Facebook Comments Box

Sunday, May 5, 2013

AZAM WAKUBALI KUTOLEWA NA AS FAR RABAT YA MOROCCO


 
 
SOKA ni mchezo wa bahati wakati mwingine. Naam sadakta, usemi huo umedhihirika jana kwenye Uwanja wa Prince Moulay Abdellah baada ya Azam kulala 2-1 mbele ya wenyeji AS FAR Rabat na kutolewa katika Raundi ya Tatu ya Kombe la Shirikisho Afrika, licha ya kupata nafasi nzuri ya kusonga mbele dakika ya 81. “Tumekosa penalti dakika ya 81, siwezi kumlaumu refa ikiwa tumekosa penalti zimebaki dakika tisa,” alisema kocha wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall baada ya mchezo.

Azam ilihitaji sare yoyote ya mabao ifuzu na ilikaribia kuipata dakika ya 81 ilipopata penalti ikiwa nyuma kwa mabao 2-1, lakini fundi wa upigaji wa michomo hiyo, John Raphael Bocco alikwenda kugongesha mwamba mpira huo.

SOURCE:AZAM FC BLOG


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU