Facebook Comments Box

Thursday, May 9, 2013

DAVIS MOYES NDIO KOCHA MPYA WA MANCHESTER UNITED KWA MIAKA 6 IJAYO


Hatimaye Manchester United imethibitisha DAVID MOYES ndio atakuwa kocha mpya wa kumrithi Sir Alex Ferguson kwa mkataba wa miaka 6.

Alex Ferguson jana alitangaza kustaafu kuifundisha timu hiyo aliyodumu nayo kwa takribani miaka 27 na akiwa anamtaja mrithi wake wake Fergie alisema: "Wakati tunajadili mtu wa kunirithi wote tulikubaliana kuhusu David Moyes.
"David ni mtu makini mwenye miiko ya kazi. Nimekuwa nikipenda ufanyaji wa kazi yake kwa muda mrefu na niliwahi kumshawishi mwaka 1998 ajiunge nami kuwa msaidizi wangu hapa. Akiwa kijana mdogo na akiwa ndio anaanza maisha yake ya ukocha na tangu wakati huo amekuwa akifanya kazi nzuri na klabu ya Everton.


"Hakuna swali kwamba ana kila ubora ambao tulikuwa tunautegemea kwa meneja mpya wa klabu hii.”- alisema Ferguson.

SOURSE: SHAFFIH DAUDA

Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU