haya na kufanya vyema. Japo ushindi umeenda kwa wakenya

Wenye medali zao wakishuka kwa kasi




Wanariadha kutoka Nchini Kenya wameendeleza Umwambawao katika mbio za Nyika za Kilimanjaro ‘Kilimanjaro Marathon 2013’ zilizofanyika leo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Wakenya walidhihirisha umwamba katika Mbio za Kilometa 42 baada ya Mkimbiaji wao Kipsang Kipkemoi kunyakua nafasi ya kwanza katika mbio hizo za mwaka huu upande wa wanaume na Wanawake ilinyakuliwa na Mwana dada Edna Joseph alebeba Medali ya Dhahabu.

Nafasi ya pili hadi ya tano kwa wanaume ni Julius Kilimo, Dominick Kiagor, Onesmo Maithiya Loshile Moikari ambapo upande wa wanawake ni Eunice Muchiri, Frida Too, Rosaline David na Jane Kenyara.
Jumla ya wakimbiaji 65000 walishiriki mbio za Kilimanjaro Marathon 2013.
Kocha wa Taifa Stars Kim Poulsen akiwa na Dr Josephine



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU