Facebook Comments Box

Sunday, November 23, 2014

TAMKO LA HIZB UT-TAHRIR JUU YA YANAYOTOKEA KENYA

Kwa mara nyengine tena Waislamu nchini Kenya   wameshuhudia uvamizi wa polisi wa misikiti miinne Sakina Musa, Swafaa na Minaa Mjini Mombasa.

Kitendo hiki cha kinyama kilichopelekea
mauaji ya mwanafunzi mmoja huku vijana wapato mia mbili na hamsini kutiwa mbaroni, kilifanywa chini ya kisingizio cha kuwafurusha vijana wenye misimamo mikali. Harakati ya Hizb
ut-Tahrir Afrika Mashariki inalaani vikali kitendo hiki na twasema yafuatayo:-

Ukatili wa polisi wa Kenya umezidi sana hasa kwa Waislamu ; Huku kukiwa kuna magenge ya-nayotekeleza mauaji kama vile Baghdad boys na Mungiki ambayo wengi ya wafuasi wake ni wakristo hatujashuhudia hata kanisa moja likivamiwa na polisi kama inavyofanywa kwa Waislamu. Bali polisi katika kuendeleza maonevu kwa Waislamu, huwapachika majina radicalists na
extremists kuhalalisha unyama wao dhidi yao. Na hii ndio sura kamili ya polisi leo ndani ya nidhamu za kibepari namna
wanavyotumiwa katika kuwafanyia unyama Waislamu. Madai ya kuwa kuna Waislamu wabaya na Waislamu wazuri
‘radicalists and moderates ni njama tu kuwagawanya Waislamu.

Na hata kama kuna tofauti baina ya Waislamu kifikra na kimisimamo,basi waachiwe wenyewe Waislamu kwani Uislamu uliwawekea utaratibu maalum wa kutatua kasoro hizo. Hivyo haijakuwa halali kwa serikali kuendeleza mateso kwa Waislamu kwa kisingizio hicho. Tunakataa miito hii pamoja na vita
kupambana na ugaidi kwani vyote hivyo ni kuushambulia Uislamu na Waislamu.

Udhalilifu huu umetokamana kukosekanwa na waakilishi wa kikweli  wa mambo ya Waislamu. Hata wale baadhi ya wanasiasa wanaojitokeza ati kukashifu unyamu huo, wao hufanya hivyo kwa lengo tu la kujitafutia umaarufu wa kisiasa. Ushahidi wa haya ni kuwa hao hao ndio huwadaa raia kuwa kushiriki kwao ndani ya nidhamu za kidemokrasia ndio njia ya kuzuia dhulma juu ya Waislamu. Na ukweli ni kuwa nidhamu za kidemokrasia ndio chanzo cha balaa zote zinazoshuhudiwa na watu wote Waislamu na wasokuwa waislamu.

Madhila haya leo ni sehemu tu ya miongoni mwa mengi yanayofanyiwa Waislamu kote dunia  na hayatokoma leo hadi pale Waislamu watapoweza kufanya kazi ya kubeba ulinganizi wa Kiislamu kwa lengo la kusimamisha utawala halisi wa Kiislamu Khilafah katika moja wapo ya nchi za Kiislamu.  Utawala huo ndio
utakaohifadhi kikweli Waislamu na Wasokuwa Waislamu na kuwakinga dhidi ya shari za maadui zao.

KUMB: 04 / 1436 AH   
25th Muharram 1436 AH
18/11/2014 CE
Shabani Mwalimu
Mwakilishi kwa Vyombo Vya Habari Hizb ut-Tahrir Afrika
Mashariki



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU