Facebook Comments Box

Monday, November 18, 2013

PICHA ZA DIAMOND AKIHUDHURIA HARUSI YA PETER WA P SQUARE

Diamond akiwa na bwana harusi Peter wa P Square. Diamond alikuwa huko Lagos Nigeria katika utengenezaji wa wimbo wake mpya wa My Number one remox alio mshirikisha Davido.

Diamond akiwa na Adebayo

Diamond akiwa na Iyanya

Adebayo akiwa na bwana harusi



Sunday, November 17, 2013

MBWANA ALI SAMATA ATAJWA KATIKA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA AFRIKA

Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF
limetangaza majina ya wachezaji wa
kiafrika watakaowania tuzo ya mchezaji
bora wa Afrika kwa mwaka 2013 na
Mchezaji bora wa Afrika anayechezea
vilabu vya ndani ya Afrika mwaka 2013.
Katika majina hayo yapo majina mawili
ya wachezaji wanaotoka Afrika Mashariki
ambao ni Victor Wanyama raia wa Kenya
anachezea Southampton FC ya England
ambaye ni miongoni mwa wachezaji 25
watakaowania tuzo ya Mchezaji bora wa
Afrika, huku Mbwana Samatta raia wa
Tanzania anayechezea klabu ya TP
Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia
ya Congo yeye ameteuliwa kuwania tuzo
ya Mchezaji bora wa Afrika anayechezea
timu za Afrika.
Wachezaji 25 watawania tuzo ya mchezaji
bora wa Afrika na 21 Mchezaji bora wa
Afrika anachezea timu za ndani ya
Afrika.
Washindi wa tuzo hizo wanatarajiwa
kutangazwa Januari 9, mwaka 2014 mjini
Lagos nchini Nigeria.
Orodha kamili ya wachezaji
waliotangazwa na CAF na timu
wanazotoka hii hapa chini.
1. Ahmed Musa - Nigeria - CSKA Moscow
2. Asamoah Gyan - Ghana - Al Ain
3.Dame N'Doye - Senegal - Locomotiv
Moscow
4. Didier Drogba - Cote d'Ivoire -
Galatasaray
5. Emmanuel Emenike - Nigeria -
Fenerbahce
6. Islam Slimani - Algeria - Sporting
Lisbon
7. John Mikel Obi - Nigeria - Chelsea
8. Jonathan Pitroipa - Burkina Faso -
Stade Rennais
9. Kévin Constant - Guinea - AC Milan
10. Kwadwo Asamoah - Ghana - Juventus
11. Luís Carlos Almada Soares (platini) -
Cape Verde - AC Omonia
12. Mehdi Benattia - Morocco - AS Roma
13. Mohamed Aboutrika - Egypt - Al Ahly
14. Mohamed Salah - Egypt - Basel FC
15. Nicolas Nkoulou - Cameroon -
Marseille
16. Pierre-Emerick Aubameyang - Gabon -
Borussia Dortmund
17. Ryan Isaac Mendes da Graça - Cape
Verde - Lille
18. Saladin Said - Ethiopia - Wadi Degla
FC
19. Seydou Keita - Mali - Dalian Aerbin
F.C
20. Sofiane Feghouli - Algeria - Valencia
21. Sunday Mba - Nigeria - Warri Wolves
22. Victor Wanyama - Kenya -
Southampton FC
23. Vincent Enyeama - Nigeria - Lille
24. Yao Kouassi Gervais 'Gervinho' - Cote
d'Ivoire - AS Roma
25. Yaya Toure - Cote d'Ivoire -
Manchester City
1. Adane Girma - Ethiopia - St George
2.Ahmed Fathi - Egypt - Al Ahly
3. Alexis Yougouda Kada - Cameroon -
Coton Sport
4. Ali Machani - Tunisia - CAB
5. Bapidi Fils Jean Jules - Cameroon -
Coton Sport
6. Daine Marcelle-Klate - South Africa -
Orlando Pirates
7. Fakhreddine Ben Youssef - Tunisia -
CSS
8. Getaneh Kebede - Ethiopia - Bidvest
Wits
9. Idrissa Kouyate - Cote d'Ivoire - CS
Sfaxien
10. Iheb Msakni - Tunisia - Esperance
11. Luyanda Lennox Bacela - South Africa
- Orlando Pirates
12. Mbwana Samatta - Tanzania - TP
Mazembe
13. Moez Ben Cherifia - Tunisia - EST
14. Mohamed Aboutrika - Egypt - Ahly
15. Rainford Kalaba - Zambia - TP
Mazembe
16. Senzo Meyiwa - South Africa -
Orlando Pirates
17. Soumbeila Diakite - Mali - Stade
Malien
18. Sunday Mba - Nigeria - Warri Wolves
19. Tresor Mputu - DR Congo - TP
Mazembe
20. Waleed Soliman - Egypt - Al Ahly
21. Yannick N'djeng - Cameroon - EST



RIPOTI YA MAREKANI KUHUSU USAFIRISHAJI WA BINADAMU 2013 ISOME HAPA



Marekani imetoa ripoti inayozungumzia usafirishaji wa binadamu ya mwaka 2013, huku ikiitaja Tanzania kuwa kinara wa kunyanyasa wasichana, kuwatumikisha katika ngono na usafirishaji wa binadamu.

Ripoti hiyo iliyotolewa na idara ya nchi hiyo inayohusika na diplomasia (US Department of State, Diplomacy in Action), pia inaitaja Tanzania kuwa ni kitovu cha njia ya kusafirisha wanawake, watoto na wanaume ambao hutumikishwa kwenye kazi za mashambani na biashara ya ngono.

Ripoti hiyo iliyozinduliwa Julai mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Seneta John Kerry inaweka bayana kwamba biashara ya usafirishaji wa binadamu hufanywa na baadhi ya ndugu na marafiki ambao hutoa ahadi kwa wahusika kwamba wanakwenda kuwasomesha au kuwatafutia ajira nzuri mijini.

“Unyonyaji wa wasichana wadogo na utumikishaji majumbani ndilo tatizo linaloongoza, ingawa kesi za watoto kusafirishwa kwa ajili ya biashara ya ngono katika mpaka wa Tanzania na Kenya zinaongezeka. Pia, wasichana wananyonywa kwenye maeneo ya utalii,” inasema sehemu ya ripoti hiyo. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, watoto kutoka Burundi na Kenya, watu wazima kutoka Bangladesh, Nepal, Yemen na India wanatumikishwa kufanya kazi kwenye sekta za kilimo, madini na majumbani nchini Tanzania.

“Baadhi ya raia kutoka nchi jirani huingia Tanzania kwa hiari yao, lakini hulazimishwa kufanya kazi majumbani kabla ya kupelekwa kutumikishwa kwenye biashara ya ngono Afrika Kusini, Ulaya na Mashariki ya Kati,” inaeleza.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki alimtaka mwandishi kumtumia ripoti hiyo kwa njia ya barua pepe ili aweze kuisoma na kuitolea maelezo.

Alipotafutwa siku ya pili, alisema kuwa ameipokea na kuikabidhi ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) ili ifanyiwe kazi na baadaye kutoa majibu.

“Ripoti niliipata nikaikabidhi ofisi ya DPP kwa kuwa wao ndio wanaoweza kuitolea maelezo baada ya kuisoma. Maoni yangu lazima yawe ya kitaalamu siwezi kusema bila kupata taarifa kutoka kwao,” alisema. Lawama kwa Serikali Ripoti hiyo inaitupia lawama Tanzania kwa kutokuwa na sheria thabiti za kupambana na biashara haramu ya kusafirisha binadamu, huku ikitolea mfano namna ilivyoshindwa kuwasaidia raia wake waliokuwa wakinyanyaswa nje ya nchi.

“Kamati ya Serikali ya kupambana na usafirishaji binadamu, haijachukua hatua za kutosha katika kutekeleza mpango mkakati wa kupambana na vitendo hivyo,” inaeleza na kuongeza:
“Serikali imeshindwa kutenga fedha kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa usafirishaji wa binadamu kama ambavyo inaelekezwa kwenye sheria ya kudhibiti biashara hiyo ya 2008.”

Taarifa hiyo inaitaka Tanzania kuongeza nguvu katika kutekeleza sheria ya kudhibiti biashara ya kusafirisha binadamu ya 2008 kwa kuwakamata na kuwashtaki wahusika wote, lakini ikaikosoa kwa kusema inatoa adhabu ndogo kwa mtu anayebainika kufanya makosa, ikiwa ni pamoja na kumhukumu kwenda jela miaka 10, kulipa faini au vyote viwili kwa pamoja.

“Sheria hiyo haifanani na nyingine kama za mtu anayepatikana na kosa la kubaka au kufanya kosa jingine la jinai. Mamlaka imesema ina kesi nne inazozichunguza, saba zipo mahakamani toka mwaka jana, zikiwepo mbili mpya,” inasema ripoti. Pia, Serikali ya Tanzania imelaumiwa kwa kushindwa kuripoti maendeleo ya uchunguzi wa maofisa wake waliotuhumiwa kujihusisha na biashara ya usafirishaji binadamu. LHRC na TGNP Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema tatizo la usafirishaji wa binadamu pia linachangiwa na wasichana kuwa na tamaa ya maisha mazuri, hivyo kukubali ahadi ambazo hupewa kwamba wanapelekwa kusoma, wasifahamu wanarubuniwa.

“Wengi wanatamani kwenda ‘majuu’ wakidhani watapata elimu, lakini baadaye wanaingizwa kwenye vitendo vinavyowafedhehesha na kuwafanya wakate tamaa kabisa,” alisema. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Usu Mallya alisema katika siku za karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wasichana waliochukuliwa vijijini kwenda mijini kufanya kazi.

Alisema pamoja na tatizo hilo kuongezeka hapa nchini, hakuna tafiti za kutosha ambazo zimefanywa na wadau mbalimbali kuonyesha madhara yaliyopatikana hadi sasa. “Katika siku za usoni kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo vya kunyimwa chakula, kupigwa na kufukuzwa kazi huku wasichana wengine wakitumika kwenye biashara ya ngono,” alisema na kuongeza:

“Ripoti hii isiishie kwenye makabrasha bali ifanyiwe kazi ili jamii yote ijue kuwa hili ni tatizo.” Ripoti hiyo inabainisha kuwa watu 47,000 pekee ndio walioweza kuokolewa mwaka jana kutoka kwenye mazingira ya utumikishwaji kati ya milioni 27 waliopo katika hali hiyo duniani. Tanzania imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi 44 ambazo zinajaribu kupambana na biashara hiyo, lakini hali inazidi kuwa mbaya zaidi.
  Chanzo:JAMIIFORUMS


Friday, November 15, 2013

HUU NDIO MUONEKANO MPYA WA RAY KIGOSI

Muonekano huu unaenda kuuona wa muigizaji na muongozaji wa bongomovie “Vicent Kigosi”unahusisha kubadilisha rangi ya nywere zake, tatoo kubwa kwenye mikono yote miwili na mavazi kama msanii wa bongoflava.

Yeye mwenyewe kwenye picha moja wapo aliandika caption ya “Je nageukia bongoflava au kuna nini kinakuja?”. Jinsi inavyoonekana ni moja ya maandalizi ya movie mpya kutoka RJ Company.



HUYU NDIO MCHEZAJI ALIE SAJILIWA NA YANGA



Tuesday, November 12, 2013

DR. SENGONDO MVUNGI AFARIKI DUNIA AFRIKA KUSINI ALIPOPELEKWA KWA MATIBABU ZAIDI



Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini amefariki dunia. -
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid leo jioni (Jumanne, Novemba 12, 2013), Dkt. Sendongo Mvungi majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark. -

"Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg-nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo (Jumanne, Novemba 12, 2013) saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini," amesema Bw. Rashid katika taarifa yake fupi ya awali. -

"Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini kwa mazishi zinaendelea na taarifa zaidi zitatolewa kesho (Jumatano, Novemba 13, 2013)," ameongeza. -

Marehemu Dkt. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, 2013 kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013. -

Katika taarifa yake, Tume pia imewaomba watanzania wote kuungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dkt. Mvungi katika kuomboleza msiba huo.


Monday, November 11, 2013

ALICHOSEMA ZITO KABWE KUHUSU TAARIFA YA SIRI YA CHADEMA

NILIPOKUWA katika ziara ya bara la
Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba
2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia
ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa
ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa
imesambazwa katika mitandao
mbalimbali ya kijamii.
“Taarifa ya Chadema inasema kwamba
chama hicho (chama changu) kilikuwa
kimechunguza mwenendo wangu tangu
mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa
mimi napokea fedha kutoka Chama Cha
Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga
Chadema.
Ripoti hiyo ilinihusisha pia na
mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea
Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti
hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi
kiasi cha dola 250,000 za Marekani
kupitia kwenye akaunti yake binafsi.
Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo
wa kiwango cha kutisha,
imenifadhaisha, kunisikitisha na
kunikasirisha.
Taarifa hii iliibuliwa katika kipindi
ambacho nilikuwa safarini kutetea haki
za Watanzania na Waafrika ambao
utajiri wao wa rasilimali unafaidiwa na
watu wachache waliohifadhi mali katika
nje za nje na pia kupigania makampuni
ya mataifa tajiri yalipe kodi stahiki
katika nchi zetu.
Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni
kutaka kunipoteza kutoka katika nia na
dhamira yangu ya dhati ya kutaka
Watanzania wafaidike na utajiri wao.
Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo
waliamua kutoa taarifa yao unazua
maswali mengi kuliko majibu.
Nafahamu kwamba mimi ni mwanasiasa
ambaye nimekuwa mlengwa (target) wa
mashambulizi kutoka kwa makundi
mbalimbali ya wanasiasa na vikundi
vyao. Kama mwanasiasa, niko tayari
kupokea changamoto zozote zinazokuja
na uanasiasa wangu.
Hata hivyo, ambacho sitakubali ni kwa
watu kutumia jina langu na uanasiasa
wangu kunichafua mimi binafsi na watu
wengine wasiohusika kwa sababu ya
kutaka kutimiza malengo yao ya
kidhalimu.
Raia huyo wa Kijerumani tayari
amekana kuhifadhi fedha zangu. Kwa
maelezo yake kwa baadhi ya viongozi
wa Chadema amekana kuwa na akaunti
inayotajwa na amekana pia kuwepo
nchini Ujerumani katika siku na wakati
uliotajwa kwenye ripoti hiyo.
Ripoti hiyo imemtaja pia mtu kama Dk.
Charles Kimei, Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya CRDB ikidai kwamba nilikutana
naye na alishiriki kwenye igizo hilo la
kunipa fedha.
Niseme mapema kwamba tangu kuzaliwa
kwangu sijawahi hata mara moja
kukutana na Dk. Kimei popote pale ndani
au nje ya nchi. Kumuingiza mtu ambaye
amejenga jina lake kwenye taaluma ya
kibenki kwa sababu tu ya lengo ovu la
kumchafua Zitto Zuberi Kabwe si
uungwana bali ni unyama.
Kutokana na uchafuzi huu wa wazi dhidi
ya taswira yangu binafsi na watu
wengine walioingizwa kwenye mkumbo
huu, nimeandika rasmi kwa Katibu Mkuu
wa Chadema, Dk.Wilbrod Slaa
kumwomba athibitishe kwamba
kinachoitwa Taarifa ya Siri ya Chadema
ni kweli ni taarifa ya chama au
kiikanushe ili niweze kuchukua hatua za
kisheria dhidi ya waandishi wa hekaya
hiyo.
Cha ajabu, nimepokea ujumbe wa
kutishiwa maisha kutoka kwa mtu
anayejiita Theo Mutahaba na kuahidiwa
KUPOTEZWA endapo nitaendelea na
jitihada zangu za kupambana na ufisadi
na kutafuta haki kwa Watanzania wote
pasipo kujali tofauti zao za kiitikadi,
kikanda, kikabila na kidini.
Natarajia kuchukua hatua kali za
kisheria dhidi ya wote ambao
wamehusika na utungaji na uenezi wa
taarifa hii. Nitahakikisha kwamba
wahusika wanatafutwa na kufunguliwa
mashitaka stahiki ya upotoshaji na
kuchafuana.
Ni matarajio yangu kwamba wale wenye
mapenzi mema na Tanzania, mimi
binafsi na utawala wa sheria,
wataelewa nia yangu ya kutafuta haki
katika suala hili.
Nimeamua kujitolea maisha yangu kwa
ajili ya Watanzania na kama alivyopata
kusema Rais Mstaafu wa Afrika Kusini,
Nelson Mandela; “Struggle Is My Life.”
Forward Ever, Backward Never- Kwame
Nkrumah
Zitto Kabwe (Mb)



Friday, November 8, 2013

KOCHA WA AZAM FC AACHIA NGAZI

Kwa mujibu wa tovuti ya Azam Fc kocha wao Stewart Hall amefikia makubaliano na kilabu hiyo ya kusitisha mkataba wao jana

BREAKING NEWS: JUMA KASEJA ASAINI YANGA

Juma Kaseja asaini Yanga.Katika habari ambazo hazijathibitishwa rasmi inasemekana golikipa na nahodha wa zamani wa team ya Simba Sc Juma Kaseja(tanzania 1) amesain mkataba wa mwaka mmoja na team ya Yanga yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.Katika kuthibitisha hilo kiongozi mmoja wa juu kabisa wa Yanga ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa Kaseja amepewa mkataba wa mwaka mmoja na Yanga na leo mchana ilikuwa wamalizane.Kiongozi alifafanua zaidi akisema baadhi ya viongozi walikuwepo uwanjani kushuhudia mchezo baina  ya Yanga dhidi ya JKT Oljoro na viongozi wengine walikuwa wamebaki kumalizana na Juma Kaseja.Hii itakuwa mara ya pili kwa Kaseja kusajiliwa na Yanga baada ya mara ya kwanza kusajiliwa ambapo aliitumikia kwa mwaka mmoja na baadaye kurejea tena Simba mpaka mwisho wa msimu uliopita ambao Simba waliaamua kumtema kutokana na kile kilichodhaniwa ni kushuka kiwango kwa golikipa huyo n



BREAKING NEWS: KOCHA MKUU WA AZAM AJIUZURU BAADA YA SARE YA 3 -3 CHAMAZI

Kocha muingereza stewart hall ametangaza
kujiuzuru kufundisha klabu ya Azam fc baada
ya kukubalina na wamiliki wa timu hiyo,
stewart aliwaaga benchi la ufundi na
wachezaji mara baada ya mechi na Mbeya
city
Stewart'' ni kweli nimewaaga wachezaji na
benchi la ufundi wenzangu, inabidi niondoke
kwa sababu nimepata kazi sehemu nyingine
na wamiliki wa timu wameridhika, nawatakia
kila la kheri''.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU