Thursday, October 24, 2013
UHABA WA MBAO KUPATIKANA BAADA YA MSITU UNAOTEGEMEWA WA SAO HILL KUTEKETEA KWA MOTO
YANGA WAFANYA YAO : SIMBA WAENDELEA KUFURAHIA SARE ZAO
![]() |
| Haruna Shamte na Joseph Owino wakijadili jambo baada ya sare na wagosi wa kaya |
Mabao ya Yanga yamefungwa na Hamis Kiiza aliyefunga mawili katika dakika ya 12 na 81 wakati lingine likifungwa na Frank Domayo mnamo dakika ya 72.
Wakati Yanga wakitoka vifua mbele leo, watani wao Simba SC wao wameshikwa sharubu baada ya kulazimishwa sare ya 0 - 0 na Coastal Union ya mkoani Tanga. Mechi hiyo imepigwa katika Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
DINI YA AJABU YAANZISHWA MBEYA
Dini inayoamini katika MUNGU lakini ikiruhusu yale ambayo dini zingine zinapinga imeanzishwa eneo la mji mdogo wa Makongolosi wilayani Chunya mkoani Mbeya,
Dini hiyo haiamini katika kutoa sadaka bali inasema tunamtolea nani sadaka wakati Vitu vyote tulivyonavyo ni mali ya MUNGU,kwa nini tunampa MUNGU mali zake Mwnyewe.!
Dini hiyo inaruhusu ulevi,uchawi na uzinzi kwa sababu vimeumbwa na MUNGU,Vile vile inaamini hakuna dhambi duniani,Dini hiyo inaitwa DIMAYO, sasa imeanza kuenezwa Mbeya
Tuesday, October 22, 2013
IKIJIANDAA KUCHEZA NA RHINO RANGERS KESHO KOCHA WA YANGA AWAOMBEA MSAMAHA WACHEZAJI
Young Africans kesho itashuka dimba la uwanja wa Taifa kucheza na maafande wa jeshi la ulinzi wa wananchi nchini (JWTZ) Rhino Rangers kutoka mkoani Tabora ikiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara mzunguko wa 10.
Monday, October 21, 2013
SHABIKI WA SIMBA AFARIKI DUNIA
MECHI YA YANGA NA SIMBA YAINGIZA MILIONI 500
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ya watani wa jadi Simba na Yanga
iliyochezwa jana (Oktoba 20 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam na kumalizika kwa sare ya mabao 3-3 imeingiza sh. 500,727,000.
Washabiki 57,422 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 63
kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000
na sh. 30,000.
Ni tiketi 131 tu ndizo hazikuuzwa ambazo ni 90 za VIP A, 40 za VIP B na
moja ya VIP C. Tiketi zilizochapwa kwa ajili ya mechi hiyo ni 57,558 ambayo
ndiyo idadi ya viti vilivyopo kwenye uwanja huo.
Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,025,564.32 wakati Kodi ya Ongezeko la
Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,382,084.75.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 62,555,371.69,
tiketi sh. 7,309,104, gharama za mechi sh. 37,533,223.01, Kamati ya Ligi
sh. 37,533,223.01, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
18,766,611.51 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh.
14,596,253.39.
UFOO SARO AFUNGUKA KUHUSU TUKIO LA KUPIGWA SHABA NA JINSI ALIVYO JIOKOA
Anasema dada yule alimpa khanga akajifunga na aliposogea barabarani alikutana na gari lililokuwa likiendeshwa na mwanamke mmoja.
“Nilipoona kuna gari linapita nikainuka kuomba msaada. Liliposimama nilimuona mwanamke akiendesha nikamweleza kwamba nilikuwa nimepigwa risasi na nilikuwa nikiomba msaada wake anikimbize hadi katika hospitali ya Tumbi na kwamba akifika pale tu aniache mlangoni.
“Si rahisi kuamini, yule mama alikataa kunisaidia akisema alikuwa akiwahi sehemu kumchukua mzazi. Sina la kusema niliamua kumsamehe tu yule mama ingawa niliumia sana,” alisema Ufoo.
Alisema muda mfupi tu baadaye alitokea kijana aliyekuwa na pikipiki, maarufu kwa jina la bodaboda ambaye alimuomba msaada wa kumkimbiza hospitali ya Tumbi na akakubali.
“Yule kijana aliniuliza iwapo nilikuwa ninao uwezo wa kujishikilia vizuri na niliposema nitaweza akanisaidia kupanda katika bodaboda.
“Wakati huo nilikuwa naona kama tumbo linazidi kujaa. Nikiwa kwenye pikipiki kuna wakati nilikuwa nikihisi kwamba naweza nikaishiwa nguvu na kuanguka katika barabara na kisha kupitiwa na gari na kupoteza maisha. Lakini nilipata ujasiri na kujishikilia,” alieleza kwa sauti ya chini.



