Facebook Comments Box

Sunday, May 5, 2013

LIVE MATCH CENTRE: RUVU SHOOTING 1 - 3 SIMBA SC

Dk 90+3 FULL TIME! RUVU 1-3 SIMBA

Dk 90 Ruvu wamepotea na Simba wanatawala tena kiungo. Dakika tatu zimeongezwa.

Dk 88 GOOOO....! Ismail Mkoko anaipatia Simba bao la tatu kwa kichwa akiunga krosi ya Kiemba. Ruvu 1-3 Simba.

Dk 86 GOOOOO....! Edward Christopher anaifungia Simba bao la pili akimalizia mpira uliotemwa na kipa Haule. Ruvu 1-2 Simba.

Dk 82 Simba wanafanya mabadiliko ametoka Haruna Chanongo ameingia Ismail Mkoko.

Dk 81 Ruvu wanafanya mabadiliko ametoka Said Madega ameingia Hamis Kisuke.

Dk 80 Kipa wa Ruvu, Haule anaumia na kutibiwa kwa muda.

Dk 74 Ngassa anachezewa faulo nje kidogo ya lango la Ruvu.

Dk 70 Simba imefanya mabadiliko ametoka Messi ameingia Edward Christopher.

Dk 64 Kulwa Mfaume anapiga shuti kali linalotoka nje kidogo ya lango la Simba.

Dk 59 YELLOW CARD...! Ngassa anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kuutumbukiza mpira wavuni baada ya filimbi ya kuotea kupulizwa.

Dk 55 Ruvu wamefanya mabadiliko wametoka Said Dilunga na Raphael Keyala na wameingia Kulwa Mfaume na Ayoub Kitala. Ruvu 1-1 Simba


Dk 52 GOOOOO.....! Abdulhaman Mussa anaifungia Ruvu bao la kwanza baada ya kuichambua ngome ya Simba. Ruvu 1-1 Simba.

Dk 51 YELLOW CARD....! Ernest Ernest wa Ruvu anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Messi wa Simba.
 
Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA!

Dk 45 HALF TIME! Ruvu 0-1 Simba  
Dk 44 YELLOW CARD....! Said Madega wa Ruvu anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Abdallah Seseme. Ruvu 0-1 Simba

Dk 42 Simba inaendelea kutawala kiungo

Dk 40 Simba inapata karibu na lango la Ruvu wanapiga lakini kipa Haule anaudaka mpira. Ruvu 0-1 Simba

Dk 36 Ruvu wamepunguza kasi yao waliyoanza nayo na kutoa nafasi kwa Simba kutawala mchezo.

DK 35: Simba SC 1 - 0 Ruvu Shooting

 Dk 34 Haruna Chanongo anakosa bao baada ya mpira aliopiga kuokolewa na kipa Haule na kuwa kona.

Dk 29 Sunzu anakosa bao la wazi akishindwa kuunga krosi ya Nassor Masoud 'Chollo'.

Dk 21 Felix Sunzu anakosa bao la wazi baada ya kichwa alichopiga kuunga krosi ya Kiemba kugonga mwamba wa juu na kutoka nje ya uwanja.

Dk 18 Ruvu wanapata kona. Said Dilunga anashindwa kuunganisha mpira wa kona na kipa wa Simba, Abel Dhaira anaudaka.

Dk 14 GOOOOO......! Amri Kiemba anaipatia Simba bao la kwanza kwa shuti kali kutoka nje ya eneo la hatari. Kiemba aliuwahi mpira uliopokonywa na Felix Sunzu kutoka kwa beki wa Ruvu, Nyambiso Athuman. Ruvu 0-1 Simba.

Dk 12 Idadi ya mashabiki waliojitokeza katika uwanja huu wa taifa ni ndogo mno.

Dk 10 Bado mpira unachezwa taratibu mno huku kila timu ikimsoma mwenzake.

DK 5:Simba SC 0 - 0 Ruvu Shooting

Mpira umeanza uwanja wa Taifa - Simba SC vs Ruvu Shooting

Simba line up: Abel Dhaira, Nassor Masoud 'Chollo', Haruna Shamte, Shomari Kapombe, Mussa Mudde, William Lucian, Haruna Chanongo, Abdallah Seseme, Felix Sunzu, Amri Kiemba na Ramadhan Singano 'Messi'.

Line up: Ruvu Shooting; Benjamini Haule, Michael Pius, Baraka Nyakamande, Nyambiso Athuman, Shaban Suzan, Ernest Ernest, Said Madega, Hassan Dilunga, Abdulhaman Mussa, Said Dilunga na Raphael Keyala.


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU