Facebook Comments Box

Thursday, October 17, 2013

SHABIKI WA YANGA AMESEMA ATAJINYONGA KAMA SIMBA ITAIFUNGA YANGA



SHABIKI maarufu wa Yanga, Steven Mwamwala amedai kuwa, kama wakifungwa na Simba mechi ya Jumapili ijayo itakayochezwa Uwanja wa Taifa, atajinyonga.

Na akamsisitizia mcheza filamu, Wema Sepetu afike uwanjani kuona mechi ya Simba na Yanga Jumapili ili ampe zawadi yake ya jezi ya Yanga aliyoigharamia Sh45,000.

Mwamwala ana historia na Yanga ilipopigwa mabao 5-0 aliangua kilio cha nguvu na video zake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Kauli ya shabiki huyo inakuwa mzigo kwa wachezaji wa Yanga kama, Athuman Idd ‘Chuji’, Kelvin Yondani, Mrundi Didier Kavumbagu na Wanyarwanda Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ kuhakikisha wanafanya vizuri na kuokoa maisha ya kijana huyo mwenye miaka 31.

Aliliambia Mwanaspoti kuwa: “Nimeandaa kamba ya katani kabisa, nimeificha na siwezi kusema nilipoiweka kama Yanga itafungwa mchezo huo, nitajinyonga ili kupoteza uhai wangu. Unajua inauma sana mnapofungwa, nataka timu yangu ishinde Jumapili ili niwe na amani kwa ushindi wowote ule ilimradi tutoke na pointi tatu.”

Kuhusu, Wema shabiki huyo alisema anampenda sana kama dada yake na anatamani akutane naye.

“Nimemtafuta sana na naomba siku hiyo aje kwa sababu nimemwandalia zawadi. “Nimemnunulia jezi ya Yanga na tayari nimeiandika jina la Wema, imenigharimu Sh 45,000,” alifafanua Mwamwala ambaye anaishi Tabata Segerea jijini Dar es Salaam.

CHANZO: MWANASPOTI


Wednesday, October 16, 2013

WANACHAMA WA YANGA KUPIGA KURA ILI KUIBADILI CLUB KUWA KAMPUNI

Uongozi wa klabu ya Young Africans leo umetangaza rasmi kuanza kwa zoezi la kupiga kura ya NDIYO  juu ya uundwaji wa kampuni au kura ya  HAPANA kwa kutoridhia klabu kuwa kampuni maazimio yaliyofikiwa katika mkutano mkuu uliofanyika Januari 16, 2013.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga kaimu katibu mkuu Lawrence Mwalusako amesema zoezi hilo linanza leo kwa wanachama hai kufika makao makuu ya klabu na kupiga kura ya NDIYO au HAPANA na zoezi hilo litaendelea mpaka novemba 10, 2013.
Ifuatayo ni Taarifa kwa Wanachama na Waandishi wa Habari
MAONI YA WANACHAMA YA KUUNDA KAMPUNI
Katika Mkutano wa Kawaida wa Wanachama wa YANGA uliofanyika tarehe 16 Januari 2013 Mwenyekiti kwa niaba ya Kamati ya Utendaji aliwapa Wanachama wafikirie mapendekezo ya YANGA kuwa Kampuni ama kutokuwa Kampuni kisha kuyawasilisha kwa Katibu Mkuu wa YANGA.
Nachukua nafasi hii kuwaambia Wanachama wa YANGA kuwa kuanzia leo tarehe 16 Oktoba 2013 mpaka tarehe 10 Novemba 2013, kutakuwa na sanduku moja (1) hapa Klabuni kwa ajili ya kukusanya kura za maoni ya Wanachama ya kuanzisha Kampuni (NDIYO) au kutokuwa Kampuni (HAPANA)
Kila Mwanachama hai atakuwa na uhuru wa kupiga kura na atalazimika kuja na Kadi yake ambapo itamzuia kupiga kura mara mbili au zaidi.
Zoezi hili ni muhimu kwa ajili ya maendeleo ya YANGA.
“YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO”
LAWRENCE MWALUSAKO


HIVI NDIO VIINGILIO VYA MECHI YA YANGA NA SIMBA




Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumapili(Otoba 20 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.

Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni katika vituo mbalimbali.

Vituo hivyo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala, Uwanja wa Uhuru, na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.

Mechi hiyo namba 63 itachezeshwa na Israel Nkongo kutoka Dar es Salaam, ambapo atasaidiwa na Hamis Changwalu wa Dar es Salaam pia, na Ferdinand Chacha wa Bukoba. Mwamuzi wa akiba ni Oden Mbaga wa Dar es Salaam.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa John Kiteve kutoka Iringa wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Stanley Lugenge wa Njombe
Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumapili(Otoba 20 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.

Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni katika vituo mbalimbali.

Vituo hivyo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala, Uwanja wa Uhuru, na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.

Mechi hiyo namba 63 itachezeshwa na Israel Nkongo kutoka Dar es Salaam, ambapo atasaidiwa na Hamis Changwalu wa Dar es Salaam pia, na Ferdinand Chacha wa Bukoba. Mwamuzi wa akiba ni Oden Mbaga wa Dar es Salaam.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa John Kiteve kutoka Iringa wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Stanley Lugenge wa Njombe

PICHA: KANSIIME ANNE YULE MCHEKESHAJI WA UGANDA AMEOLEWA








Tuesday, October 15, 2013

HATIMAE DR NDALICHAKO AONDOKA NECTA

Uthibitisho huu umetoka kwa mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) Prof Rwekaza Mukandala kuwa Katibu Mtendaji wa NECTA Dr Joyce Ndalichako ameondoka NECTA na nafasi yake sasa inakaimiwa na Dr Charles Msonde aliyekuwa msaidizi wake.

Kwa mujibu wa Profesa Mukandala, ni kwamba Dr Ndalichako ameanza likizo ya utafiti (Sabbatical leave) ya mwaka mmoja kuanzia Oktoba mosi mwaka huu hadi Septemba 30 mwaka 2014 licha ya kuwepo kwa taarifa za kuwepo shinikizo la kisiasa lilikuwa likimzonga Dr Ndalichako kutakiwa kujiuzulu.Dr. Ndalichako


CHANZO: JAMII FORUM



MCHUNGAJI WA KANISA LA ANGLIKANA GONGO LA MBOTO AFUMANIWA GUEST NA MKE WA MTU

TOFAUTI na inavyoaminika na wengi kuwa watumishi wa Mungu ni watu safi, safari hii Mchungaji Obed Ntimba wa Kanisa la Anglikana Gongo la Mboto, Dar es Salaam amejikuta akivunja agano la Muumba baada ya kunaswa gesti akiwa na mke wa mtu.
  
 Tukio hilo la aibu lilimkuta mchungaji huyo Ijumaa iliyopita saa saba na nusu za mchana katika gesti moja (jina lipo) iliyopo nyuma ya Jengo la Ubungo Plaza jijini Dar.
  
Siku moja kabla ya tukio, makachero wetu walitonywa kuhusu dhambi hiyo na mtu wa karibu na watu hao akisema kuwa anaumia kwa sababu mchungaji huyo ana mke na watoto na mwanamke huyo, Rose ni mke wa mwanajeshi kwa hiyo aliamini tendo wanalotaka kulifanya ni uovu katika jamii.
  
 Mtoa habari wetu huyo alisema tukio hilo lilipangwa kukamilika kesho yake Ijumaa katika gesti hiyo ndipo kazi ya kuwafuatilia hatua moja baada ya nyingine ilianza.
  
Ijumaa saa sita mchana, mtonyaji wetu alipiga simu  na kuweka wazi kwamba wawili hao wapo njiani kuelekea gesti, kila mmoja kwa usafiri wake.
  
 Ndipo makachero wetu  walipowatonya polisi na kuambatana nao mpaka kwenye gesti hiyo na kujipanga kwa mbinu za kisasa za kutoonwa na ‘adui’.

 Makachero hao  walifanikiwa kupata ramani ya chumba walichoingia wawili hao ambapo ‘rumu’ namba 1B ndiyo iliwasilishwa kwamba Rose na mchungaji wake wamo humo.

Saa saba na nusu mchana, Makachero wetu na polisi waliingia hadi mapokezi ya gesti hiyo kwa kificho na kutoa maelekezo kwa mhudumu. Mhudumu aliongozana nao hadi mlangoni na kugonga lakini haukufunguliwa.
  
 BAADA YA DAKIKA TANO
Wakati mlango huo ukigongwa na mhudumu bila kufunguliwa, mchungaji huyo alisikika akisema na kuuliza:
“Subirini kwanza.”
“Lakini ninyi ni akina nani?”
  
 Baada ya dakika tano kupita, mlango ulifunguliwa, mchungaji akakutana na macho ya timu nzima. Alipigwa butwaa asijue la kufanya huku akitetemeka, Rose alikuwa ndani ya khanga moja!
  
 MCHUNGAJI MSOBEMSOBE HADI POLISI
Polisi waliwabeba msobemsobe wote hadi Kituo cha Polisi cha Urafiki-Ubungo, Dar ambapo kila mmoja alianza kujieleza.
  
 MCHUNGAJI APANGULIA HUDUMA YA KIROHO
Kituoni hapo, Mchungaji Ntimba alipobanwa kuhusu sababu za kuingia gesti na mke wa mtu, alisema waliingia kwa ajili ya huduma ya kiroho kwani mwanamke huyo alikuwa anataka kufungua kanisa ndipo alipomuomba yeye amsaidie.
  
 “Mimi sikuwa na lengo baya jamani. Huyu dada alihitaji kufungua kanisa, akaniambia ili nimshauri hawezi kukaa  sehemu ya wazi kwa kuwa mume wake ni mwanajeshi anaweza kuonekana na watu wakampa taarifa.
  
 “Ndipo nikaamua kwenda naye katika nyumba ile ya kulala wageni kwani wageni wengi wanaokuja kwa ajili ya huduma, wakitokea nchi mbalimbali huwa wanalala pale na wahusika wa pale wananifahamu sana.
  
 “Baada ya kuingia gesti nilibanwa na haja ndogo, nikaenda kujisaidia. Cha kushangaza niliporudi nilimkuta huyu dada amevua nguo zote na kuanza kunishawishi lakini sikuwa na lengo hilo jamani,” alijitetea mchungaji huyo.

 Baadhi ya picha zilizopo  zinamuonesha mchungaji huyo akiwa amevaa suruali lakini amesahau kufunga zipu huku kondom zikiwa pembeni kitandani!
  
 MSIKIE MKE WA MTU SASA
Baada ya mchungaji kutoa maelezo yake, mke wa mtu naye alianza kutiririka ya kwake huku akionesha ushahidi wa meseji za simu ambazo mchungaji huyo alikuwa akimtumia akimshawishi kumpa penzi.
  
 “Huyu mchungaji nilikwenda kwake kwa lengo la kufanya kazi kanisani lakini kuanzia hapo amekuwa akinishawishi kuwa anataka nimpe penzi ili aweze kuniweka katika sehemu nzuri kanisani.
  
 “Nilikuwa nakataa, lakini akasema tukutane pale gesti tuongee zaidi. Nilikataa kukutana gesti, akaniambia pale ni ofisini, mara nyingi akiwa anaongea na waumini mambo muhimu ya huduma ya kiroho huwa anakutana nao pale.

 “Nikakubali lakini kabla hata hatujaongea chochote alianza kuvua nguo zake na kuanza kunilazimisha tufanye mapenzi huku akiwa na ‘kinga’ kabisa na mimi nikavua nguo lakini kabla hajatimiza lengo lake ndipo wakaingia watu wakiwa na askari.
  
 “Mimi nashukuru sana kwa sababu hawa ndiyo wameniokoa. Nilikuwa nikisikia habari za huyu mchungaji kuwa ana tabia ya kuwafanyia wasichana wengi vitendo hivyo na kweli leo ndiyo nimeamini,” alieleza mwanamke huyo.
  
 Katibu wa kanisa hilo (jina halikupatikana mara moja) alimuombea msamaha mchungaji kwa waandishi huku akionesha kuumizwa na kitendo hicho baada ya kuoneshwa ushahidi na kukiri kwamba una ukweli tofauti na alivyokuwa akifikiria awali kabla ya kuachiwa kwa dhamana.


-Source: Global Publisher.


PICHA: SHEIKH KISHKI AKITOA MAWAIDHA YA SIKU YA IDD LEO

Sh. Nurdin Kishki akitoa khutba baada ya kuongoza Sala ya iddy.

Eneo: Dar es salaam (Mbagala - Zakhiem)




Waumini wakiwa wametulia wakisikiliza Mwaidha

Waumini wakichukua kumbukumbu ya tukio hili adhimu




MAWAIDHA YA SHEIKH BOMBO LEO KATIKA SIKU YA IDD

Picture
Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu wakiwa wamekusanyika katika viwanja vya Kiwanja Ngoma Sokomatola Jijini Mbeya kwa ajili ya Ibada ya swala ya Eid El Haj wakiungana na waislamu wengine duniani kuadhimisha ibada ya Hija inayokamilika leo Meccah, Saudi Arabia.
Kutoka kwenye blogu ya Mwanafasihi Mahiri, Mkwinda — Waumini wa dini ya Kiislamu mkoani Mbeya wameungana na Waislamu wenzao duniani katika kusherehekea ibada ya Eid na kutoa ujumbe wa kuzitaka nchi za Magharibi ziache uvamizi katika nchi za Kiislamu ambazo zina maslahi ya kiuchumi.

Akizungumza katika Ibada ya Swala ya Eid katika viwanja vya Kiwanja Ngoma, Sokomatola Jijini Mbeya, kiongozi wa Ibada hiyo ambaye ni Imamu katika msikiti wa Baraa Bin Azb Isanga, Shekhe Ibrahim Bombo alisema kuwa uvamizi unaofanywa na nchi za Magharibi umelenga kupora mali za wananchi wa nchi hizo.

Shekhe Bombo alisema kuwa limekuwa ni jambo la kawaida kwa nchi za Magharibi kudondoka mate kwa mali zilizopo katika
nchi za Kiislamu, hivyo njia pekee inayofanywa na nchi hizo ni kuzichonganisha ili machafuko yaibuke na wao kutumia fursa hiyo kuhujuma mali zilizopo katika nchi hizo.

Alisema kuwa ipo mifano mingi katika nchi zenye utajiri mkubwa duniani ambazo zimevamiwa na mali zake kuporwa na wageni kutoka nchi za Magharibi. Alizitaja nchi hizo kuwa ni pamoja na Libya, Afghanistan, Misri, Syria, Yemen, Iran na Pakistan ambako kumekuwa kukiibuka mapigano ya mara kwa mara huku wageni wakiingia katika nchi hizo wakijifanya wanasuluhisha migogoro ilhali wakiingilia utawala wa ndani na kujinufaisha kwa mali zilizomo: ''Tunalaani vitendo vya nchi za Magharibi kufanya uchonganishi kwa nchi zenye utajiri wa mafuta, itafika mahala dunia nzima haitakubali kwa dhuluma hii, tunaungana na wenzetu duniani kulaani dhuluma hii.''alisema Shekhe Bombo.

Shekhe Bombo alidai kuwa katika uvamizi huo yanafanyika mauaji ya kikatili kwa raia wasio na hatia ilhali akina mama na watoto wakidhalilishwa na kubakwa jambo ambalo halipaswi kuvumilika na kwamba itafika wakati Waislamu wote wataungana kupinga ukatili huo.

Aidha aliwataka waumini wa dini ya Kiislamu kutokubali kutenganishwa kwa imani zao moja na kwamba Waislamu wote wanaongozwa na Kitabu kimoja na Mtume mmoja na kwamba miongozo ya Uislamu inafuata taratibu za kitabu cha Koran na Hadith za Mtume Muhammad (SAW): ''Sisi sote ni Waislamu! inakuwaje  tukubali kutofautiana na wenzetu walioko Mecca Saudi Arabia ambao wanatekeleza ibada hii ya Hijja leo nasi tukiadhimisha kwa kufanya ibada ya Swala ya Eid el Haj?" alihoji Shekhe Bombo.

Wakati Waislamu wengine wameswali leo, kesho Waislamu wengine wanatarajia kuswali swala ya Eid kutokana na matangazo yatakayotolewa na viongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).



HUKUMU YA BABU SEYA KUFANYIWA MAPITIO UPYA NA MAJAJI WATATU

Jopo la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani nchini Tanzania waliotoa hukumu ya wanamuziki maarufu nchini, Nguza Viking “Babu Seya” na mwanaye Johnson Nguza “Papii Kocha”, linatarajia kupitia upya hukumu hapo Oktoba 30, mwaka huu, gazeti la HabariLeo limeandika.

Nguza Viking na wanaye watatu walihukumiwa na Hakimu Mkazi  Addy Lyamuya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kifungo
cha maisha jela mwaka 2004.

Baada ya hukumu hiyo, walikata rufaa mwezi Februari, mwaka 2010 katikaMahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam lakiniJaji Thomas Mihayo naye aliwatia hatiani na kuafiki hukumu ya Mahakama ya Kisutu.

Walikata tena rufaa katika Mahakama ya Rufani na safari hii, Jopo la majaji watatu -- Nathalia Kimaro, Mbarouk Mbarouk na Salum Massati -- liliwaachia huru Nguza Mbangu na Francis Nguza baada ya kubainika hawakuwa na hatia, na kuamuru Nguza Viking na Johnson Nguza watumikie kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto wadogo wa shule ya Msingi kama ilivyohukumiwa na mahakama zilizotangulia.


NGASSA KUCHOMA NYUMBA ZAKE TANO MOTO KAMA HATAIFUNGA SIMBA

MRISHO KHALFAN NGASSA

Saleh "Jembe" anamkariri mshambuliaji nyota wa Yanga, Mrisho Ngassa akisema kuwa hasira zake ni kama atashindwa kufunga au angalau kutoa pasi itakayozaa bao litakaloimaliza Simba: “Niko vizuri na ninajiona niko tayari kwa mchezaji, nataka kufanya kazi nzuri na ninajua Simba nitawafunga.  Kama nitashindwa kufunga basi nitatoa angalau pasi ya bao litakalosababisha Simba wafungwe. La sivyo nitachoma nyumba zangu tano ninazomiliki,” alisema Ngassa kwa kujiamini.

Yanga na Simba zinakutana Jumapili katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.



PICHA: RAIS AKUTANA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA LEO

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Viongozi wa Vyama vya Siasa nchini, waliofika ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Vyama vya Upinzani muda mfupi kabla ya kuanza mazungumzo kuhusu Rasimu ya Katiba ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha kutoka kushoto ni Isaack Cheyo UDP, James Mbatia NCCR Mageuzi, Professa Ibrahim Lipumba CUF, Freeman Mbowe CHADEMA, Philip Mangula CCM na Bibi Nancy Mrikaria aliyemwakilisha Mwenyekiti wa TLP Mhe. Agustine Lyatonga Mrema.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha ikulu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Mh. Freeman Mbowe mara baada ya mazungumzo nao leo ikulu jijini Dar es Salaam. Nyuma kushoto ni Kiongozi wa NCCR Mageuzi, Mh. James Mbatia na Professa Ibrahim Lipumba wa CUF.
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mhe. Tundu Lissu wa CHADEMA. Nyuma ni Mhe. James Mbatia NCCR Mageuzi.
 
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mhe. John Mnyika.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Vyama vya Upinzani na wasaidizi wao waandamizi muda mfupi kabla ya kuanza mazungumzo kuhusu Rasimu ya Katiba ikulu jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto mbele ni Isaack Cheyo UDP, James Mbatia NCCR Mageuzi, Professa Ibrahim Lipumba CUF, Freeman Mbowe CHADEMA, Philip Mangula CCM na Bibi Nancy Mrikaria aliyemwakilisha Mwenyekiti wa TLP Mhe. Agustine Lyatonga Mrema. Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu CUF Bwana Julius Mtatiro, Mhe. Tundu Lissu CHADEMA, Bwana Martin Mng’ong’o NCCR Mageuzi, Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge William Lukuvi, Mhe. Habib Mnyaa CUF, Mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. John Mnyika, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Mhe. Steven Wassira na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mathias Chikawe.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU