Facebook Comments Box

Wednesday, July 24, 2013

AZAM FC KUFANYA ZIARA KAMA YA MANCHESTER CITY

935239_563553203685040_41751076_n 
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Wana lambalamba Azam fc wanatarajiwa kuondoka  Agosti 2 mwaka huu kuelekea nchini Afrika kusini kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiandaa na michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara na michuano ya kimataifa mwakani ambapo watakaa kwa wiki mbili.
Afisa habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga amesema wameamua kufanya ziara bondeni kwani wao wameendelea zaidi kisoka kwa maana ya kuwa na ligi bora, timu bora na mfumo wa kisasa wa kuendesha soka, hivyo watajifunza mambo mengi kutoka kwao.
Jafar alisema ziara hiyo itakuwa na manufaa makubwa sana kwani watacheza na klabu kubwa za huko wakiwemo Supersport United na Orland Pirates.
“Malengo yetu ni kufanya makubwa katika michuano ya kimataifa, lakini Ubingwa wa ligi kuu ni muhimu sana kwetu. Na ndio maana tunaenda Afrika kusini kuweka kambi ya wiki mbili”. Alisema Jafar.
Kuhusu usajili, Jafar alisema wao hawajasajili mchezaji yeyote mpaka sasa na hawana mpango wa kufanya hivyo kwani kikosi chao kipo kamili gado.
“Timu yetu ni nzuri sana, kusajili mara kwa mara kunaharibu timu, sisi tuna wachezaji wengi wakiwemo vijana wetu na ndio maana hatuhangaiki na usajili”. Alisema Jafar.
Wakati huo huo shirikisho la soka Tanzania, TFF, limethibitsha kupokea barua kutoka klabu ya Azam fc kuwa wanatarajia kuondoka nchini kuelekea Afrika kusini.
Katibu mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema Azam wamefanya vziuri kuwataarifu wao ili waende kwa kibali sahihi.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU