Facebook Comments Box

Thursday, October 24, 2013

YANGA WAFANYA YAO : SIMBA WAENDELEA KUFURAHIA SARE ZAO

Haruna Shamte na Joseph Owino wakijadili jambo baada ya sare na wagosi wa kaya
Yanga SC leo imeweka kimbindoni pointi tatu baada ya kuichabanga mabao 3 - 0 timu ya Rhino Rangers kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Hamis Kiiza aliyefunga mawili katika dakika ya 12 na 81 wakati lingine likifungwa na Frank Domayo mnamo dakika ya 72.
Wakati Yanga wakitoka vifua mbele leo, watani wao Simba SC wao wameshikwa sharubu baada ya kulazimishwa sare ya 0 - 0 na Coastal Union ya mkoani Tanga. Mechi hiyo imepigwa katika Uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU