Facebook Comments Box

Monday, October 28, 2013

NI JAMAL MALINZI




Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera, Jamal Malinzi amechaguliwa kuwa Rais Mpya wa shirikisho la soka nchini, TFF. 

Malinzi ameshinda uchaguzi huo wa leo uliokuwa ukifanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa NSSF, Water Front jijini Dar es Salaam kwa kupata asilimia 78 ya kura na kumbwaga mpinzani wake Athuman Nyamlani. 

Malinzi atachukua nafasi ya Leodegar Tenga aliyekuwa Rais wa TFF tangu mwaka 2005. Taarifa za kuchaguliwa kwa Malinzi kuwa rais mpya wa TFF, zimepokelewa kwa furaha na binti yake, mtangazaji wa Clouds FM, Loveness aka Diva aliyetweet: 

My dad is the new president TFF¦.. What a good news. Cant wait to get home and give him a big hug and a kiss. Gooooo Daddy” Diva (@DivaBos) October 27, 2013

Malinzi alishika nyadhifa mbalimbali Yanga zikiwemo seneta, mkurugenzi wa kuchaguliwa, kaimu katibu mtendaji na katibu mkuu. 

Amekuwa mwenyekiti wa mashindano ya mpira wa miguu mkoa wa Pwani (2009-2011) na mjumbe wa Baraza la Michezo la Mkoa wa Dar es Salaam (2009-2012). 

Toka 2011 hadi sasa ni mjumbe kwenye Kamati ya Utendaji ya Chama cha Mpira wa Miguu wilaya ya Misenyi, pia mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Kagera.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU