Facebook Comments Box

Tuesday, April 9, 2013

TAKUKURU YAWAACHIA HURU WACHEZAJI WANNE WA AZAM BAADA YA KUSHINDWA KUTHIBITISHA TUHUMA YA RUSHWA DHIDI YAO



TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) iliyokuwa ikifanya uchunguzi wake dhidi ya wachezaji wanne wa Azam FC
waliotuhumiwa kupokea rushwa kupanga matokeo, imeshindwa kuthibitisha tuhuma hiyo.
Wachezaji ambao walikumbwa na kashfa hiyo ni kipa Deogratius Mushi 'Dida' na mabeki Erasto Nyoni, Said Morad na Aggrey Morris ambao wapo huru baada ya uchunguzi kushindwa kuthibitisha tuhuma hizo. 

Kosa la kupokea rushwa ni kinyume na Kifungu cha 15(1) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2007.
Kwa mujibu wa kifungu hicho ni kosa kwa mtu yoyote kuomba, kupokea, kushawishi au kulazamisha kupewa rushwa au kuahidi kutoa rushwa. 

Afisa Uhusiano wa TAKUKURU, Doreen Kapwani alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa Wachezaji hao walituhumiwa kupokea rushwa kwa lengo la kupanga matokeo ya mechi kati ya Azam FC na Simba SC iliyochezwa Oktoba 27, mwaka jana Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo Simba ilishinda mabao 3-1.

"Tuhuma hizo ziliwasilishwa TAKUKURU Mkoa wa Temeke Novemba 9, mwaka jana na Azam ikiwatuhumu wachezaji hao kupokea kiasi cha Sh7 milion kutoka kwa uongozi wa Simba wagawane na kupanga matokeo ya mechi hiyo."


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU