Facebook Comments Box

Sunday, May 5, 2013

UPDATES ZA KANISA LILILOLIPULIWA LEO ARUSHA

 DSCN2226
DSCN2228Ulinzi ukiimarishwa eneo ulipotokea mlipuko huo na kujeruhi makumi ya waumini

Mkuu wa Mkoa Mulongo naye  amefika  eneo  la  tukio  na  kuwafariji  wahanga  wa  tukio  la  bomu....

RPC  wa  mkoa  wa  Arusha  naye aliambatana  na  mkuu  wa  mkoa  na  muda  huu  alikuwa  anatoa  nasaha  zake  kwa  wananchi....
RPC  amesema  tukio  hili  ni  la kigaidi. Amesema kuwa  aliyehusika alijitokeza nyuma ya jengo kwa kujificha na kurusha bomu. ...
Amesema kuwa Polisi wanawasaka waliohusika  na  unyama  huu  na  ameomba yeyote  mwenye taarifa yoyote aisaide polisi. ..
Waliojeruhiwa ni 50 .Hao wana majeraha ya kawaida  na 3 wako  mahututi
Mpaka sasa  mtu mmoja anashikiliwa  na  polisi kwa mahojiano  zaidi


 INASEMEKANA KUWA BOMU LIMELIPUKA KATIKA KANISA KATOLIKI PAROKIA MPYA YA OLASITI ILIYOKUWA INAZINDULIWA LEO JIJINI ARUSHA MUDA HUU. BOMU HILO LIMELIPUKA WAKATI WAUMINI WA KANISA HILO LA KATOLIKI WAKIENDELEA NA SHEREHE ZA UZINDUZI WA KANISA HILO JIPYA JIJINI ARUSHA  NA MPAKA SASA  HAIJAWEZA KUJULIKANA IDADI KAMILI YA WATU WALIOJERUHIWA LAKINI TAARIFA ZINASEMA KUWA KUNA BAADHI YA WATU WAMEJERUHIWA NA KUWAHISHWA HOSPITALI KWAAJILI YA MATIBABU NA MPAKA MUDA HUU HAKUNA ALIYEPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA BOMU HILO KULIPUKA.

Mh Zitto Kabwe alizungumzia hilo katika ukuta wake wa facebook



Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU