Facebook Comments Box

Thursday, October 24, 2013

YAYA TOURE ASIKITISHWA NA UBAGUZI WA RANGI KATIKA SOKA


Kiungo wa kati wa Manchester City Yaya Toure ameonesha kughadhabishwa na kulitaka shirikisho la kandanda barani ulaya, UEFA kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya ushangiliaji wenye kuashiria ubaguzi wa rangi, baada ya kudai kuwa vilifanyika dhidi yake timu yao ilipotoka na ushindi wa 2-1 jijini Moscow.

Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Ivory coast alisema alimlalamikia mwamuzi wa mchezo huo Ovidiu Hategan kuhusu kitendo hicho, alipokuwa nahodha wa timu yake.


Toure anafikiri kuwa pengine shirikisho la soka barani ulaya litachukua hatua ya kufungia uwanja kwa miezi au miaka kadhaa.


Mwezi May, UEFA ilitangaza kuchukua hatua kwa vitendo vinavyoashiria ubaguzi wa rangi kwa kufungia kwa muda mfupi viwanja iwapo ni kosa la kwanza, na kufunga moja kwa moja kwa
kosa la pili sambamba na adhabu ya kulipa
pauni 42,800.


Chanzo: BBC swahili


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU