Facebook Comments Box

Tuesday, October 15, 2013

HATIMAE DR NDALICHAKO AONDOKA NECTA

Uthibitisho huu umetoka kwa mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) Prof Rwekaza Mukandala kuwa Katibu Mtendaji wa NECTA Dr Joyce Ndalichako ameondoka NECTA na nafasi yake sasa inakaimiwa na Dr Charles Msonde aliyekuwa msaidizi wake.

Kwa mujibu wa Profesa Mukandala, ni kwamba Dr Ndalichako ameanza likizo ya utafiti (Sabbatical leave) ya mwaka mmoja kuanzia Oktoba mosi mwaka huu hadi Septemba 30 mwaka 2014 licha ya kuwepo kwa taarifa za kuwepo shinikizo la kisiasa lilikuwa likimzonga Dr Ndalichako kutakiwa kujiuzulu.Dr. Ndalichako


CHANZO: JAMII FORUM



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU