Wednesday, July 24, 2013
GONZALO HIGUAIN NA PEPE REINA WANAFANYA VIPIMO VYA AFYA NAPOLI SASA HIVI

Inaonekana Arsenal imepoteza nafasi ya kumsajili mshambuliaji wa kiargentina Gonzalo Higuain ambaye imemuwania kwa muda mrefu baada ya mshambuliaji kukaribia kujiunga na klabu ya Napoli ya Italia.
Kwa mujibu wa mtandao wa Sky News ni kwamba hivi sasa nchini Italia mshambuliaji Gonzalo Higuain na kipa wa Liverpool Pepe Reina ambaye nae alihusishwa na Arsenal huko nyuma wapo kwenye vipimo vya afya vya kujiunga na klabu ya Napoli.
Kwa mujibu wa mtandao wa Sky News ni kwamba hivi sasa nchini Italia mshambuliaji Gonzalo Higuain na kipa wa Liverpool Pepe Reina ambaye nae alihusishwa na Arsenal huko nyuma wapo kwenye vipimo vya afya vya kujiunga na klabu ya Napoli.

Real
Madrid na Napoli zimekubalina ada ya uhamisho wa Higuain kuwa kiasi cha
£32million na kukubaliana na mchezaji mwenyewe mkataba wa miaka mitano
kwa mshahara wa paundi 140,000 kwa wiki.
AZAM FC KUFANYA ZIARA KAMA YA MANCHESTER CITY
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Wana
lambalamba Azam fc wanatarajiwa kuondoka Agosti 2 mwaka huu kuelekea
nchini Afrika kusini kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiandaa na michuano
ya ligi kuu soka Tanzania bara na michuano ya kimataifa mwakani ambapo
watakaa kwa wiki mbili.
Afisa
habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga amesema wameamua kufanya ziara
bondeni kwani wao wameendelea zaidi kisoka kwa maana ya kuwa na ligi
bora, timu bora na mfumo wa kisasa wa kuendesha soka, hivyo watajifunza
mambo mengi kutoka kwao.
Jafar
alisema ziara hiyo itakuwa na manufaa makubwa sana kwani watacheza na
klabu kubwa za huko wakiwemo Supersport United na Orland Pirates.
“Malengo
yetu ni kufanya makubwa katika michuano ya kimataifa, lakini Ubingwa wa
ligi kuu ni muhimu sana kwetu. Na ndio maana tunaenda Afrika kusini
kuweka kambi ya wiki mbili”. Alisema Jafar.
Kuhusu
usajili, Jafar alisema wao hawajasajili mchezaji yeyote mpaka sasa na
hawana mpango wa kufanya hivyo kwani kikosi chao kipo kamili gado.
“Timu
yetu ni nzuri sana, kusajili mara kwa mara kunaharibu timu, sisi tuna
wachezaji wengi wakiwemo vijana wetu na ndio maana hatuhangaiki na
usajili”. Alisema Jafar.
Wakati
huo huo shirikisho la soka Tanzania, TFF, limethibitsha kupokea barua
kutoka klabu ya Azam fc kuwa wanatarajia kuondoka nchini kuelekea Afrika
kusini.
Katibu mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema Azam wamefanya vziuri kuwataarifu wao ili waende kwa kibali sahihi.
Tuesday, July 23, 2013
SOMA WASIFU WA KOCHA MPYA WA BARCELONA

FC Barcelona imefikia makubaliano rasmi kumsaini Gerardo Martino kuwa kocha mkuu wa timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili, kwa mujibu wa mtandao rasmi wa FC Barcelona.
Kilichobakia kwenye makubaliano hayo ni kusaini mkataba baada pande zote mbili kukubalina kila kitu.
Ratiba rasmi ya kuwasili kwake Nou Camp, utiaji saini wa mkataba na kutambulishwa rasmi itatangazwa msaa kadha yajayo.
Gerardo ambaye anajulikana kama ‘Tata’, alizaliwa jijini Rosario (Argentina) November 20, 1962. Ana uzoefu mkubwa wa soka la America ya Kusini, kwanza kama mchezaji na baada kama kocha, kazi yake ya mwisho ilikuwa kuiongoza klabu ya Newell's Old Boys, ambao alishinda nao ubingwa wa mwaka huu.
Gerardo Martino anakuwa kocha wa nne raia wa Argentina kuifundisha FC Barcelona baada ya Roque Olsen, Helenio Herrera na César Luis Menotti.
WASIFU WA KOCHA GERARDO MARTINO TATA
Kilichobakia kwenye makubaliano hayo ni kusaini mkataba baada pande zote mbili kukubalina kila kitu.
Ratiba rasmi ya kuwasili kwake Nou Camp, utiaji saini wa mkataba na kutambulishwa rasmi itatangazwa msaa kadha yajayo.
Gerardo ambaye anajulikana kama ‘Tata’, alizaliwa jijini Rosario (Argentina) November 20, 1962. Ana uzoefu mkubwa wa soka la America ya Kusini, kwanza kama mchezaji na baada kama kocha, kazi yake ya mwisho ilikuwa kuiongoza klabu ya Newell's Old Boys, ambao alishinda nao ubingwa wa mwaka huu.
Gerardo Martino anakuwa kocha wa nne raia wa Argentina kuifundisha FC Barcelona baada ya Roque Olsen, Helenio Herrera na César Luis Menotti.
WASIFU WA KOCHA GERARDO MARTINO TATA
SOURSE:SHAFFIH DAUDA
OCD: MSIWAPE MAJAMBAZI DAWA ILI WASIKAMATWE WAPENI POLISI DAWA ILI WAWAKAMATE
Inaripotiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Polisi katika wilaya ya Mufindi, PCD
Ambwene Manyasi amewataka waganga wa jadi kuacha mara moja kuwapatia
majambazi dawa za kutokukamatwa na polisi, na badala yake waganga hao
wawapatie askari polisi dawa za kuwaona na kuwakamata wahalifu.
Eliasa Ally wa gazeti la Majira anaripoti kutoka Mufindi kuwa kauli na wito huo umetolewa na OCD huyo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mufindi, wakati akizungumza na waganga wa jadi na tiba asilia kutoka Mudindi.
OCD amesema ni jukumu la kila mwananchi kuuchukia uhalifu na kulisaidia jeshi la polisi kutimiza wajibu wake. Amenukuliwa akisema ifuatavyo:
"Ninyi waganga wa jadi na tiba asili kazi yenu kubwa ni kutubu magonjwa yanayowasibu watu na siyo kutibu mbinu za majambazi ili wasiwe wanakamatwa wanapofanya uhalifu, hapo tutakuwa hatusaidiani, badala ya waganja kuwa wachonganishi, wawe waunganishaji wa wananchi, polisi na jamii. Badala ya kutoa dawa ya sisi polisi tusiwaone wala tusiwamamate majambazi, sasa nyinyi waganja mtoe dawa ya kutuwezesha kuwaona na kuwakamata kiurahisi majambazi wanaofanya uhalifu katika jamii yetu, huo ndiyo ushirikiano na polisi jamii tunayoizungumzia."
Aliwataka waganga hao kuhakikisha kuwa shughuli zao haziwi chanzo cha kutokea kwa maovu, kufumbia macho maovu na kusababisha jamii iwachukie waganga na polisi.
OCD alisema Jeshi la Polisi limejikita katika mambo makubwa matatu ambayo aliyataja kuwa ni polisi jamii, hali ya weledi na hali ya usasa.
Eliasa Ally wa gazeti la Majira anaripoti kutoka Mufindi kuwa kauli na wito huo umetolewa na OCD huyo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mufindi, wakati akizungumza na waganga wa jadi na tiba asilia kutoka Mudindi.
OCD amesema ni jukumu la kila mwananchi kuuchukia uhalifu na kulisaidia jeshi la polisi kutimiza wajibu wake. Amenukuliwa akisema ifuatavyo:
"Ninyi waganga wa jadi na tiba asili kazi yenu kubwa ni kutubu magonjwa yanayowasibu watu na siyo kutibu mbinu za majambazi ili wasiwe wanakamatwa wanapofanya uhalifu, hapo tutakuwa hatusaidiani, badala ya waganja kuwa wachonganishi, wawe waunganishaji wa wananchi, polisi na jamii. Badala ya kutoa dawa ya sisi polisi tusiwaone wala tusiwamamate majambazi, sasa nyinyi waganja mtoe dawa ya kutuwezesha kuwaona na kuwakamata kiurahisi majambazi wanaofanya uhalifu katika jamii yetu, huo ndiyo ushirikiano na polisi jamii tunayoizungumzia."
Aliwataka waganga hao kuhakikisha kuwa shughuli zao haziwi chanzo cha kutokea kwa maovu, kufumbia macho maovu na kusababisha jamii iwachukie waganga na polisi.
OCD alisema Jeshi la Polisi limejikita katika mambo makubwa matatu ambayo aliyataja kuwa ni polisi jamii, hali ya weledi na hali ya usasa.
Subscribe to:
Posts (Atom)









