Facebook Comments Box

Thursday, October 24, 2013

UHABA WA MBAO KUPATIKANA BAADA YA MSITU UNAOTEGEMEWA WA SAO HILL KUTEKETEA KWA MOTO


 Msafara  wa rais Jakaya  Kikwete ukiwa  umesimama kwa muda eneo la  msitu wa  taifa  wa Sao Hill Mufindi  katika barabara kuu ya Iringa- Mbeya  kufuatia  moto mkubwa kuwaka katika msitu huo.
 Askari polisi akimamisha  msafara  wa rais Kikwete kutokana na moto  mkubwa  kutanda  eneo hilo la Changalawe katika  msitu wa Taifa  wa Sao Hill umbali wa mita  mbili kuelekea  barabara  ya Ikulu ndogo mjini Mafinga
 Askari  wa FFU  wakishuka katika gari lao kwenda  kuangalia  usalama  wa rais Kikwete na  kulia gari la kwanza ni naibu waziri wa ujenzi gari la pili na la tatu ni magari ya Ikulu yakiwa  yamesimama
 hapa  askari  wakishuka  kuingia katika moshi mzito  kuangalia  usalama  wa rais katika eneo hilo ambalo moshi mzito  ulitanda barabarani


 Msafara  ukipita  eneo hilo salama huku kulia ni askari wa JKT mafinga wakizima moto  huo


Yakiwa ni masaa takribani mawili  kupita  kutoka Rais Jakaya  Kikwete kufanya  kikao chake  cha majumuisho   ya ziara  yake   na  viongozi wa mkoa wa Njombe na  kuwataka  kuchukua hatua  katika kuthibiti moto  ili  kuepusha ukame ,moto  mkubwa umezuka katika msitu wa Taifa  wa Sao Hill Mufindi na kupelekea  msafara  wa  Rais kusimama kwa  muda  kiusalama kutoka na moshi mzito  uliotanda  barabara  kuu ya Iringa Mbeya .

Moto  ulio ulioanza  kuwaka  mida ya saa nane  mchana    ulizuia kwa  muda  kama dakika tatu hivi msafara  wa Rais Kikwete  kufimama katika eneo la Changalawe mjini  Mafinga umbali  wa mita 2  kufika  njiapanda  ya   kuingia ofisi ya mkuu  wa wilaya ya  Mufindi na Ikulu ndogo  ya  wilaya ya Mufindi.

Kutokana na tukio hilo la moto msafara  wa rais  Kikwete  ulisimama na baada ya maofisa  usalama  kushuka na kutazama usalama  zaidi wa msafara  huo ndipo  walioruhusu msafara  huo  kuendelea .

Hata  hivyo  jitihada  kubwa  zilionekana kufanywa na  kikosi  cha askari  wa  JKT Mafinga  pamoja na  wananchi ambao  walikuwa  wakizima  moto  huo .

Huku   vyombo  vya  usafiri  yakiwemo mabasi ya abiria yanayosafiri  kutoka Dar es Salaam kuwenda  mikoa ya  kusini na nchi  za kusini mwa Tanzania yakikwama  kuendelea na  safari  kutoka na moto  huo kushikakasi na  moshi  mzito  kutanda  barabara 

Mkuu  wa  mkoa  wa  Iringa Dr  Christine Ishengoma  alisema kuwa  uongozi  wa  mkoa  tayari  umeagiza  mkuu wa wilaya ya Mufindi kuwasaka   waliohusika na  uchomaji  moto huo ili  kuchukulia  hatua  kali.


Mkuu  huyo  wa  mkoa alisema  kuwa mkoa  wa Iringa umekuwa  ukichukua hatua  kali  kwa wale wote wanaoanzisha  moto  kichaa kama  huo hivyo  kupitia  ofisi ya mkuu wa wilaya ya Mufindi wahusika  watasakwa  popote  walipo .

Mbali na  hilo mkuu  huyo amelipongeza  jeshi la JTK Mafinga kwa  kuchukua hatua  za haraka katika kukabiliana na moto  huo huku akisema madhara  zaidi  yatokanayo na moto  huo yatatolewa baada ya  moto  huo kuthibitiwa Chanzo: Francis Godwin-Iringa


YANGA WAFANYA YAO : SIMBA WAENDELEA KUFURAHIA SARE ZAO

Haruna Shamte na Joseph Owino wakijadili jambo baada ya sare na wagosi wa kaya
Yanga SC leo imeweka kimbindoni pointi tatu baada ya kuichabanga mabao 3 - 0 timu ya Rhino Rangers kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Hamis Kiiza aliyefunga mawili katika dakika ya 12 na 81 wakati lingine likifungwa na Frank Domayo mnamo dakika ya 72.
Wakati Yanga wakitoka vifua mbele leo, watani wao Simba SC wao wameshikwa sharubu baada ya kulazimishwa sare ya 0 - 0 na Coastal Union ya mkoani Tanga. Mechi hiyo imepigwa katika Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.


DINI YA AJABU YAANZISHWA MBEYA

Dini inayoamini katika MUNGU lakini ikiruhusu yale ambayo dini zingine zinapinga imeanzishwa eneo la mji mdogo wa Makongolosi wilayani Chunya mkoani Mbeya,

Dini hiyo haiamini katika kutoa sadaka bali inasema tunamtolea nani sadaka wakati Vitu vyote tulivyonavyo ni mali ya MUNGU,kwa nini tunampa MUNGU mali zake Mwnyewe.!

Dini hiyo inaruhusu ulevi,uchawi na uzinzi kwa sababu vimeumbwa na MUNGU,Vile vile inaamini hakuna dhambi duniani,Dini hiyo inaitwa DIMAYO, sasa imeanza kuenezwa Mbeya



Tuesday, October 22, 2013

IKIJIANDAA KUCHEZA NA RHINO RANGERS KESHO KOCHA WA YANGA AWAOMBEA MSAMAHA WACHEZAJI


Young Africans kesho itashuka dimba la uwanja wa Taifa kucheza na maafande wa jeshi la ulinzi wa wananchi nchini (JWTZ) Rhino Rangers kutoka mkoani Tabora ikiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara mzunguko wa 10.

Mchezo huo ambao utachezwa kuanzia majira ya saa 10 jioni kwa saa za Afrika mashariki, ni muhimu kwa timu ya Young Africans kupata pointi 3 ili iweze kujiweka katika mazuri ya kutetea Ubingwa wake.

Akiongea mara baada ya mazoezi ya leo kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts amesema matokeo ya juzi yamemsikitisha yeye, benchi la ufundi, wachezaji, viongozi pamoja na wanachama lakini haikuwa dhamira yao kupoteza pointi 3 muhimu.

Tulikuwa tunaongoza 3-0 mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika, lakini kipindi cha pili wachezaji wangu walizembea sana, hawakucheza kwa umakini wala kusikiliza maaelekezo yangu hali iliyopelekea wapinzani wetu kuweza kusawazisha mabao yote 3.

"Tunawaomba sahamani sana wapenzi, washabiki na wanachama wa Young Africans kwa ujumla kwa matokeo ya juzi, tulistahili kushinda lakini kutokua makini kwa wachezaji wetu ndio kulipelekea matokeo hayo kubadilika, kikubwa kwa sasa nimeongea na wachezaji na wameahidi kutorudia makosa katika michezo inayofuata" alisema Brandts. 

Washabiki, wapenzi na wanachama wa Young Africans mnaombwa kesho kujitokeza kwa wingi kuja kuwapa nguvu vijana katika mchezo dhidi ya Rhino Rangers ambapo Yanga ikishinda itafikisha pointi 19 na kwa na tofauti ya pointi 1 tu na wanaongoza Ligi Kuu kwa sasa.


Monday, October 21, 2013

SHABIKI WA SIMBA AFARIKI DUNIA

Habari ambazo bado hatujapata uhakika nazo vizuri, zinasema shabiki mmoja wa Simba ambae alizimia wakati Simba ikiwa nyuma kwa bao 3, amefariki, anjulikana kwa jina la Luhanga, mkazi wa Mburahati, Dar Es Salaam, inasemekana atazikwa leo huko huko mburahati.
Katika mchezo huo, mashabiki wa pande mbili walizimia na kupatiwa huduma ya kwanza.
Tutawaletea habari zaidi tukipata uhakika wa mkasa huo.
Simba na Yanga zilitoka sare ya 3-3, mabao ya simba yakifungwa kipindi cha pili.


MECHI YA YANGA NA SIMBA YAINGIZA MILIONI 500

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ya watani wa jadi Simba na Yanga
iliyochezwa jana (Oktoba 20 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam na kumalizika kwa sare ya mabao 3-3 imeingiza sh. 500,727,000.

Washabiki 57,422 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 63
kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000
na sh. 30,000.

Ni tiketi 131 tu ndizo hazikuuzwa ambazo ni 90 za VIP A, 40 za VIP B na
moja ya VIP C. Tiketi zilizochapwa kwa ajili ya mechi hiyo ni 57,558 ambayo
ndiyo idadi ya viti vilivyopo kwenye uwanja huo.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,025,564.32 wakati Kodi ya Ongezeko la
Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,382,084.75.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 62,555,371.69,
tiketi sh. 7,309,104, gharama za mechi sh. 37,533,223.01, Kamati ya Ligi
sh. 37,533,223.01, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
18,766,611.51 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh.
14,596,253.39.



UFOO SARO AFUNGUKA KUHUSU TUKIO LA KUPIGWA SHABA NA JINSI ALIVYO JIOKOA


“Nyumbani kwetu, pale Kibamba si mbali sana na barabarani, wakati nikikaribia kufika barabarani wakati huo nikitokwa na damu nyingi huku nikihisi tumbo langu limejaa sana nilikutana na dada mmoja ambaye nilimuomba khanga ili nijifunge kuzuia damu zisitoke kwa wingi”.

Anasema dada yule alimpa khanga akajifunga na aliposogea barabarani alikutana na gari lililokuwa likiendeshwa na mwanamke mmoja.

“Nilipoona kuna gari linapita nikainuka kuomba msaada. Liliposimama nilimuona mwanamke akiendesha nikamweleza kwamba nilikuwa nimepigwa risasi na nilikuwa nikiomba msaada wake anikimbize hadi katika hospitali ya Tumbi na kwamba akifika pale tu aniache mlangoni.

“Si rahisi kuamini, yule mama alikataa kunisaidia akisema alikuwa akiwahi sehemu kumchukua mzazi. Sina la kusema niliamua kumsamehe tu yule mama ingawa niliumia sana,” alisema Ufoo.

Alisema muda mfupi tu baadaye alitokea kijana aliyekuwa na pikipiki, maarufu kwa jina la bodaboda ambaye alimuomba msaada wa kumkimbiza hospitali ya Tumbi na akakubali.

“Yule kijana aliniuliza iwapo nilikuwa ninao uwezo wa kujishikilia vizuri na niliposema nitaweza akanisaidia kupanda katika bodaboda.

“Wakati huo nilikuwa naona kama tumbo linazidi kujaa. Nikiwa kwenye pikipiki kuna wakati nilikuwa nikihisi kwamba naweza nikaishiwa nguvu na kuanguka katika barabara na kisha kupitiwa na gari na kupoteza maisha. Lakini nilipata ujasiri na kujishikilia,” alieleza kwa sauti ya chini.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU