Facebook Comments Box

Friday, January 25, 2013

KIGOMA: KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAKATIZA MKATABA NA MKANDARASI

 
Kikao cha kamati ya ulinzi na usalama chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Mkoa Luteni Kanali mstaafu Issa Machibya kimeridhia kusitishwa kwa Mkataba wa Mkandarasi M/S Kalyango Contructoins And Building Company Limited aliyekuwa akijenga daraja Nkwasi Wilayani Uvinza.

Mkandarasi Kalyango  Construction alikabidhiwa eneo la kazi Julai 5, 2012 na kutakiwa kukamilisha ujezi wa daraja la NKWASI   Okitoba 15, 2012, lakini pamoja na kuongezewa muda hadi Desemba 30, 2012 mkarandasi huyo alishindwa kukamilisha kazi hiyo.

Hadi anasimamishwa mkarandasi huyo alikuwa amelipwa zaidi ya milioni 25.7 ambazo ni kati ya shilingi milioni 97.4 alizostahili kulipwa kama angekamilisha ujenzi.

Baada ya taarifa ya mkuu wa mkoa safari  ikawa ni kuelekea eneo la ujenzi ambapo meneja wa wakala wa barabara mkoani Kigoma Narisi Choma ndiye aliyetoa taarifa kwa wafanyakazi wa  mkarandasi Kalyango kuwa hawatakiwi kuendelea na kazi.

Muda na  kwa nyakati tofauti wajumbe wa kamati ya  ulinzi na usalama, katika ziara zao, wamekuwa wakiwaonya wakandarasi wanaofanyakazi chini ya kiwango, kauli ambazo zinaungwa mkono na wakazi wa mwambao wa kusini mwa ziwa Tanganyika.




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU