Facebook Comments Box

Tuesday, June 25, 2013

CARLO ANCELOTTI NDIO KOCHA MPYA WA REAL MADRID: PSG WAMCHUKUA BEKI WA ZAMAN WA MAN U KUWA KOCHA



Hatimaye Real Madrid wamemtangaza kocha Carlo Ancelotti kuwa kocha wao mpya.

Kocha huyo wa zamani wa Chelsea na PSG amechukua nafasi iliyoachwa wazi na na Jose Mourinho, ambaye amerudi Stamford Bridge.
Ancelotti, 54, amesaini mkataba wa miaka mitatu kuongoza benchi la ufundi la Santiago Bernabeu 


Wakati akiondoka PSG, mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa na beki wa Manchester United Laurent Blanc ameteuliwa kuchukua nafasi ya Ancelotti ndani ya klabu hiyo inayomilikiwa na waarbu matajiri kutoka Qatar.

Blanc tayari ana uzoefu na kazi ya ukocha baada ya kuzifundisha klabu ya Bordeaux na timu ya taifa ya Ufaransa.
 
SOURSE: SHAFFIH DAUDA


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU