Facebook Comments Box

Friday, August 22, 2014

YANGA KUIFUATA SIMBA UNGUJA KESHO


 Simba
 Yanga
kitongoni Pemba:
Timu ya yanga inatarajiwa kutua mjini unguja Zanzibar hapo kesho ikitokea Pemba ilikokuwa imeweka kambi yake ya wiki moja, timu hiyo yanga itacheza mechi mbili tu za kirafiki mjini hapo ambapo mechi yake ya kwanza inatarajiwa kuwa siku ya juma pili jioni itakapo pambana na timu ya Shangani FC.

Wakati huo kocha wa timu hiyo Maximo amewaomba radhi wana yanga wa mjini Pemba kwa kutokucheza na timu ya Coastal Union kwa kile alichoita kuwa haikuwa kwenye program yao na pili muda wao umekwisha kwa kuwa walipanga kucheza mechi moja tu kisiwani pemba na mechi 2 Unguja.

Na baada ya hapo wataenda Dar es salaam kucheza mechi moja ya kimataifa, lakini kocha huyo aliwapongeza wana yanga hao kwa kuwa bega kwa bega na timu yao kwa kipindi chote ambacho timu hiyo ilikuwa visiwani humo.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU