Facebook Comments Box

Thursday, September 19, 2013

ARSENAL YAPATA USHINDI UGENINI KWA KUWAFUNGA WENYEJI WAO MABAO 2 - 1





Wachezaji wa Arsenal Theo Walcott na Aaron Ramsey jana usiku waliiwezesha timu yao kupata ushindi mzuri ugenini pale walipokwamisha nyavuni mabao yao mawili dhidi ya moja la wenyeji wao Marseille na kuihakikishia timu yao ushindi wa mabao 2-1, katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa, Arsenal ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Walcott dakika ya 65 kabla ya kuongeza la pili dakika ya 83 lililofungwa na Ramsey.
Marseille walipata bao la kufutia machozi dakika ya 90 kwa njia ya penalti baada ya ndugu yake Andrew Ayew, Jordan Ayew kuangushwa kwenye eneo la hatari na Mwamuzi kuamuru adhabu ya Penati.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU