Facebook Comments Box

Thursday, July 3, 2014

AZAM WASAJILI MSHAMBULIAJI WA HAITI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Haiti, aliyecheza Kombe la Mabara mwaka jana nchini Brazil, Leonel Saint-Preux ametua Azam FC kwa ajili ya kujiunga nayo kwa msimu ujao.

Kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon amesema amekuwa na mchezaji huyo kwa siku mbili na atahitaji muda zaidi kumuona kabla ya kuamua kumsajili au la. Mshambuliaji huyo aliyezaliwa Machi 12, mwaka 1985 in Cap-Haitien mara ya mwisho alichezea klabu ya FELDA United F.C. ya Ligi Kuu ya Malaysia.

Preux alianzia Zenith ya kwao,ambako alikuwa mfungaji mzuri katika Ligi ya nchini humo. Saint-Preux alisaini Minnesota Thunder ya Daraja la Kwanza Marekani Aprili 15, mwaka 2009, kabla ya kuhamia Hanoi ya Vietnam.

Machi 2010 alisiani mkataba wa awali na Aztex, lakini akatemwa baada ya kufeli vipimo vya afya. Kimataifa Saint-Preux, alianzia kuchezea timu za vijana za Haiti wa umri tofauti. Alikuwemo kwenye kikosi cha Haiti kilichofuzu michezo ya Olimpiki mwaka 2008 mjini Beijing, akifunga bao la kukumbukwa kutoka umbali wa mita 40 timu yake ikishinda 2-1 dhidi ya Canada.

Alianza kuchezea timu ya wakubwa ya Hati mwaka 2007. Alifunga
bao lake la kwanza timu ya taifa ya Haiti Novemba 19, mwaka 2008 katika sare ya 1-1 Surinam. Haiti ilifungwa 10-0 na Hispania kwenye michuano.
Hii ndio mechi ambayo Haiti ilitandikwa goli 10 kwa 0 mshambuliaji huyu wa azam anaonekana akikabwa na beki ya Hispania ambayo imeonesha udhaifu mkubwa kwenye kombe la dunia linalo endelea Brazil hivi sasa. Katika mechi hiyo mshambuliaji huyu mpya wa azam hakuweza kumsaidia timu yake kabisa.
CHANZO: BIN ZUEIRY


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU