Facebook Comments Box

Wednesday, January 23, 2013

KAULI YA CHADEMA KUHUSU MANENO YA NAPE NNAUYE



Mkurugenzi wa Sera na Mafunzo wa CHADEMA, BENSON KIGAILA

CHADEMA wamesema kauli iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye kwamba Chadema kitakufa kutokana na kuwa na Sumu ya Ubaguzi haina ukweli wowote, na wamemtaka kiongozi huyo kutafakari zaidi kauli hiyo kwa maslahi ya Chama chake.

Mkurugenzi wa Sera na Mafunzo wa CHADEMA BENSON KIGAILA anasema CHADEMA haiwezi kufa kwa dhana iliyozungumzwa na Nape na badala yake Chama hicho tawala ndicho kinachoweza kufa kutokana na changamoto ikiwemo ufisadi.

Akikaririwa Benson amesema “anachodai yeye kwamba kuna ubaguzi ndani ya CHADEMA, tunataka tumwambie kwamba chama cha siasa kinakufa pale kinapoacha msingi wake, dhamiri yake na majukumu yake ya kusimamia malengo na maslahi ya Umma”

Kwenye mistari mingine Chadema imemtaka Naibu Katibu wa CCM Mwigulu Nchemba kutoa ushahidi wa kauli aliyoitoa hivi karibuni kwamba Chadema  imekuwa ikipanga mipango ya mauaji.




Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU