Facebook Comments Box

Saturday, December 21, 2013

ZITTO KABWE APOKELEWA KAMA RAISI MKOANI KIGOMA ALIPO WASILI LEO ASUBUHI TAZAMA PICHA






Zitto Kabwe akiwa katika gari la wazi mara baada ya kutua kigoma asubui ya leo ambapo amepata mapokezi ya kishindo.
 



KIBONZO: KIPANYA NA WATAFUNA NCHI



HEBU JIONEE JINSI WANAOBEBA MADAWA YA KULEVYA WANAVYO PASULIWA ILI KUYATOA

Dawa za Kulevya hazifai hakuna asiyefahamu jambo hili lakini unakuta baadhi ya watu wanayaweka maisha yao rehani na kukubali kuwa 'Punda' na kubeba mizigo hii haifai waache mara moja wote wenye tabia hii ni hatari kwa maisha yao.



Picha ya X-ray inavyoonesha tumboni madawa yaliovyo kwa mtu aliyebeba.

Athari inayoweza kupatikana yakiwa mwilini kama unavyoweza kujionea hapo juu.


Operesheni ikifanyika tayari kuyaondoa madawa hayo yaliyo sababisha kijana huyu kufariki.


Utumbo umetolewa tayari ili kuanza kuyatoa madawa hayo.


Kama uonavyo weza kujionea dawa hizo zikiwa ndani ya utumbo mpana.
Dawa zikianza kutolewa pamoja na kushafishwa kama unavyoona katika picha.




Kabla mtu hajazimeza zinakuwa hivi, sasa hebu fikiria mtu anameza kete hadi 5000 hii ni balaa kubwa sana.



Friday, December 20, 2013

RAIS ATENGUA UTEUZI WA MAWAZIRI WANNE WALIOTAKIWA KUJIUZURU NA WABUNGE

 Waziri wa Maliasili na Utalii - Mh. Khamis Kagasheki
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa - Mh. Shamsi Vuai Nahodha
 Waziri wa Mambo ya Ndani - Dk. Emanuel Nchimbi
Waziri Mkuu - Mh. Peter Pinda

Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi  Kagasheki amejiuzulu wadhifa wake baada ya mjadala mkali wa Bungeni mjini Dodoma hapo jana Tarehe 20 Desemba siku ya Ijumaa.

Hii inatokana na Operesheni Tokomeza iliyolenga kuondoa ujangili uliokithiri nchini.
 

Tangu kuanza kwa operesheni hiyo, kumekuwa na malalamiko mbalimbali kutoka kwa wabunge, wanaharakati na wananchi dhidi ya askari waliokuwa wakiiendesha yakiwamo ya watu kujeruhiwa,kubakwa,kuchomewa nyumba, mifugo kuuawa, kupigwa na uporaji.


Operesheni hiyo ilikuwa ikiendeshwa kwa pamoja na askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Polisi, Usalama wa Taifa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa).

Operesheni hiyo ilizuiwa baada ya suala hilo kutinga bungeni na watunga sheria hao kuweka kando tofauti zao za kiitikadi na kuungana wakitaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki na Waziri wa Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi, Mathayo David Mathayo wawajibike.

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi , Dk David Mathayo David, akitoa utetezi wake, akidai kuwa ameonewa na kamwe hawezi kujiuzuru.
 

Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda ametaka uthibitisho usio na shaka kwa waliohusika wote na taasisi zao kuchunguzwa kiundani ili hatua stahiki zichukuliwe. Kuendelea kulinda rasilimali na hifadhi za Taifa amekutaja kuwa ni  muhimu. Pia amesema ameongea na Waziri mmoja mmoja kuwa ni busara ushauri wa wabunge utekelezwe. Amebainisha kuwa hata baada ya kuongea na Rais, Mkuu wa nchi huyo ameridhia tume iundwe na kila aliyehusika awajibike.

Amesema Rais ameshauri kutengua uteuzi wa mawaziri wote wanne ( Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Shamsi Vuai Nahodha, Wazir wa Mambo ya Ndani Dkt Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt David Mathayo, na Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi Kagasheki) kama ambavyo wabunge walivyopendekeza.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe  James Lembeli alisema kuwa kamati yake imeridhishwa na matokeo ya ripoti ya kamati iliyosababisha hayo yote, na kwamba maelezo ya taarifa ya kamati kimsingi yote yamekubalika. 


Kuhusu kumhusisha Dkt Mathayo ni kuwa  Rais alishatoa maagizo tisa miongoni likiwepo swala la kushughulikia wafugaji wanaohamahama. Amesema pia Rais aliagiza pia kuwa wafugai wawe wa kisasa, pia kutafuta missing link ya mifugo isipotee na pia kutafuta masoko nje ya nchi, ambapo amesema mengi hayajatekelezwa.


Ameweka bayana kuwa chimbuko kubwa ni Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, na kwamba Waziri hakuwa anapewa taarifa za mara kwa mara.

 
Ameomba kipengele kiongezwe kuwa Katibu mkuu na watendaji wake wakuu  waliohusika kuandaa Mpango kazi wa 'Operesheni Tokomeza' wawajibishwe.


Amesema rushwa iliyoko ndani ya wizara ya Maliasili na Utalii inatisha. Spika amuomba Mwanasheria mkuu kutumia kifungu kuongeza muda. Naye ameomba  kuundwa tume ya kisheria ya mahakama.




KIBONZO: HAMU YA KUSOMA



UWANJA WA AMANI ZANZIBAR WAREKEBISHWA NA KUWEKWA NYASI BANDIA

Na Camera ya Kitongoni Mjini Unguja:
Uwanja wa Amani wa Zanzibar maarufu kama Amani Stadium umefanyiwa marekebisho na kuwekewa nyasi bandia.

Baada ya kukamilika ulifanyiwa majaribio kwa mechi ya vijana wa  chini ya miaka 20.

Hii ni katika maandalizi ya sherehe za mapinduzi. Uwanja huo umekuwa wa kisasa zaidi kwa wakati huu kama unavyoweza kujionea mwenyewe kwenye picha mbalimbali hapo juu.


PICHA: OMARY MAKAME ALIE TUHUMIWA KUMUUA PADRI ZANZIBAR AACHIWA

Picha Omary Makame akiwa anatoka nje ya mahakama baada ya kupewa dhamana. Omary alikuwa anashitakiwa kwa kosa la kumuua kwa risasi padri Zanzibar



FIFA CLEARED OKWI MOVE TO TANZANIAN CLUB

The Acting Competitions Director of the Uganda FA, Decolas Kiiza, has clarified that FIFA cleared striker Emmanuel Okwi to join Tanzanian league champs Young Africans FC.
“Yes we wrote to FIFA and they said the player was free to transfer,” Kiiza told MTNFootball.com.
Early this week the FA’s Chief Executive Officer, Edgar Watson, said they had contacted FIFA to get more clarification on the issue.
Young Africans signed Okwi early this week on a two-year deal and yet FIFA had provisionally released the player to join local side SC Villa from Tunisia’s Etoile du Sahel.
But Okwi’s former team, Simba SC in Tanzania, is also unhappy that the Tunisian giants did not pay the full transfer package when Okwi moved early this year.
Okwi is expected to fly out to Dar es Salaam on Friday to complete the contract details with Young Africans and also feature against former side Simba SC in a special encounter on Saturday.
Allan Papaok, a director in the company that has rights over the player, said today that they have not finalised the deal for Okwi’s move.
“We might fly there this weekend to conclude the deal,” he added.
However, many football administrators in Uganda are wondering how FIFA could clear Okwi to transfer to Young Africans, yet he was released on a provisional basis to join SC Villa from Etoile du Sahel, who he claimed were not meeting contractual obligations.


Thursday, December 19, 2013

OKWI KUTUA LEO SAA 9:30

Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Uganda Emmanuel Okwi anatarajiwa kutua leo mchana majira ya saa 9:30 katika uwanja wa ndege wa Mwalimu JK Nyererer akitokea nchini Uganda kwa shirika la ndege la Rwanda.

Hii ni taarifa rasmi kwa wapenzi wa soka, wanacham na mashabiki kuwa rasmi mchezaji huyo atawasili leo na kupokelewa na viongozi wa klabu ya Yanga pamoja na mashabiki na wanachama kwa ujumla.

Ujio wa Emmanuel Okwi leo unafuatia kukamilisha masuala yake yaliyokuwa yamembakisha nchini Uganda na moja kwa moja leo ataungana na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa jumamosi dhidi ya Simba SC katika Nani Mtani Jembe.



YANGA KULIPWA MILIONI MOJA KILA DAKIKA KATIKA MECHI ZAO

Katibu mkuu wa Yanga Beno Njovu akiongea na waandishi wa habari kuhusu mkataba mpya wa Yanga wa kurusha mechi zake. kushoto ni bwana Goitha muwakilishi wa Tv itakayorusha mechi za Yanga za kimataifa
Klabu ya Young Africans SC imeingia mkataba wa kurusha mchezo wake wa hatua ya kwanza ya mashindano ya klabu Bingwa Afrika dhidi ya timu ya Alh Ahly ya Misri kwa gharama ya dola za kimarekani elfu 55,000 sawa na mil 90/= za kitanzania kwa muda wa dakika 90.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Young Africans Katibu Mkuu  Bw. Beno Njovu amesema wameingia mkataba huo na kampuni ya SGM kutoka nchini Ufarans na moja kwa moja wameipa uwakala kampuni ya MGB ya Zamaleki ya Cairo.
Mkataba huo unawapa kibali kampuni ya SGM kurusha moja moja mchezo mchezo wa Yanga dhidi ya Al Ahly utakaofanyika Tanzania nchini Misri, nchi za Afrika Kaskazini na Mashariki ya Mbali huku pia vituo vya telesion vya ndani ya nchi vikipewa fursa ya kuonyesha ndani ya nchi.
SGM imefikia hatua hiyo kufuatia kuona ratiba ya Klabu Bingwa Afrika iliyotoka mwanzoni mwa wiki kuonyesha kuwa timu ya Young Africans itaanza na timu ya Komoronize katika hatua ya awali na kisha kukutana na Al Ahly katika hatua ya 32 bora.
Mwakilishi wa SGM Bw. Francis Gaitho amesema wao wameamua kuingia makubaliano hayo na Yanga mapema wakiwa na uhakika kuwa timu ya Yanga itasonga mbele katika hatua ya awali na hivyo watakutana na mabingwa watetezi Al Ahly.
Yanga itaanza kucheza na timu ya Komoronize ya Visiwa vya Comoro Februari 8 mwakani uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kabla ya kurudiana nao wiki baadae nchini kwao Comoro na kikifanikiwa kuvuka hatua hiyo ndo itakutana na Al Ahly Februari 28, 02, 02 Machi na kurudiana baada ya wiki moja nchini Misri.


Wednesday, December 18, 2013

KIVUKO CHA MV MAGOGONI KINAELEA BAADA YA INJINI KUZIMA

Kivuko cha Mv Magogoni kinaelea juu ya maji kwa wakati huu baada ya injini yake kuzima.
Kivuko hicho kimebeba watu wengi na magari mpaka mwanzoni kama kawaida yake.
Abiria wamevaa maboya ila sio wote ambao wamepata maboya.
Juhudi zinafanyika kuwaokoa kuna mitumbwi ambayo imekuwa ikifika hapo na kuwachukua baadhi ya abiria.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU