Facebook Comments Box

Thursday, August 21, 2014

JUSA NA MAALIM SEIF WAMTANGAZA MANSOUR SHUJAA

Mansour
Na mwandishi wetu Unguja :

Wiki  moja  kabla  ya  kupewa  dhamana  Mh. Mansour  Yusuph  Himid  katika  mkutano  wa  Chama cha wananchi  Cuf  uliofanyika  kwenye  viwanja  vya  Demkokrasia  Kibanda maiti  mjini  Unguja  alitangazwa  kuwa  ni  shujaa  tena  kidume haswaa, hayo  yalisemwa na Mh.Ismail  Jussa  Ladhu  pale aliposimama  na kuzungumzia  kwa  ufupi  juu  ya  kukamatwa kwa  waziri  huyo  wa  zamani wa serikali  ya  Smz, mh.Jussa  alisema kuwa  walipokuwa  wamempelekea  chai  ya  asubuhi  bw. Mansour  aliwaambia  wasimletee  tena  chai  kwa  kuwa atakunywa  tu  uji  wa kule  gerezani na kuwa  uji  ule wa  gerezani  ni mtamu sana  huku  akimalizia  kwa  kumwita  ni shujaa  tena  kidume hasa.

Maalim  Seif  yeye  kwa  upande  wake  akimzungumzia  mh.  Alisema  kuwa  Mansour  Yusuph  Himid  wote  tunajua  kuwa  ni  raia  wa  Zanzibar  kazaliwa  Zanzibar  na  baba  yake  ni miongoni  mwa  wanamapinduzi, waliokuwa hawamjui  wajue  hivyo, ametoka  katika   mifupa ya wanamapinduzi, kapatwa na mtihani kakamatwa na sasa  hivi  yuko  jela, Na mh. Jussa  amewaambia  kuwa  kwenda  jela  ni  ishara  nzuri, niwaulizeni  nabii  Yusuph  hakwenda  jela?  Sasa  ikiwa  mitume  walikwenda  jela  itakuwaje  sisi? Yanayo  mkuta  Mansour  leo  hii  wanampitisha  kwenye  njia  zile  zile  walizompitisha  Maalim  seif, Maalim  Seif  kwanza  alifukuzwa  Chama, kama  vile  haitoshi  wakamtafutia  shitaka  halina  dhamana  wakamuweka  jela kwa muda  waliotaka  wenyewe  ulipofika  muda  wakaniambia  toka, lakini  wakaniambia unatoka  lakini  huna  ruhusa  ya  kuzungumza  kwenye  mikutano  ya  hadhara  nikaitikia  Inshaallah, tumeanzisha  Cuf  mkutano  wa kwanza  tumeufanya  malindi  pale  mimi  nipo  kama  makamu  mwenyekiti  lakini  ndiyo  nilifungwa   mdomo  nilikuja  kwenye  jukwaa  pale  nyote  mnakumbuka  nikatoa  mkono  tu  wakaenda  wenyewe  mpaka  wakaamua  basi  sasa  kesi  tunaifuta  na  maalim  Seif  Yule  Yule  sasa  ni  makamu  wa  rais  wa  Zanzibar.

Nakumbuka  wakati  ule  napelekwa  jela  askari   walikuwa  wananitukana  na  kuninyanyasa  mie  kimyaa   kabisa  lakini  mungu  si  Athumani  wala  si  Msaki  mmoja  wao yupo  Dar  es  salam  pale  akiniona  sasa  hivi  anapiga  saluti, kwa hivyo  nasema  na  Mansour  ni  ishara  njema  na  hatujui  mwenyezimungu  huko  mbele  kamuandikia  nini ,lakini  najua  kamuandikia  mambo  mema  Inshaallah, lakini  papo  hapo  niseme  nataka  niamini  kwamba  Mansour  hakukamatwa  kwa sababu  yeye  si  mwanachama  tena  wa  chama  cha  mapinduzi, nataka  niamini  kwamba  Mansour  kakamatwa  kwa  sababu  ametoka  hadharani  na kuunga  mkono  mamlaka  kamili  kwa Zanzibar, nataka  niamini  kwamba  Mansour  hakukamatwa  kwa sababu  kasema  wazi  wazi  kwamba  atamuunga  mkono  maalim  Seif  mwakani  kwenye  uchaguzi, nataka  niamini  kwamba  Mansour  hakukamatwa  kwa  sababu  kasema  atagombea  jimbo  la Kiembe  samaki  kwa  tiketi  Cuf, Nataka  niamini kuwa  hizo  siyo  sababu  hizo  siyo  sababu  zilizofanywa  Mansour  akamatwe, Nataka  niamini  kwamba  Mansour  atatendewa  haki  kama  raia  yoyote  mwingine  katika  nchi  hii  na kwamba  yale  mashitaka  yote  yanayomkabili  basi  sheria  itachukua  mkondo   wake  pasiwepo  na  shinikizo  za  kisiasa,akitoa  mfano  kwenye  kesi  Maalim  seif  alisema  yeye  siku  moja  ya  kesi  hakimu  anayehusika  alikuwa  anakutana  watu  kwenye  ofisi  ya  waziri  kiongozi  halafu  wanaamua  kesho  tukafanye  kwa maalim  Seif, sasa  nataka  niamini  hayo  hayatatendeka   kwa  Mansour kwamba  mahakama  iliyo  huru  itaweza  kabisa  kusikiliza  shitaka  lilipo  mbele  yake  kwa  mujibu  wa  sheria  za  Zanzibar, kwa  sababu  sasa  hivi  siyo  tena  mwaka  64, wala  sasa  hivi  siyo  tena  mwaka  74  wala  siyo  tena  84  sasa  hivi  viongozi  wote  tunapiga  kelele  tunataka  utawala  wa  sheria.
Tumeambiwa  kabla  ya  kufa  huajaumbika  huyu  mh. Mansour  si alikuwa  Waziri  huyu  na walikuwa  wakimpigia  saluti  huyu si mwenzao? Sasa  kama  watu  wapo  walikula  njama  basi  wajue  mwenyezimungu  anahukumu  hapa  hapa  duniani  Akhera  inakwenda  hesabu tu, kwa  hivyo  yaliyomfika  Mansour  yanaweza  kumfika  mtu  yeyote sasa  kama  kuna  watu  kweli  wamekula  njama   Mnsour   akae  ndani  basi  wajue  kuwa  wakati  mwingine  ukilitandika  godoro  uliloweka  miba ili mwenzako  aje  alale  basi  ipo  siku  utakuja kulilalia wewe alimalizia  maalim  Seif.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU