Facebook Comments Box

Tuesday, October 15, 2013

NGASSA KUCHOMA NYUMBA ZAKE TANO MOTO KAMA HATAIFUNGA SIMBA

MRISHO KHALFAN NGASSA

Saleh "Jembe" anamkariri mshambuliaji nyota wa Yanga, Mrisho Ngassa akisema kuwa hasira zake ni kama atashindwa kufunga au angalau kutoa pasi itakayozaa bao litakaloimaliza Simba: “Niko vizuri na ninajiona niko tayari kwa mchezaji, nataka kufanya kazi nzuri na ninajua Simba nitawafunga.  Kama nitashindwa kufunga basi nitatoa angalau pasi ya bao litakalosababisha Simba wafungwe. La sivyo nitachoma nyumba zangu tano ninazomiliki,” alisema Ngassa kwa kujiamini.

Yanga na Simba zinakutana Jumapili katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU