Facebook Comments Box

Friday, August 22, 2014

HALI ILIVYO JIONI HII KATIKA BARABARA MBALIMBALI ZA JIJI LA DAR

Kumekuwa na foleni kubwa katika barabara ya Nyerere hii ikitokana na timu ya wachezaji wa zamani wa timu ya Real Madrid waliokuwa wakitoka uwanja wa ndege. Foleni hii ilikuwa katika barabara zote zinazokutana pale Tazara mara baada ya wachezaji hao kuondoka foleni imepungua na kubaki foleni ya Tazara. Foleni inaanzia sokota mpaka tazara.
Vilevile kuna foleni inayo anzia matumbi mpaka buguruni sheli watumiaji wa njia hiyo watafutie mbadala kama una haraka 

Basi lililowabeba wachazaji wa zamani wa Real Madrid lilitokea uwanja wa ndege wa Mwa Julius Nyerere. Baada ya basi hilo foleni ilipungua na kubaki ile ya kawaida.
Foleni ya uwanja wa ndege
MOROGORO ROAD NA MANDELA ROAD:

Kuna foleni ambayo sio kubwa sana trafiki wapo pale wakisaidia kuita magari kwa hiyo foleni imekuwa ikitembea japo si katika hali ya kuridhisha.

Kumeripotiwa pia foleni ndefu ya magari yanayotoka mkoani/mbezi kuja ubungo.

KAWAWA ROAD NA ALI HASSAN MWINYI ROAD:
 Hapa kuna foleni ambayo inaanzia hasa sehemu ya magomeni kwa barabara ya Kawawa hii inatokana na ujenzi wa barabara ziendazo kasi. Ila kwa upande wa Kawawa na Ally hassan Mwinyi kuna foleni ambayo inatembea kiasi.










Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU