Facebook Comments Box

Tuesday, June 25, 2013

TUME YA UCHAGUZI YA AHIRISHA TENA UCHAGUZI WA MADIWANI ARUSHA

Tume ya Uchaguzi ya Taifa imetangaza kuahirisha uchaguzi mdogo wa Madiwani uliokuwa ufanyike tarehe 30.06.2013 katika Kata nne -Elerai, Themi, Kaloleni, Kimandolu- za halmashauri ya Manispaa ya Arusha.

Mwenyekiti wa tume hiyo amesema badala yake uchaguzi huo utafanyika tarehe 14 Julai 2013.

Amesema sababu kubwa ya kuahirisha tena uchaguzi huo ni kutokana na kuendelea kutokuwepo kwa viashiria vizuri vya hali ya amani inayoruhusu uchaguzi huo kuendeshwa.

Uchaguzi huo awali ulipangwa ufanyike Jumapili ya terehe 16 Juni 2013, lakini uliahirishwa baada ya kutokea shambulio na mlipuko wa bomu kwenye mkutano wa mwisho wa kampeni za CHADEMA, siku ya Jumamosi ya tarehe 15 Juni 2013, shambulio ambalo lilisababisha vifo vya watu wawili papo hapo na wengine wawili siku chache baadaye.



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU