Facebook Comments Box

Thursday, October 24, 2013

YANGA YAWASIMAMISHA WACHEZAJI WAKE BAADA YA KUTOKA SARE YA BAO 3 KWA 3 NA SIMBA

 Wachezaji wa Yanga wakitafakari baada ya kufungwa bao 3 za haraka haraka na Simba kipindi cha pili.

Timu ya Yanga imepata Ushindi wa Mabao 3 kwa bila dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora Uwanja wa Taifa jana (Jumatano) baada ya kuwasimamisha baadhi ya wachezaji wake wa kikosi cha kwanza eti wakiamini kuwa ndiyo walio sababisha timu ya Simba irudishe mabao matatu waliokuwa wametangulia kuwafunga wao katika kipindi cha kwanza katika mpambano wao uliochezwa katika uwanja wa Taifa siku ya Jumapili ya tarehe 20/10/2013, mpambano ambao ulitoa matokeo ya 3-3 kwa timu zote mbili.

Wachezaji wanaotuhumiwa kwa Uzembe huo na waliwekwa benchi katika mechi iliyofuata ya ligi kuu kati ya Yanga na Rhino Rangers ni NADIR HAROUB 'KANAVARO' ambaye nafasi yake ilichukuliwa na TWITE, ATHUMANI IDDI 'CHUJI' na GOLKEEPER ALI MUSTAFA 'BATTEZ' ambaye nafasi yake ilichukuliwa na DEO MUNISH 'DIDA'.

Yanga hawana haja ya kumtafuta mchawi wa kufungwa kwao kwani wao sio wakwanza kutoka sare au kufungwa, na kama watakuwa wakimtafuta mchawi kila watakapo fungwa itakuwaje? kwani mpira ni mchezo wa makosa mchezaji anapofanya makosa ndipo mwingine anatumia makosa hayo kufunga, na kama kungekuwa hakuna makosa yoyote basi mabao yasingepatikana katika mechi mbalimabali!.

Kocha wao Brandis amewaomba radhi Yanga kwa kutoka sare na Simba, Tatizo lao Yanga wameisha jiona kuwa wao ni timu ya kushinda tu kila mechi kwamba wao hawastahili kufungwa na timu yoyote jambo ambalo sio sahihi katika soka. Ili mchezo wa mpira ukamilike kuna matokeo ya aina tatu ambayo ni aidha kushinda, kufungwa na kutoka sare.




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU